• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WALIMU WA SOMO LA HISABATI WAJENGEWA UWEZO WILAYANI IRAMBA

Posted on: September 5th, 2023

Walimu wa somo la Hisabati pamoja na Viongozi wa Elimu ngazi ya Mkoa, Wilaya, Kata na shule katika Halmashauri ya Wilaya ya Iramba mkoani Singida, wamejengewa uwezo katika kuongeza mbinu mbalimbali za ufundisha wa somo hilo ili kuboresha ufundishaji na ujifunzaji wa somo la hisabati kwa lengo la kuongea ufauli.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo Mratibu msaidizi, Program ya shule Bora, kutoka Taasisi ya elimu nchini (TET), Mwesiga Kabigumila amesema Wilaya hiyo inanufaika na mafunzo hayo baada ya utafiti na uchanganuzi wa matokeo ya elimu ya msingi mwaka 2022 kuonyesha kiwango cha ufaulu somo la hilo kipo chini ya asilimia 34 ikiwa ni cha chini zaidi kuliko halmashauri zingine sita za mkoa huo.

Kabigumila, alisema mafunzo hayo yanawahusu walimu wa shule za msingi 50 wa somo la hisabati, waratibu kata 10, walimu wakuu 20 na viongozi wengine mbalimbali, wa halmashauri hiyo na mkoa wa Singida.

Kwa mujibu wa Mwesiga, mafunzo hayo yana lengo la kuboresha mbinu za ufundishaji na ujifunzaji bora, hasa kwenye mahiri zenye changamoto darasani, kwa walimu wanaofundisha hisabati ili kuleta mageuzi chanya kwa wanafunzi kufanya vyema zaidi.

“Kufanya vibaya kwa Iramba kwenye elimu ya msingi mwaka 2022, kwa kiwango cha chini sana ya asilimia 34, imekuwa ni moja ya sababu ya kuleta mafunzo haya, ili walimu wapate mbinu, zitakazowasaidia katika ufundishaji wa somo la hisabati,”alifafanua Mwesiga.

Aidha Mwesiga, aliwataka washiriki kuyaelewe mazingira ya wanafunzi wao wanaowafundisha sambamba na kutengeneza zana zinazotoka kwenye maeneo yao rafiki kwa ajili ya kuboresha na kusaidia mbinu za ufundishaji na ujifunzaji somo la hisabati.        

Kwa upande wake, Kaimu Afisa Elimu mkoa wa Singida, Sarah Mkumbo, aliwataka washiriki wazingatie mafunzo yanayotolewa na wataalamu wa elimu, ili mbinu wanazopewa ziweze kuleta tija katika somo hilo, na hivyo kuongeza ufaulu kwa wanafunzi wa wilaya ya Iramba.

Mkumbo amesema kuwa, pamoja na kazi nzuri inayofanywa na uthibiti ubora katika kutekeleza majukumu ya kuwasimamia walimu lakini mafunzo wanayofundishwa yatawajenga kiuwezo na hivyo kuwaongezea maarifa zaidi ya ufundishaji wa kazi zao za kila siku darasani.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.