• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WAAJIRI WATAKIWA KUVIONGEZEA NGUVU VITENGO VYA MAWASILIANO SERIKALINI

Posted on: May 23rd, 2025

Makatibu Tawala Mikoa na Wakurugenzi wa Halmashauri nchini, wametakiwa kuwekeza zaidi kwenye vitengo vya mawasiliano serikalini, kwa kuviongezea nguvu za rasilimali na weledi, ili vitekeleze majukumu ya kuihabarisha jamii kuhusu utekelezaji wa miradi mbalimbali ya  maendeleo inayotekelezwa na Serikali.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mhe Mohamed Mchengerwa amesema hayo leo Mei 23, 2025, wakati akifungua Kikao Kazi cha siku mbili cha Maafisa Mawasiliano na Habari Serikalini kinachofanyikia jijini Dodoma.

Amesema, Mhe Rais Dkt Samia ameweka historia katika utekelezaji wa miradi mingi ya maendeleo hadi kwenye ngazi za msingi kwa jamii, hivyo ni muhimu kwa taasisi za umma hususani Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa, kuzifikisha taarifa sahihi za mafanikio hayo kwa wananchi, kupitia vyombo vya habari.

Mhe Mchengerwa amesema, hatua hiyo inapaswa kuchukuliwa zaidi wakati huu ambapo jitihada mbalimbali zinafanyika kupitia taasisi hizo, kukuza na kuendeleza tasnia za habari na mawasiliano kwenye maeneo yao.

Katika kikao hicho, Waziri Mchengerwa alikiri pia kuwepo kwa upungufu wa Maafisa Habari katika baadhi ya maeneo nchini, jambo linaloathiri utoaji wa taarifa kwa umma ambapo amemuagiza Katibu Mkuu kuhakikisha anafanyia kazi suala hilo kwa kuhakikisha kila Mkoa na Halmashauri unapata Maafisa Habari ili kuuhabarisha umma kwa mapana zaidi.

Kadhalika amewataka Maafisa Mawasiliano na Habari Serikalini, kuwa wabunifu na kutambua fursa walizonazo kufikisha taarifa kwa upana zaidi kwenye mifumo ya mawasiliano ya taasisi zao na vyombo vya habari vya umma na binafsi nchini.

”Ninyi ni jeshi kubwa, mpo zaidi ya 200 nchi nzima hivyo mkiamua kutekeleza majukumu yenu ipasavyo, Tanzania na dunia itapata taarifa sahihi kuhusu hatua hizi kubwa za maendeleo yanayofanyika nchini,” amesema.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe Rosemary Senyamule, ameshauri  Maafisa habari  kutangaza mafanikio  mbalimbali yaliyofikiwa katika miradi mbalimbali ya kimkakati  hata yaliyofikiwa nje ya maeneo yao kama ilivyo treni ya kisasa inayotumia (SGR), viwanja vya ndege ili wananchi wafahamu hata yale yanayofanyika katika Taifa kwa ujumla na sio katika Halmashauri pekee.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – TAMISEMI anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila, alieleza kuwa baadhi ya changamoto zinazowakabili Maafisa Habari ni pamoja na ukosefu wa vitendea kazi, rasilimali fedha na ushirikiano mdogo kutoka kwa baadhi ya viongozi wa halmashauri, hali inayorudisha nyuma jitihada za Serikali katika kutoa taarifa kwa wananchi.

Kikao kazi cha Maafisa habari kinalenga kufanya tathimini ya utendaji kazi katika maeneo mbalimbali,kubadilishana uzoefu na kujengeana uwezo kadhalika kupokea maelekezo ya Serikali juu ya utoaji wa habari za Serikali na za TAMISEMI.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA:"WATUMISHI MSIKUBALI KUTUMIKA VIBAYA,KUWENI NA UTAMBULISHO MZURI"

    May 27, 2025
  • ANUANI ZA MAKAZI KUJA NA FURSA LUKUKI ZA MAENDELEO KWA WANANCHI

    May 26, 2025
  • WANAFUNZI NI SALAMA CHINI YA MRADI WA SHULE BORA .

    May 26, 2025
  • WAAJIRI WATAKIWA KUVIONGEZEA NGUVU VITENGO VYA MAWASILIANO SERIKALINI

    May 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.