• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

SEKTA BINAFSI ZAONGEZA NGUVU KATIKA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA SINGIDA.

Posted on: September 30th, 2017

  Wadau mbalimbali wa sekta binafsi wameweza kuongeza nguvu katika kuboresha sekta ya Afya Mkoani Singida kutokana na ushirikiano mzuri ulipo baina yao na serikali.

Hayo yamebainishwa katika mkutano maalumu wa siku mbili uliohitimishwa jana Mjini Singida, ambapo viongozi wa serikali, taasisi na mashirika 15 yanayotoa huduma za Afya na Ustawi wa jamii Mkoani hapa wamejadiliana namna ya kuboresha ushirikiano baina yao.

Mratibu wa Ukimwi Mkoa wa Singida Dkt Mohamed Mbalazi amesema katika mapambano dhidi ya Ukimwi na Virusi vya Ukimwi (VVU) Mkoani hapa, Sekta binafsi zimekuwa na mchango mkubwa.

Dkt Mbalazi amesema wadau hao wameweza kutoa dawa za kupunguza makali ya VVU, tiba lishe, mafunzo kwa watoa huduma wa afya, ufuatiliaji wa watumia wa dawa za VVU pamoja na kuandaa takwimu jambo ambalo limeboresha mapambano dhidi ya VVU na Ukimwi.

“Sisi kama watendaji wa serikali tunathamini na kutambua mchango wa wadau wa sekta afya kwakuwa ni nguzo muhimu sana, mfano wadau wetu shirika la EGPAF, wametenga bilioni 1.6 kwa ajili ya mapambano dhidi ya Ukimwi na maambukizi ya VVU” Mkoani Singida”, amesema na kuongeza kuwa,

“Fedha hizo zitaongea nguvu pale ambapo kuna changamoto au bajeti inakuwa haitoshelezi, lakini pia tunaendelea kutoa wito kwa wadua wengine waendelee kuongea nguvu na wigo wa ushirikiano kwakuwa lengo letu ni moja yaani kumsaidia mwananchi apate huduma bora za afya”, amesisitiza Dkt Mbalazi.

Naye Afisa Lishe Mkoa wa Singida Teda Sinde amesema wadau wamekuwa watekelezaji wazuri wa masuala ya Lishe Mkoani hapa hasa kwa ngazi ya jamii hivyo ushirikiano kati yao umekuwa wa manufaa makubwa.

Teda amesema mkutano huo wa wadau umewawezesha watendaji na viongozi wa serikali kuelewa kwa upana zaidi kazi wanazofanya wadau pamoja na changamoto wanazopitia ili waweze kusaidiana katika kuboresha hali ya Lishe Mkoani hapa.

“Mkutano huu umeongeza na kuboresha ushirikiano baina yetu na wadau wetu ambao wengi wao wanatoa chakula lishe na elimu ya lishe kwa akina mama wajawazito, watoto wenye umri wa miezi sita mpaka 59 na akina mama wanaonyonyesha watoto chini ya miezi sita”, ameeleza Teda.

Ameongeza kuwa mkutano huo umeweza kusaidia katika kupanga mikakati ya utoaji huduma ili kuepusha wadau wanaotoa huduma ya aina moja kutoelekeza nguvu katika maeneo yanayofanana au ambayo hayana uhitaji mkubwa kuliko mengine.

Akifungua Mkutano huo Mwakilishi wa Kaimu Katibu Tawala Mkoa, Cosmas Sikali aliwataka wadau kujadili sera, sheria, kanuni, maeneo ya kipaumbele katika miradi mbalimbali, mafanikio na changamoto katika utekelezaji wa mipango mikakati inayosisitiza ushirikiano kati ya Sekta ya Umma na binafsi.

Sikali amesema endapo nguvu hizi kwa pamoja zitaunganishwa na kuratibiwa vizuri kwa kiasi kikubwa changamoto zilizopo katika sekta ya afya na ustawi wa jamii pamoja na maradhi kwa wananchi yataweza kupungua.

Ameongeza kuwa serikali peke yake haitaweza kufikia malengo ya kupunguza vifo vya watoto, akina mama wajawazito na kuweza kudhibiti magonjwa ya kuambukiza  na yasiyoambukiza, pamoja na  kuboresha afya ya mazingira  na kupata maji safi na salama bila kushirikiana na Sekta binafsi.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Salum Manyatta amesema mkutano huo umeshirikisha wadau wote muhimu wanatoa huduma za afya na ustawi wa jamii mkoa wa Singida.

Dkt Manyatta amesema mkutano huo umeweka malengo na maazimio ya pamoja na wadau wa sekta binafsi ili kuimarisha sekta ya afya na ustawi wa jamii Mkoani Singida.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.