• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

UMEME JUA KUCHOCHEA UPATIKANAJI WA MAJI MKOANI SINGIDA.

Posted on: February 25th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Daktari Fatuma Mganga,Ameshiriki katika ufunguzi wa programu ya siku tatu  mafunzo ya awamu ya kwanza ya kuwaongezea uwezo na maarifa  wataalam 30 wa RUWASA kupatiwa mafunzo ya usanifu,usimamizi,na uendeshaji wa miradi  inayotumia nishati ya umeme jua,utafiti na uendelezaji wa rasilimali za maji chini ya ardhi iliyoandaliwa na RUWASA na Shirika la Global Water Centre.

         Wataalamu hao wanapata mafunzo hayo kwa lengo la kwenda kuwa wakufunzi kwa wataalamu wengine zaidi ya 300 ili kuwa wabobevu katika suala la usanifu ,usimamizi,na uendelezaji wa miradi inayotumia umeme jua, utafiti na uendelezaji wa rasilimali za maji chini ya ardhi.

Akizungumza wakati akifungua mafunzo hayo,Katibu Tawala Mkoa wa Singida,amesema kuwa  mradi huo unatarajiwa kwenda kupunguza gharama za upatikaji wa  maji kwa wananchi hasa wale wa vijijini wenye uwezo mdogo na hali duni kwa kupata maji ya uhakika,kwa gharama nafuu na kwa ufanisi zaidi.

Amewaasa washiriki hao kutumia mafunzo hayo vizuri kwa lengo la kwenda kuleta mabadiliko katika jamii zetu katika maswala ya usanifu na miradi hiyo akisema  kuwa nia mafunzo hayo endapo yakifanyiwa kazi vizuri yatakwenda kuwa na manufaa makubwa kwa wananchi wote wakiwemo wale ambao wanapata changamoto ya maji.

"Ni vema tukawa wasikivu na kuelewa vizuri  kwasababu tutakachokipokea sisi ndicho kitakacho kwenda kuleta tija katika eneo kubwa zaidi ,hivyo tuhakikishe tunafahamu zaidi namna ya kutunza miradi hiyo kwani itakuwa jambo la fedheha kushindwa kuendeleza mradi huu na kupata matokeo hasi ambayo haikutarajiwa kwa kurejea katika matumizi makubwa ya gharama ikiwemo matumizi ya mafuta ya dizeli ambayo gharama yake ni kubwa ukilinganisha na gharama za umeme wa jua"amesema Daktari Mganga.

Pia katika mafunzo hayo,wataalamu wanatarajia kufanya ziara ya  katika miradi wa Kinyamwenda uliopo takribani kilometa 40 kutoka Singida Mjini kwa lengo la kujifunza zaidi namna ya kuwa na maarifa sahihi ya usimamizi wa miradi ya maji inayotumia nishati ya jua

Umuhimu wa programu hiyo ni kuongeza ufahamu wa kutosha juu ya mfumo wa matumizi ya nishati ya umeme jua katika miradi ya maji na kutambua mafanikio na changamoto juu ya miradi inayotumia nishati hiyo kwa kuainisha changamoto na utatuzi wake hususani katika miradi iliyokwama na kufahamu mitaala inayoweza kuboresha na kuendeleza ujuzi ili kuwa na utekelezaji wenye mafanikio katika miradi inayotumia mfumo wa nishati ya umeme jua na kujifunza namna ya kuongoza programu na viashiria vya mafanikio katika miradi inayotumia nishati ya umeme wa  jua kuhakikisha wananchi wanapata rasilimali maji ya kutosha na yenye viwango vya hali ya juu.


Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.