• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

*SINGIDA WENYEJI MAONESHO YA (7) YA MIFUKO NA PROGRAMU ZA UWEZESHAJI, WAJIPANGA KUPOKEA WAGENI NA KUHAKIKISHA YANAFANA*

Posted on: September 5th, 2024

Mkoa wa Singida umejiandaa kikamilifu kuwa wenyeji wa Maonesho ya saba (7) ya kitaifa ya mifuko ya programu za uwezeshaji wananchi kiuchumi, yatakayofanyika kuanzia Septemba 8 hadi 14, 2024, katika viwanja vya Bombadia.

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego, amesema kuwa maandalizi yote muhimu yamekamilika ili kuhakikisha wageni kutoka mikoa mbalimbali wanapokelewa na kuhudumiwa vizuri huku akisisitiza umuhimu wa wananchi wa Singida kujitokeza kwa wingi na kushiriki kikamilifu.

"Kushiriki katika maonesho haya ni fursa adimu kwa wananchi wetu wa Singida ...tujiandae kupokea wageni wengi na hii kwetu sisi ni fursa kubwa kwa wajasiriamali wetu.....," amesema RC Dendego.

Ameongeza kuwa maonesho haya yanatoa nafasi ya pekee kwa wananchi kupata uelewa wa kina kuhusu programu mbalimbali za uwezeshaji wananchi kiuchumi na jinsi wanavyoweza kunufaika nazo huku akitoa rai kwa wafanyabiashara kutoa huduma nzuri na kuepuka upandishaji wa bei usioeleweka ili wageni watamani kurudi tena Singida.

Akizungumzia hali ya ulinzi na usalama amesema, serikali ya mkoa imejipanga kikamilifu ili kuhakikisha usalama wa wageni na washiriki wote wa maonesho hayo lengo likiwa ni kuboresha nafasi ya Singida kama kituo cha mikutano na maonesho.

Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Bi. Beng’i Issa, ameeleza kuwa maonesho hayo yatakuwa na taasisi nyingi zinazotoa mikopo na ruzuku kwa ajili ya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi.

"Tuna matarajio makubwa ya watu kushiriki vizuri na kupata huduma na fursa mbalimbali kupitia programu mbalimbali na mifuko ya uwezeshaji hapa nchini. Hii itatusaidia kuinua uchumi wetu binafsi," amesema Bi. Beng’i Issa.

Maonesho hayo yatafunguliwa rasmi na Waziri wa Nchi, Sera, Bunge, na Uratibu, Mheshimiwa William Lukuvi tarehe 8 Septemba 2024, na kilele chake kitakuwa tarehe 14 Septemba 2024, ambapo Mgeni Rasmi atakuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.