• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

SIKU YA WANAWAKE DUNIANI YAFANA MKOANI SINGIDA

Posted on: March 8th, 2024

MKE wa Waziri Mkuu Mstaafu,Tunu Pinda ameitaka ,Serikali, wadau wa maendeleo, taasisi za Serikali na wananchi kwa ujumla   mkoani Singida kuchukua hatua za makusudi kushughulikia masuala ya ubaguzi wa kijinsia na uonevu wanavyofanyiwa Wanawake.

Wito huo ameutoa leo Machi 8, 2024 wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika kimkoa wilayani Ikungi mkoani hapa ikiwa na kauli mbiu ya wekeza kwa mwanamke kuharakisha maemdeleo ya taifa na ustawi wa jamii.Pinda alisema Tanzania inaunga mkono jitihada za kimataifa za kukuza usawa wa kijinsia  ikiwa ni pamoja na kujielekeza katika utekelezaji wa mikakati ya kufikia kizazi chenye usawa.

Alisema Serikali katika kutekeleza hilo imezindua Kamati ya ushauri ya Kitaifa ya utekelezaji wa ahadi za nchi kuhusu kizazi chenye usawa uliofanyika tarehe 16 Disemba, 2021 Jijini Dodoma ambapo Mgeni rasmi alikuwa rais Dk. Samia Suluhu Hassan.

Alisema kuanzishwa kwa kamati hiyo ni jitihada za Serikali katika kutoa msukumo wa utekelezaji wa masuala ya haki na usawa kwa wanawake na wanaume.

Nachukua nafasi hii kumpongeza Mwanamama, Amiri Jeshi Mkuu, na Raisi Dk. Samia Suluhu Hassan kwa uhodari wake wa kufanya kazi kubwa ya kuleta mabadiliko kila sekta nchini katika kuleta miradi ya maendeleo endelevu, kila mkoa hadi wilaya, kata na hata mtaa na sisi wanawake tukiwa ni wanufaaika wakubwa wa Maendeleo haya,"alisema Pinda.

Aidha, aliwapongeza wanawake wote nchini na hususani wanawake wa Mkoa wa Singida kwa upambanaji, wajasiri na hodari kwa kuchapa kazi.

Alisema lengo kuu la kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani ni kutoa fursa kwa jamii kupima utekelezaji wa maazimio, matamko, mikataba na itifaki mbalimbali za kimataifa, kikanda na kitaifa zinazohusu masuala ya maendeleo ya jinsia na uwezeshaji wanawake.

Alisema kufanya hivyo ni kuhakikisha kuwa haki za wanawake kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na kisiasa zinapatikana na zinalindwa.

"Kuadhimisha siku ya wanawake duniani ni kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa kutambua na kuthamini uwezo na mchango mkubwa wa wanawake katika kuleta maendeleo pamoja na kuelezea jitihada mbalimbali zilizofanywa na serikali na wadau mbalimbali katika kuwajengea uwezo wa kiuchumi na kijamii ili waweze kushiriki kikamilifu katika kujiletea maendeleo yao, familia zao, jamii na Taifa kwa ujumla," alisema Pinda.

Alisema kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka huu inaendana na jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita katika kuwekeza kwa wanawake kiuchumi, Kijamii, Kiafya, Elimu, Michezo na Utamadumi.hivyo ni wajibu kwa wanawake kutambua hilo na kumuunga mkono Rais kwa juhudi kubwa anazozifanya katika kuwezesha wanawake,na kuleta mabadiliko kila sekta nchini katika kuleta Miradi ya maendeleo endelevu.

Aliongeza kuwa Serikali kupitia Wizara ya Mendeleo Jamii Jinsia,Wanawake na Makundi Maalumu, inayoongozwa na Mwanamama, Doroth Gwajima  inadhamini na kuwatambua umuhimu wa wanawake wote na wajasiriamali ni miongoni mwa watu muhimu katika kukuza uchumi wa mtu moja moja na Pato la Taifa.

"Nitoe rai kwa Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri kutenga eneo maalumu katika masoko yao kwa ajili ya malezi yaani Day care Center ili kuwezesha wanawake wajasiriamali wenye watoto waweze kupata sehemu maalumu ya kunyonyesha na watoto kupata muda wa kucheza, hali hii itaboresha zaidi malezi na makuzi ya Awali ya Watoto na kuimarisha usalama wao," alisema Pinda.

Kwaupande wake Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba, amesema siku ya Mwanamke Duniani ni siku ya kutazama na kutafakari juu ya nafasi ya Mwanamke katika suala zima la maendeleo. ni siku ya kujipima na kutathimini namna gani wanawake wamewezeshwa kujitambua na kushirikishwa katika mipango ya maendeleo ya jamii kwa kushirikiana na wanaume.

"Kwa namna ya pekee katika kusheherekea siku hii sisi wanasingida tunataka kumuelezea mwanamke Jasiri muongoza njia, shupavu na mfano bora wa kuigwa sio tu na kila mwanamke bali kila mtanzania bila kujali ni mwanamke au mwanaume. Mwanamke huyo ni: Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan". Amesema RC Serukamba

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.