• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

TUMEWEKA MIKAKATI YA KUINUA ELIMU SINGIDA, HATUTAFELI TENA; RC NCHIMBI.

Posted on: October 26th, 2017

  Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amewahakikishia wazazi, walezi, wanafunzi na wadau wa elimu Mkoani hapa kuwa Singida haitapata ufaulu mbaya kielimu kama ilivyokuwa mwaka huu kutokana na mikakati iliyowekwa.

Dkt Nchimbi ametoa hakikisho hilo mapema jana ofisini kwake alipokutana na waandishi wa habari mara baada ya kikao cha wadau wa elimu kilichoweka mikakati ya kuinua ufaulu wa kielimu mkoani hapa.

Dkt Nchimbi amesema baada ya Mkoa wa Singida kufanya vibaya katika matokeo ya darasa la saba yaliyotoka hivi karibuni, wadau muhimu walikutana kutafakari changamoto na suluhisho ili ufaulu uwe mzuri katika mitihani ijayo.

"Mwaka jana tulikuwa wa 12 kati ya mikoa 26 tukiwa na ufaulu wa asilimia 69 lakini mwaka huu tumekuwa wa 26 na ufaulu umeshuka hadi asilimia 61, ufaulu huu haumfurahishi mtu yoyote yule", amesema na kuongeza kuwa,

"Kama Mkoa tumejua sehemu tulipokosea hivyo tumeweka mikakati, kwanza tutahakikishwa wanafunzi wa shule zote za Msingi wanapata chakula shuleni, pili walimu wote watapewa motisha ya viwanja kwa utaratibu ulio rafiki na mishahara yao, tatu tumeipatia Tume ya Utumishi wa Waalimu (TSC) miezi mitatu iweze kusikiliza kesi na malalamiko ya waalimu", amefafanua Dkt Nchimbi.

Ameongeza kuwa Mkoa utaongeza ukaguzi pamoja na kuwakutanisha wathibiti ubora na maafisa elimu ili waweze kushirikiana vizuri katika kuhakikisha elimu bora inatolewa mashuleni.

Dkt Nchimbi ameeleza kuwa baadhi ya changamoto ambazo zimeonekana kuwa kikwazo kikubwa katika kuinua ubora wa elimu ni pamaoja na kutokuwa na usimamizi na ukaguzi wa karibu wa elimu Singida huku waalimu wakiachiwa jukumu la kusimamia elimu bila kukaguliwa mara kwa mara.

Ameongeza kuwa waalimu wamekuwa na malalamiko mbalimbali lakini maafisa utumishi wameshindwa kuwasaidia hivyo kuwakatisha tamaa huku akiwataka waalimu kufundisha mada zote na zile wanazopata ugumu kutakuwa na utaratibu wa walimu 'tembezi' kutoka shule nyingine watakaowasaidia kwa kipindi hiki.

Aidha Dkt Nchimbi ameishukuru serikali kuleta mkakati wa kuboresha elimu 'EQUIP' utakaodumu kwa muda wa miaka miwili kwakuwa utasaidia kutatua baadhi ya changamoto za elimu Mkoani hapa.

Naye Afisa Elimu Mkoa wa Singid Florian Kimolo amesema amesikitishwa na hali ya ufaulu kwa matokeo ya darasa la saba mwaka huu na kueleza kuwa hali hiyo haipendezi na haikubaliki.

Kimolo amesema idara yake itaimarisha ufatiliaji pamoja na kufanyia kazi taarifa za ukaguzi kutoka kwa wadhibiti ubora wa elimu pamoja na kusimamia ufanisi wa wanafunzi katika kuzijua K. K. K tatu ambazo ni kusoma, kuhesabu na kuandika.

Ameongeza kuwa jitihada nyingine zitawekwa katika kuwaelimisha wazazi/walezi waweze kuwasimamia watoto wao katika masomo pamoja na kuwahamasisha kupenda elimu.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.