• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

"Skimu ya Itagata Itigi igawanywe kwa vijana wenye uhitaji"- Serukamba

Posted on: June 22nd, 2023

Wataalamu wa Kilimo katika Halmashauri ya Wilaya ya Itigi wameshauriwa kufanya tathmini katika Skimu ya Umwagiliaji maji ya Itagata yenye ukubwa wa ekari 400 na kuigawa kwa vijana 100 au zaidi wa kata hiyo ili iweze kutumika katika uzalishaji baada ya ushirika wa eneo hilo kushindwa kuiendesha.

Ushauri huo umetolewa leo (Juni 22, 2023) na Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba, alipo hutubia Baraza la Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Itigi lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi hiyo likiwa na lengo la kujadili namna ya kufunga hoja za ukaguzi (CAG).

Amesema lengo la Skimu hiyo halijafikiwa kwa kuwa wapo baadhi ya watu ambao wameodhi mashamba huku wakilima kidogo jambo ambalo husababisha kupatikana kwa mapato kidogo ya Halmashauri na ukosefu wa ajira kwa vijana kupitia kilimo.

Aidha ameeleza kwamba namna pekee ya kuhusisha skimu hiyo ni kupitia kwenye ushirika na kuwagawia vijana wa maeneo hayo na kuwawekea utaratibu maalumu ambao utawafanya walime na wakopeshwe mbolea na mbengu ambazo watazirudisha wakivuna.

"Nashauri watafutwe vijana 100 wa kike na kiume wapewe mashamba hayo kila mmoja heka 4 Halmashauri muwakopeshe mbegu na mbolea nina hakika watalipia tozo za Tume ya Umwagiliaji mtapata kodi na uchumi wa eneo hilo utabadilika" alisema Serukamba.

RC Serukamba amesisitiza kwamba kama zoezi hilo halitafanyika skimu hiyo itaendelea kuharibika na kupoteza fedha za Serikali.

Amesema watu kutoka nje ya eneo hilo wamekuwa wakichukua mashamba makubwa ndani ya skimu hiyo huku wakilima kidogo na sehemu kubwa kuyakodisha jambo ambalo amesema halina tija kwa Halmashauri.

Awali Afisa Kilimo Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri hiyo Mkinguzi Mgalula, alisema  skimu hiyo yenye ukubwa wa ekari 400 ilijengewa miundombinu ya umwagiliaji ikiwemo bwawa lenye uwezo ujazo wa Lita Milioni moja na laki moja na mifereji yeye urefu wa Mita 550 na ilitegemewa kutumiwa na wakulima  200 lakini mpaka sasa wanao faidika ni wachache.

Hata hivyo amesema wamepokea maelekezo ya RC na muda si mrefu wataanza utekeleza wa agizo hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Kemilembe Lwota, akizungumza wakati wa kikao hicho.



Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.