• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC SINGIDA ATOA SIKU 30 KWA MKURUGENZI MANYONI KUPIMA NA KUWEKA ALAMA KITUO CHA WAZEE WASIOJIWEZA CHA SUKAMAHELA.

Posted on: April 8th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Halima Dendego, ametoa muda wa mwezi mmoja kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni kutuma timu ya Wataalamu wa Ardhi kwenda katika Kituo cha Makazi ya Wazee wasiojiweza cha SUKAMAHELA kwa ajili ya kupima na kuweka mipaka ya kituo hicho ili kudhibiti wananchi wasivamie eneo hilo na kuanzisha shughuli za kiuchumi ikiwemo mashamba.

Dendego ametoa kauli hiyo leo (8-Aprili-2024) baada ya kutembelea Kituo hicho na kukabidhi zawadi mbalimbali kutoka kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, ikiwemo Televisheni, friji, nguo, vyakula kwa ajili ya sikukuu ya EID.

Aidha, amesisistiza kuwa baada ya mwezi mmoja kuisha apatiwe taarifa ya utekelezaji wa agizo hilo vinginevyo atawachukulia hatua Watendaji ambao hawatatekeleza agizo hilo nia ikiwa ni kuhakikisha Wazee wanaotunzwa kwenye kituo hicho wanakaa na kuhudumiwa vizuri bila ya kubughuziwa na mtu.

“Hawa Wazee wametutumikia sana wametufanya tuwe hapa tulipo hivyo ni lazima tuwaheshimu, tuwalee na Tuwatunze” Alisisitiza DENGEGO. 

Kuhusu tatizo la kukosekana kwa huduma ya maji na umeme kwenye kituo hicho ambacho kilianzishwa mwaka 1974 kwa ajili ya kutoa huduma kwa Waathirika kwa ukoma, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka Watendaji wa Shirika la Ugavi wa Umeme - TANESCO – Mkoani Singida na wa Mamlaka ya Maji waende kwenye kituo hicho na kuweka kambi ili huduma hizo muhimu ziweze kupatikana muda wote kwenye kituo hicho.

Amefafanua kuwa siku 14 zinatosha kabisa kuweka huduma za maji na umeme kwenye kituo hicho kama hatua ya kuhakikisha wazee hao wanaishi maisha yenye staha ikilinganishwa na hali ilivyo kwa sasa.

Amesisitiza kuwa kupatikana kwa huduma hizo kutasaidia ulinzi kwa wazee hao pamoja na kuwaepusha na vitendo vya kushambuliwa na wanyama wakali hasa nyakati za usiku.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga, amesisitiza Watumishi wa Serikali wanaofanya kazi kwenye kituo hicho kufanya kazi kwa weledi, bidii na ufanisi katika kuwalinda na kuwatunza Wazee hao ili waishi maisha mazuri na yenye furaha kama watu wengine.

Amesema kuwa Wazee ni hazina na baraka hivyo lazima wahudumiwe ipasavyo na kupatia huduma za msingi kama jamii nyingine.

Mkuu wa Kituo cha Makazi ya Wazee wasiojiweza cha SUKAMAHELA Bi. Kusajo Kafuko, ametaja changamoto mbalimbali zinazokwamisha utoaji wa huduma bora kwa wazee hao ikiwemo kukosekana kwa huduma maji, umeme pamoja na kukosekana kwa mlezi wa kiume.

Ameeleza kuwa anaimani kubwa kuwa ujio wa viongozi hao utasaidia kutatua changamoto hizo ambazo zinakwamisha utoaji wa huduma bora kwa Wazee hao walemavu.

Kituo cha Makazi ya Wazee Wasiojiweza cha SUKAMAHELA wilayani MANYONI kilianzishwa mwaka 1974 kwa ajili ya kutoa huduma za tiba kwa Waathirika wa ugonjwa wa ukoma ambapo kwa sasa kinahudumia wazee kutoka Mikoa ya SINGIDA na DODOMA.


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.