• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WAKUU WA MIKOA 11 WATOA TAMKO KUHUSU UTENDAJI WA RAIS MAGUFULI.

Posted on: June 24th, 2017

  Wakuu wa Mikoa 11 wametoa tamko la kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kutokana na kazi ya kizalendo ya kutetea na kulinda rasilimali za Watanzania kwa maslahi ya taifa zima.

Tamko hilo limetolewa jana jioni wakati wakuu hao wakihitimisha mkutano wa kawaida wa ujirani mwema baina ya mikoa hiyo ambao umefanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida.

Wakiongozwa na Mwenyekiti wa mkutano huo ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanry wakuu wa mikoa ya Singida, Rukwa, Katavi, Kagera, Dodoma, Manyara, Geita, Shinyanga, Mwanza na Kigoma wamesema wanamuunga mkono Rais na wataendelea kuzingatia maelekezo yake katika utendaji wao.

“Sisi wasaidizi wake (rais Magufuli) tutaendelea kutekeleza   na kuzingatia maelekezo katika utendaji wetu wa kila siku. Aidha, wakati wote tutakuwa pamoja na wananchi na kuwatumikia kwa kutimiza wajibu wetu kwa uaminifu, uadilifu na tutahakikisha maslahi ya wananchi na taifa yanapewa kipaumbele cha kwanza”, sehemu ya nukuu ya tamko hilo.

Katika tamko hilo pia wametoa wito kwa wananchi na wawekezaji wote halali wa ndani na nje ya nchi kumuunga mkono rais Magufuli kwa kazi nzuri ya kulinda rasilimali za taifa na wakati wote wazingatie sheria za nchi.

“Tutumie fursa nyingi zinazoendelea kutengenezwa kwa hatua hizo za kizalendo anazochukua mheshimiwa mpendwa wetu rais Dkt. Magufuli Kwa mafanikio, maendeleo na tija kuelekea Tanzania ya uchumi wa kati na uchumi wa viwanda”, sehemu nyingine ya tamko hilo.

Katika Mkutano huo Mwenyekiti Mwanry amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Singida kwa kuandaa mkutano huo na kupendekeza mikutano ya ujirani mwema ya mikoa ifanyike kikanda ili kuimarisha ulinzi na usalama wa taifa pamoja na kubadilishana uzoefu na kupeana taarifa mbalimbali za kimaendeleo.

“Tumekutana hapa kwa mapenzi ya nchi yetu na ya rais wetu Magufuli. Tuliokutana leo hii changamoto za mikoa yetu zinafanana. Changamoto hizi ni pamoja na uharibifu wa mazingira, uhaba wa mvua, kilimo cha kuhama hama na uhamiaji haramu”, amesema Mwanry na kuongeza;

“Kwa hiyo tukiacha kila Mkoa utatue changamoto hizi kivyake hatutafanikiwa kizitatua. Tumekubaliana kukutana mara kwa mara ili changamoto zinazotukabili sote tuzipatie ufumbuzi wa kudumu kwa pamoja”.

Aidha, mwenyekiti huyo amesema wamekubaliana kusimamia matumizi bora ya ardhi pia kusimamia ulinzi na usalama hasa kwa Mikoa ile iliyopo mipakani na nchi jirani.

Kwa upande wake Mwenyeji wa Mkutano huo Dkt Rehema Nchimbi amesema mkutano huo umekua wa manufaa makubwa kwa mikoa iliyohudhuria pamoja taifa kwakuwa wameweza kubadilishana mawazo kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wote.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.