• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

RC Singida awataka Wahudumu wa Afya kutoa lugha rafiki pindi wanapowahudumia Wagonjwa

Posted on: October 1st, 2022

MKUU wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba, ametoa onyo kwa wahudumu wa afya mkoani hapa watakaobainika kutoa lugha chafu kwa wazee wanapokwenda kupata matibabu kwenye vituo vilivyoainisha wakibainika watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

Alitoa onyo hilo juzi wakati wa maadhimisho ya siku ya wazee duniani yaliyofanyika kimkoa katika Wilaya ya Ikungi mkoani hapa.

Serukamba katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Jerry Muro, alisema serikali itahakikisha hakuna mzee atakayetolewa lugha mbaya na wahudumu wa afya.

Alisema serikali imedhamiria kuondoa kero ya upatikanaji wa dawa kwa wazee ambapo hivi sasa upatikanaji kwa mkoa umeongezeka kutoka asilimia 87 hadi kufikia asilimia 94 mwaka 2021/2022.

Serukamba aliagiza katika  vituo vya kutolea huduma za afya vitengwe vyumba na madirisha ya kuhudumia wazee na kutolewe matangazo yenye ujumbe unaosomeka kuwa Mpishe Mzee Ahudumiwe Kwanza'.

Kuhusu vitendo vya ukatili kwa wazee, alisema Mkoa wa Singida hautakubari kuona vitendo hivyo vinajitokeza na kuwataka wananchi kuachana na imani potofu vya kishirikina ambazo zinachochea mauaji ya wazee.

Mkuu wa Mkoa alisema hadi kufikia Juni 2022 Mkoa ulikuwa unawatambua wazee 55,920 ambapo hadi sasa wazee 10,385 ambao ni sawa na asilimia 19 wamepatiwa vitambulisho vya matibabu.

Aliagiza viongozi wakiwamo Wakuu wa Wilaya kuhakikisha wanasimamia wazee wote katika wilaya zao wanapatiwa vitambulisho vya matibabu haraka.

Kuhusu uundwaji wa mabaraza ya wazee, Serukamba alisema hilo ni agizo la serikali hivyo lazima litekelezwe na kwamba kwa sasa yapo mabaraza 637 yaliyoanzishwa mkoani hapa katika ngazi za wilaya.

"Nawaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya hakikisheni mnasimamia ili mabaraza yaliyoanzishwa yanafanya kazi kwa ufanisi kama ambavyo yameanishwa kwenye sera ya wazee ya mwaka 2013," alisema.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.