• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

Posted on: May 13th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe.Halima Dendego ameshiriki katika ukaguzi wa miradi mbali mbali katika Halmashauri ya Wilaya ya Singida ambayo inategemewa kuzinduliwa na Mwenge wa Uhuru Mkoani Singida ifikapo Julai mwaka huu.Mheshimiwa Dendego Amefanya ukaguzi huo akiambatana na Wajumbe wa kamati ya usalama wa mkoa,Kaimu KatibuTawala wa Mkoa,Mkurugenzi wa Halmashauri ya Singida,Sekretarieti ya Mkoa,Madiwani,Mwenyekiti wa kijiji,Serikali ya kijiji,Watendaji wa kijiji na wananchi.

Ziara hiyo iliyoanzia katika kijiji cha Pohama, imekagua ujenzi wa Ofisi ya Kijiji cha Pohama mradi wenye gharama ya Shilingi 66,400,000 ambapo shilingi 61,000,000 ni mapato ya ndani huku shilingi 5,400,000 ikiwa ni nguvu za wananchi Ujenzi uliokamilika mwaka 2024 unaosaidia utoaji wa huduma za utawala,kijamii na kiuchumi kwa maendeleo ya wananchi wa ndani na nje ya wilaya ili kudumisha ustawi wa jamii.

Kadhalika ukaguzi umefanyika katika ujenzi wa nyumba ya Waalimu(2 in 1) katika Shule ya Msingi Pohama mradi unaotarajiwa kusaidia waalimu kuishi katika mazingira bora,kuwawezesha kuwa karibu na vituo vyao vya kazi,kuwapunguzia gharama za maisha na kuongeza motisha na usalama wa watumishi.Mradi huu unatekelezwa kwa Shilingi 75,000,000 kwa mapato ya ndani huku 5,000,000/- ikiwa ni nguvu za wananchi.

Sambamba na hilo Mkuu wa Mkoa wa Singida amefanya ukaguzi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Ngimu katika Tarafa ya Mgori,Kata ya Ngimu,Kijiji cha Ngimu linalojumuisha ujenzi wa Jengo la wazazi,Jengo la upasuaji,Jengo la Maabara,Jengo la kufulia,vyoo matundu 8,mfumo wa maji taka,kichomea taka,placenta pit,Ash pit,na uwekaji maji safi na umeme.

Awali akisoma taarifa,Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida Bi.Ester Chaula amesema Mradi huo unaotarajiwa kukamilika June 2025 unagharimu kiasi cha Shilingi 686,779,126/-ambapo utasaidia kuboresha huduma za afya kwa wananchi wa Halmashauri ya Wilaya wenye uhitaji wa uangalizi na usaidizi maalumu kutoka katika kata ya Ngimu,Itaja na maeneo jirani.

Kadhalika ukaguzi umefanyika katika Shule mpya ya Amali iliyopo katika Tarafa ya Ilongero, Kata ya Msange yenye gharama za Shilingi 544,225,626/-ambayo inatarajiwa kuongeza idadi ya wasomi,na kuongeza ari ya kujiajiri na kuongeza ajira katikabkada ya ualimu endapo ujenzi huo ukikamilika.


Mradi wa maji katika Kijiji cha Kinyamwenda,Tarafa ya Mgori,Kata ya Itaja uliokamilika Julai 2024 ikijumuisha ujenzi wa tangi la kuhuifadhia maji lenye ujazo wa lita 100,000 kwenye mnara wa mita sita wenye gharama ya Shilingi 849,137,591 na tayari mradi huo umekamilika kwa asilimia mia moja.

Mradi huo wa maji unawawezesha wananchi wa Kijiji hicho kupata maji safi na salama ya kutosha katika matumizi ya kawaida na ya kiuchumi kadhalika kupunguza maambukizi ya magonjwa yatokanayo na ukosefu wa maji salama na kuwapatia wananchi muda wa kutosha katika shughuli za kiuchumi ikiwemo kilimo na ufugaji.

Pia ukaguzi umefanyika katika mradi wa ujenzi wa sanduku Kalavati la Mawe katika barabara inayounganisha Sagara-Pohama na Mgori ambapo ujenzi huo wenye gharama ya Shilingi 144,665,670 kutoka mfuko mkuu wa Serikali umewaepusha watumiaji kungojea masaa 2-4 kwa maji ya mvua kupita katika barabara sambamba na kuondokana na tatizo la kukwama na kushindwa kupita kwa watumiaji kutoka sehemu moja kwenda nyingine.

Mheshimiwa Dendego ametoa maelekezo  kwa Uongozi wa Wilaya kuhakikisha wanakamilisha miradi yote kwa wakati na kwa ubora wa hali ya juu ili kuipa thamani fedha na matokeo yanayoonekana katika miradi hiyo.

Kadhalika amesisitiza utunzaji wa mazingira kwa kuhakikisha usafi unazingatiwa katika maeneo yote huku akiwataka wananchi kufika kwa wingi kuupokea mwenge wa Uhuru utakapowadia wilayani hapo kwa lengo la kuzindua miradi mbalimbali itakayoleta tija kubwa kwao.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • "SINGIDA IMEJIPANGA KUONGOZA UFAULU KITAIFA":RC DENDEGO

    June 04, 2025
  • MRADI WA TACTIC KULETA NEEMA MANISPAA YA SINGIDA.

    June 02, 2025
  • "WAHITIMU MSIBWETEKE,JIENDELEZENI KATIKA FANI ILI MJIAJIRI"-DKT.MGANGA

    May 30, 2025
  • DKT.MGANGA:"WATUMISHI MSIKUBALI KUTUMIKA VIBAYA,KUWENI NA UTAMBULISHO MZURI"

    May 27, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.