• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

TAMASHA LA WANAWAKE NA UCHAGUZI SINGIDA LAFANA

Posted on: October 9th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego, amewahimiza wanawake mkoani Singida kujitokeza kugombea nafasi za uongozi katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024 na uchaguzi mkuu wa mwakani 2025 ili waweze kuwa na nafasi ya kushiriki katika ngazi za maamuzi.

Amesema hayo leo (Oktoba 9,2024) wakati akifungua kongamano la wanawake na uchaguzi wa serikali za mitaa 2024 ambalo linawashirikisha wanawake kutoka wilaya zote za mkoa huu lengo likiwa ni kuwahamasisha kujitokeza kushiriki uchaguzi mwaka huu na mwakani huku sambamba na  kampeni za uchaguzi zitakazonza rasmi  20 hadi 26 Novemba 2024 huku akiviomba vyama vyote vya siasa vitakavyoweka wagombea kufanya kampeni za kistaarabu kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu zilizopo.

"Nitumie nafasi hii kuwakumbusha kwamba 27 Novemba, 2024 ni siku ya uchaguzi wa Viongozi wetu wa Serikali za Mitaa (Wenyeviti wa Vijiji, Mitaa na Vitongoji) nchi nzima, Kaulimbiu ya uchaguzi huu inasema “Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Maendeleo ya Taifa letu, maandalizi yote ya kufanikisha uchaguzi huu yamekamilika kwa kuanza na zoezi la uandikishaji wa wapiga kura lililofanyika kuanzia tarehe 25 Septemba, 2024 hadi tarehe 01 Oktoba, 2024,"amesema Dendego.

Mheshimiwa Dendego amesema takwimu za wamawake mkoani Singida haziridhishi kwani pamoja na mkoa kuwa na idadi kubwa ya wanawake lakini wenyeviti wanawake ni 96 tu, mitaa ipo 53 wenyeviti Wanawake wapo 03 tu na jumla ya Wanawake katika nafasi ya ujumbe wa Serikali katika ngazi zote wapo 3,125. Aidha, katika nafasi ya Udiwani kati ya Kata 136 za Mkoa, Madiwani Wanawake wapo 04 tu wa kuchaguliwa.

"Takwimu hizi haziridhishi, niwaombe wanawake wenzangu kwa kuanza na uchaguzi huu wa Serikali za Mitaa twendeni tukapindue meza, tujitokeze kwa wingi kugombea nafasi zote kwani Sifa tunazo, uwezo tunao, vipawa na maarifa ya uongozi tunayo, wanawake ni Jeshi kubwa tukiamua tunaweza," amesema Dendego.

Naye Spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Kamisaa wa Sensa, nchini Anne Makinda,amewataka wanawake katika uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu wajiandikishe,wagombee nafasi za uongozi na kwenda kupiga kura  kwa kufanya maajabu katika chaguzi hizo kwa kuhakikisha wanawake wanakuwa wenyeviti wa vitongoji,vijiji na mitaa nao wanakuwa wanawake hadi dunia ishangae.


Naye Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dk.Fatuma R. Mganga, amesema kongamano hili ni kwa ajili ya kuhamasisha wanawake kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024 huku akisema uwakilishi wa wanawake katika nafasi mbalimbali za uongozi katika mkoa ww Singida ni mdogo sana kwani katika vitongoji 2000 vilivyopo mkoani Singida uwakilishi wa wanawake kwenye uongozi ni asilimia 4 tu huku vijiji 441 vilivyopo Mkoa wa Singida ni wanawake watano tu ndo walipata nafasi ya uongozi kuwa wenyeviti wa vijiji ambao ni sawa na asilimia moja

"Katika Manispaa ya Singida kuna mitaa 53 lakini wanawake waliodhubutu kuchukua fomu na kushinda ni watatu tu wakati katika nafasi ya ujumbe  kati ya nafasi 11,000 za wajumbe wa serikali za mitaa wanawake 3,125 ndo wajumbe wa serikali za mitaa," alisema.

Dk.Mganga amehitimisha kwa kusema kuwa kutokana na uwakilishi mdogo wa wanawake katika uongozi serikali ,Mkoa wa Singida  hautanyamaza juu ya suala hilo  na ndio sababu ya kuandaa kongamano ili kuwapa uelewa na ujasiri wanawake kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa serikali za mitaa.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.