• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

“TUMEPATA UHAKIKA WA MBEGU BORA YA ALIZETI, MBEGU FEKI ZILITUKATISHA TAMAA”, WAKULIMA WA ALIZETI SINGIDA.

Posted on: August 15th, 2017

  Wakulima wa zao la alizeti Mkoani Singida wamepata uhakika wa mbegu bora ya alizeti ambayo itawasaidia kuzalisha kibiashara tofauti na hapo awali walipokuwa wakipata mbegu zisiso na uhakika wa mavuno mazuri.

Mwenyekiti wa chama cha Wakulima wa Alizeti Mkoa wa Singida Athumani Sima amesema hayo mapema leo katika mkutano wa wadau wa kilimo cha alizeti ulioandaliwa na mradi wa Faida Mali kupitia Shirika la AMDT ambalo limejikita katika kusaidia wakulima wa zao hilo kupata mbegu bora.

Sima amesema hapo awali wakulima walikuwa wakinunua mbegu kwa wauzaji ambao sio waaminifu na hivyo kutovuna vizuri kutokana na mbegu hizo kuota vibaya na kutoa alizeti kidogo.

Amesema mradi wa Faida Mali umewahakikishia kuwasaidia upatikanaji wa mbegu bora na ya kisasa na hivyo kukifanya kilimo cha alizeti kuwa kama biashara nyingine ambazo zina faida kubwa.

“Hawa Faida Mali sisi tunawaamini kwakuwa wamekuwa wakishirikiana na serikali hivyo watatusaidia katika kupata mbegu bora, tulikuwa tunaumizwa na wauzaji wengine akikuuzia mbegu inaota hapa, pale haioti matokeo yake unapata hasara” amesema na kuongeza kuwa,

“Mkulima akipata Mbegu bora hiyo ni hatua ya kwanza ya mafanikio, kwakweli baadhi yetu tulianza kukata tamaa kwa kuona tunapata hasara tu, unalima alizeti miaka mingi huoni faida kubwa kama ambavyo unatarajia, lakini mradi huu umetuonyesha njia ya mafanikio, nawaomba wakulima wengine waweze kujiunga katika vikundi ili waweze kufikiwa na mradi huu au miradi mingine”, amesisitiza.

Naye Mkulima wa alizeti Kutoka kata ya Kinampundu Wilaya ya Mkalama Samwel Laida amesema utaratibu wa kununua alizeti kwa magunia ya lumbesa badala ya vipimo vya mizani unawapunja wakulima na kuwafanya warudi nyuma kiuchumi.

Laida amesema wanunuzi wa alizeti wanapakia alizeti katika magunia na kushindilia ambapo kipimo hicho sio sahihi na hakilengi kumwinua mkulima hivyo basi mradi wa Faida Mali unapowasaidia kutafuta masoko uangalie na vipimo vinavyotumika katika kununua zao hilo.

Kwa upande wake Meneja wa Mradi wa Faida Mali Mkoa wa Singida Christopher Mkondya amesema ili wakulima wazalishe kibiashara watawasaidia kupata mbegu bora na ya kisasa, kupata huduma mbalimbali za ugani, masoko na kuwaunganisha wakulima hao na huduma za kifedha.

Mkondya amesema kwa kushirikia na Autainsurance watawasaidia wakulima kupata elimu ya faida za bima na hivyo watakata bima ya mazao yao ili wakipata majanga yoyote kama vile moto, mafuriko, au mbegu kutoota wataweza kufidiwa na kuepuka hasara.

Ameongeza kuwa kupitia watoa huduma wao ambao ni Ersoko wamejipanga kutoa elimu kwa wakulima hasa kwa kuwatumia ujumbe mfupi wa maneno ambapo mkulima atapata taariza zote za kilimo cha alizeti kulingana na eneo alipo kwa kumuelekeza mbinu za kulima kisasa, muda wa kupanda, aina ya mbolea na taarifa za masoko ya mazao yake.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.