• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

*WAKUU WA IDARA YA KILIMO KIKAANGONI KWA KUTOWAFIKIA WAKULIMA

Posted on: November 30th, 2024

Wakuu wa Idara za Kilimo Mkoani Singida wamepewa muda wiki mbili kuhakikisha wanaandikisha wakulima katika daftari la kilimo kufikia asilimia 85 au zaidi Kwa lengo la kuhakikisha wakulima wanapata huduma ya mbegu na mbolea za ruzuku kuelekea Msimu mpya wa kilimo.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe.Halima Dendego wakati wa kikao Cha mrejesho wa wadau sekta ya kilimo kutathimini uandikishaji wa wakulima ambapo halmashauri zote za Mkoani Singida ziliwasilisha utekelezaji wa uandikishaji huo umefikia hatua gani ili kurahisisha upatikanaji wa mbegu na mbolea kuelekea Msimu wa kilimo ulionza sasa.

Akizungumza katika kikao hicho,Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe.Halima Dendego amesisitiza utendaji WA kazi Kwa bidii Kwa vitendo zaidi kuliko mikakati ya maneno isiyo ya vitendo akiwataka kutoka mijini na kuwafuata wakulima maeneo Yao mpaka vijijini wanapoishi ili kuwa rahisi kuwapata na kuwapatia elimu ya kilimo wakati wa kuwasajili.

"Msirudi nyuma,rudini kazini mkawe sababu ya wakulima wetu kufanya vizuri kwasababu tunataka kuona kilimo chenye tija kufikia Disemba 31 iwe asilimia mia moja.Tujitume wenyewe na tusisubiri maelekezo kutoka Kwa viongozi wa juu Bali tuende mpaka vijijini walipo tuwafikie Kwa urahisi na tuwape elimu ya kilimo juu ya mbegu na mbolea za ruzuku."amesema RC Dendego

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama,Mhe.Moses Machali akizungumza katika kikao hicho amesema ni wazi kuwa wanalo jukumu kubwa la kuhakikisha wakulima wanajisajili hivyo amewashauri wakurugenzi kuvutumia vizuri vyama vya ushirika na  AMCOS kurahisisha ufikiwaji mzuri na wa uhakika k a mkulima kuhudumiwa huku akisisitiza matumizi ya mfumo WA uandikishaji kiteknolojia katika simu ili kuwafikia wakulima wengi Kwa wakati mfupi.

Naye Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Kilimo na uzalishaji Bw Starnslaus Choaji amemhakikishia Mkuu wa Mkoa kufanyia kazi Yale yote yaliyoazimiwa katika kikao hicho na kuwataka wakuu wa Idara ya kilimo kukutana na kutatua changamoto zote zitakazojitokeza na kuonekana kikwazo katika kufikia malengo yaliyowekwa.

Pia amesema kuwa ni vema kuwahisha mbegu Kwa wakulima kwani mvua zinatarajiwa kuwa chini ya kiwango mwaka huu na kuainisha mawakala mbali mbali ambao wapo tayari kufanya nao kazi Kwa bei rafiki Kwa wakulima kumudu gharama na upatikanaji wa haraka.

Akizungumza baada ya kikao,Bw.Eli Jackson Muna kutoka Wilaya ya Ikungi Kata ya Ntutu amesema wakulima wanategemea mbegu na mbolea za ruzuku kuwahishwa mapema katika maeneo Yao ili kuweza kuzipata na kupanda mapema Kutokana na Hali ya hewa iliyopo huku akiomba mzunguko wa kupata huduma hiyo kuwa mfupi Ili kumfikia mkulima Kwa haraka zaidi.

Katika Mkoa wa Singida mpaka sasa wakulima 108,506 sawa na asilimia 34 wameandikishwa kati ya malengo ya wakulima 316,684 yaliyowekwa huku upatikanaji wa mbegu za alizeti ukiwa Tani 105 kati ya Tani hitajika 1206 na mahindi yakihitajika Tani 316,684.Mbolea mahitaji ni Tani 15,834 huku ikitumika Tani 3,501.





Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.