• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC SERUKAMBA AWATAKA WATENDAJI KUSIMAMIA MIRADI IKAMILIKE KWA WAKATI NA UBORA

Posted on: October 25th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amewahimiza Watendaji wa kila Halmashauri kuhakikisha wanasimamia miradi ya maendeleo inayotekelezwa Mkoani humo ili iweze kuishi kwa wakati.

Serukakamba ametoa maagizo hayo leo (tarehe 25 Oktoba, 2023) wakati wa ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya sekta ya afya na elimu pamoja na kusikiliza changamoto za wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Singida na Manispaa na kuhimiza Watumishi hasa Wahandisi kuhakikisha wanasimamia miradi na kuijenga kwa kiwango cha ubora kulingana na thamani ya fedha zinazotolewa na Serikali.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa licha ya kuridhishwa na miradi ya ujenzi wa vituo vya afya lakini amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri hizo pamoja na Wahandisi wa Mkoa wa Singida kuhakikisha wanatembelea miradi pamoja na kuangalia mipango kazi ya Wakandarasi ili kuharakisha utekelezaji wa ujenzi wa miradi hiyo.

Amesema kuwa Mkoa wa Singida ni kati ya Mkoa ambao unapokea fedha nyingi za maendeleo hivyo kuna kila sababu ya kusimamia miradi hiyo na kuimaliza kwa wakati uliopangwa kwa ajili ya kuanza kutumiwa na Wananchi.

Kutokana na hali hiyo amemwagiza Mhandisi wa Mkoa kuhakikisha anatembelea miradi yote na kuikagua ili kujiridhisha na utendaji wa mafundi na kueleza kuwa Mkandarasi ambaye ataonekana kuwa siyo mwaminifu asitishiwe mkataba wake na kupewa kazi Mkandarasi mwingine ambaye ataonesha kuwa ni mwaminifu.

Amesema kuwa kwa sasa miradi mbalimbali ya maendeleo Mkoani humo ikiwemo Afya, Elimu, Maji, Miundombinu ya Barabara, nishati ya Umeme pamoja na Sekta ya Kilimo inaendelea vizuri na kwa kasi sambamba na kiwango bora kwa kuzingatia thamani ya fedha.

Akizungumzia miradi ya Sekta ya Elimu, amesema kuwa inatakiwa kukamilika ndani ya mwezi wa Desemba mwaka huu ili ifikapo Januari mwaka kesho watoto wanaoanza kidato cha kwanza wakute miundombinu yote imekamilika.

Hata hivyo amesema anataraji kuanza ziara ya kutembelea kila aina ya mradi unaotekelezwa katika halmashauri zote za Wilaya Mkoani humo kwa kuhakikisha anatembelea kila mradi bila ya kuchaguliwa ni mradi gani aende.

“Nimepanga baada ya wiki moja ijayo nitatembelea Wilaya zote za Mkoa wa Singida na kufika kwenye kila mradi ili niweze kujionea utendaji wa miradi hiyo na sitahitaji kupangiwa ni mradi gani wa kutembelea, kwa kufanya hivyo nitaweza kutambua ni wapi ambapo wanakwama au wanafanya vizuri” RC Serukamba.


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.