• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO SINGIDA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIDIJITALI.

Posted on: September 6th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Singida, Dkt. Fatuma Mganga, amewasisitiza wafanyabiashara wadogowadogo kutumia vizuri fursa za kidijitali kwa manufaa ya kukuza biashara zao na kuongeza kipato, akibainisha kuwa teknolojia ni nyenzo muhimu ya kufikia masoko mapya kwa haraka na kujifunza mbinu za kibiashara kwa vitendo.

Amesema hayo wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Wafanyabiashara Ndogondogo Mkoa wa Singida lililofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida, ambapo alihudhuria kama mgeni rasmi.

Dkt. Fatuma Mganga alieleza kuwa wafanyabiashara wadogowadogo ndio nguzo ya uchumi wa Mkoa wa Singida na wanapaswa kupewa kipaumbele kuwa wafayabiashwara kuwa na mvhango mkubwa kwa taifa zima.

“Serikali na sisi mkoani hapa tunatambua kundi hili katika ukuaji wa uchumi. Ninyi ndio mnaochachusha na kuuchangamsha uchumi wa Singida, hivyo tunawathamini na kuwapa kipaumbele,” alisema.

Aidha, alihimiza kila mfanyabiashara kuhakikisha anajisajili na kupata kitambulisho cha mjasiriamali ili aweze kunufaika na mikopo iliyotengwa na serikali.

“Tuhakikishe kila mmoja wetu anacho kitambulisho chake. Hakuna tajiri ambaye ameajiriwa; kila tajiri ni mfanyabiashara au mjasiriamali. Hivyo, ninyi ni watu muhimu sana katika kukuza uchumi wa mkoa wetu,” alisisitiza

                  Kwa upande wake Bi. Donatila Vedasto, Katibu Tawala Msaidizi wa Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji mkoa wa Singida, alisema kuwa lengo la kongamano hilo ni kuwaunganisha wafanyabiashara wadogowadogo na kuhamasisha usajili ili kujikwamua kiuchumi na kutambulika na serikali Pamoja na kupata fursa za mikopo kwa haraka.

“Kwa sasa tuna zaidi ya wafanyabiashara wadogowadogo 15,000 katika halmashauri saba, wengi wao wakiwa Manispaa ya Singida. Ili wanufaike na mikopo, lazima wawe na vitambulisho vya mjasiriamali,” alisema.

Bi.Vedasto aliongeza kuwa nidhamu ya fedha ni msingi wa maendeleo ya biashara. “Biashara haina ubia na mtu binafsi. Ukivitenganisha, unasonga mbele. Lakini ukivichanganya, unakwamisha maendeleo,” alisema.

                   Aidha Mratibu wa Wafanyabiashara Wadogowadogo Mkoa wa Singida, Bi.Irene Beichumila, alieleza kuwa hadi kufikia 30 Agosti 2025, jumla ya vitambulisho 880 vimesajiliwa na zaidi ya shilingi milioni 100 za mikopo zimelipwa kwa wanufaika kupitia Benki ya NMB. Hata hivyo, alibainisha changamoto ya baadhi ya wafanyabiashara kushindwa kulipia vitambulisho licha ya kujisajili.

         Baadhi ya washiriki walitoa maoni yao baada ya kongamano hilo. Semeni Chamleta Gamwai, msafirishaji bodaboda, alisema amejifunza umuhimu wa mikopo, usajili na bima. Havijawa Omary, Mwenyekiti wa Umoja wa Mama Lishe Tanzania (UMALITA), alisisitiza kuwa makongamano hayo yanawapa wanawake nafasi ya kujikita zaidi kwenye fursa za biashara. Naye Abiud Mlowezi, Katibu wa Maafisa Usafirishaji (bodaboda), alisema wameona matumaini mapya ya maendeleo kutokana na maeneo yaliyotengwa na serikali kwa ajili ya biashara.

     Kongamano hilo liliambatana na mada mbalimbali kutoka taasisi za NMB, TRA na NSSF, ambapo wafanyabiashara walipata elimu ya huduma na mikakati ya kuimarisha mitaji. Hatua hiyo inatarajiwa kuongeza kasi ya ukuaji wa biashara ndogo ndogo na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika Mkoa wa Singida, huku mwakilishi wa wizara ya Maendeleo ya jamii aliupongeza mkowa wa Singia kwa hatua hii kubwa ya kongamano hilo.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO SINGIDA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIDIJITALI.

    September 06, 2025
  • ELIMU YA WATU WAZIMA -NGUZO YA MAENDELEO ENDELEVU

    September 01, 2025
  • SINGIDA YAAZIMIA KUBORESHA HALI YA LISHE KWA WATOTO NA WATU WAZIMA.

    August 22, 2025
  • SINGIDA YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA KUFIKIA VIWANGO VYA JUU VYA USAFI WA MAZINGIRA

    August 15, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.