• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WANAFUNZI NI SALAMA CHINI YA MRADI WA SHULE BORA .

Posted on: May 26th, 2025

Waalimu na wahandisi wametakiwa kutumia vizuri rasilimali zinazotolewa na Serikali katika kukamilisha ujenzi wa madarasa mapya na ambayo ujenzi wake unaendelea kwa viwango vilivyo bora ili kuwawezesha wanafunzi kujifunzia katika mazingira mazuri na wezeshi kwa waalimu kufundishia.

Hayo yamezungumzwa leo Mei 26,2025 Mkoani Singida katika Mafunzo ya siku mbili ya waalimu na Wahandisi kujengeana uwezo juu ya ukamilishaji wa ujenzi wa madarasa katika mradi wa 'Shule Bora' wakijadili juu ya mbinu,taratibu za kutumia kukamilisha ujenzi wa vyumba vipya vya madarasa vilivyosalia kadhalika na suala la mazingira ya Shule za Msingi.

Akifungua kikao hicho,Mwalimu Winfred Chilumba ambae ni mratibu wa Shule Bora kutoka TAMISEMI amewaasa Waalimu na Wahandisi kuhakikisha wanatumia mafunzo hayo katika kuketa tija kwa thamani ya pesa kuonekana kwa lengo la kuhakikisha shule zote zinakua vizuri kwa majengo mazuri yenye viwango zingativu.

"Katika fedha hizi za serikali tunazopokea tuhakikishe tunaonyesha uthamani wake kwa kumuunga mkono Rais wetu katika utekelezaji"amesema Mwl.Chilumba.

Naye Mratibu wa Program hiyo Mkoani Singida,Bwana Fredrick Ndahani amefafanua kuhusu Shule Bora akisema kuwa Programu hiyo inajikita katika maeneo makuu matatu ambayo ni ujifunzaji katika kuhakikisha watoto wanapata nafasi ya kuanza na kuhitimu elimu ya msingi,kadhalika katika ufundishaji katika kuwajengea waalimu uwezo wa namna nzuri ya ufundishaji katika madarasa ya awali na ya msingi na pia katika ujumuishi kwa kuhakikisha hakuna mwanafunzi anakosa kabisa haki ya kusoma bila kujali tofauti zao za kimaumbile au jinsia.

Marrystela Emanuel Ndavi, Mwalimu Mkuu Wa Shule ya Msingi Mwembemoja iliyopo Manispaa ya Singida amesema kuwa mafunzo hayo yanakwenda kuwa na tija kubwa sana kwao kwani wanajifunza mambo mbalimbali yenye manufaa katika kuhakikisha ujenzi bora wa majengo ya shule ikiwemo ujenzi unaozingatia mabadiliko ya tabianchi ikiwemo joto au baridi ili waweze kusoma katika mazingira ya aina zote.

Kadhalika ameainisha sababu za miradi mbalimbali ya ujenzi wa madarasa ya shule kukwama kuwa ni ushirikiano mdogo kutoka kwa wananchi ambao hushindwa kutoa nguvu kazi pale ambapo kazi huanza ikiwemo uchimbaji msingi,kubeba mawe nakadhalika hivyo kusuasua kwa kazi hiyo.

Programu hii  ya elimu  Kitaifa inalenga kuboresha ubora,ujumuishwaji na ujifunzaji salama kwa wasichana na wavulana katika Shule za msingi za Serikali nchini Tanzania na inajumuisha jumla ya Mikoa tisa ikiwemo mkoa wa Singida,Dodoma,Katavi,Kigoma,Mara,Rukwa,Simiyu,Pwani na Simiyu ikijumuisha Halmashauri 67,kata 1450,Shule 5,557 waalimu zaidi  49,000 na wanafunzi milioni nne.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DKT.MGANGA:"WATUMISHI MSIKUBALI KUTUMIKA VIBAYA,KUWENI NA UTAMBULISHO MZURI"

    May 27, 2025
  • ANUANI ZA MAKAZI KUJA NA FURSA LUKUKI ZA MAENDELEO KWA WANANCHI

    May 26, 2025
  • WANAFUNZI NI SALAMA CHINI YA MRADI WA SHULE BORA .

    May 26, 2025
  • WAAJIRI WATAKIWA KUVIONGEZEA NGUVU VITENGO VYA MAWASILIANO SERIKALINI

    May 23, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.