• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WANANCHI KIJIJI CHA SAGARA WAMPA MAUA RAIS SAMIA BAADA YA KUJENGEWA ZAHANATI

Posted on: October 26th, 2023

WAKAZI wa Kijiji cha Sagara Kata ya Itaja Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Mkoani Singida wamefurahishwa na ujenzi wa Zahanati ya Sagara iliyozinduliwa rasmi Oktoba 25, 2023 na Mkuu wa Mkoa huo Peter Serukamba ambapo wamemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwaondolea adha ya kutembea umbali mrefu kwa ajili ya kufuata huduma za afya.

Furaha hiyo imewapelekea Wananchi hao kutangaza shukrani zao kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kitendo cha kuelekeza fedha nyingi za miradi ya maendeleo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Zahanati hiyo ambayo itaweza kuhudumia zaidi ya watu 2000 wakazi wa Kijiji hicho.

Bila kupepese macho wananchi hao wamesema wanaendelea kumuombea kwa Mwenyezi Mungu Rais Dkt. Samia ili aendelee kuwa na afya njema na azidi kutafuta fedha kwa kujenga na kuhimalisha miradi ya maendeleo na kusisitiza kwamba amekuwa mkombozi mkubwa cha changamoto ambazo wanawake walikuwa wakizipitia.

Wakizungumza na Waandishi wa habari muda mfupi baada ya kuzinduliwa Zahanati hiyo wananchi wa Kijiji hicho wamesema kuwa kitendo cha kukosa huduma ya afya kwa ukaribu kulisababisha adha kubwa na wakati mwingine kupelekea baadhi ya akina mama kujifungulia njiani.

Hawa Mussa ni moja wa Wakunga ngazi ya Kata amesema Kijiji hicho ambacho kipo mpakani na Mkoa wa Manyara hakikuwa na huduma muhimu ya Zahanati jambo ambalo lilikuwa likisababisha usumbufu mkubwa hususani kwa akina mama waliokuwa wakihitaji huduma ya kujifungua sambamba na huduma za Watoto.

Amesema Kijiji hicho ambacho kina makabila mbalimbali wakiwepo Wamang'ati, Wanyaturu na Wabarabaigi kilikuwa na shida kubwa ya huduma hiyo ambapo kwa sasa huduma za afya kwa wananchi hao zinaenda kuimarika.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amesema, Wananchi wote wa Kijiji hicho na waliopo jirani watanufaika na Zahanati hiyo na hayo ndiyo malengo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuona Watanzania wote afya zao zinaimarika.

Hata hivyo amewaomba Wataalamu wa huduma za afya katika Zahanati hiyo kuhakikisha wanakuwa karibu na wateja wao ambao ni wagonjwa na kutenga muda wa kutosha kuzungumza nao pindi wanapokuja kupatiwa huduma ili kubaini matatizo yao kabla ya kuwapatia matibabu.

“Wagonjwa wanatakiwa kupatiwa muda wa kuzungumza nao badala ya kutumia lugha kali na za vitisho hata wakati mwingine kuwapatia majibu ambayo pengine si ugonjwa husika”. Serukamba

Serukamba amewasihi Wauguzi kutambua kuwa huduma wanayoitoa inatakiwa kutolewa kwa watu wote bila ubaguzi hususani akina mama wajawazito pamoja na lugha rafiki hasa wakati wa huduma bila kujali anayehudumiwa anaishi mazingira mazuri au si mazuri.

Pamoja na hayo Serukamba ameuagiza uongozi wa Kijiji hicho kuhakikisha wanatunza mazingira kwa kupanda miti ya kutosha kwa lengo la kuifanya Zahanati kuwa katika mazingira mazuri safi na yenye kuvuti ili hata mama mjamzito anaposindikizwa pawe na mazingira rafiki kwa wasindikizaji kupumzika.

Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskas Muragili akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Sagara Kata ya Itaja kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba wakati wa hafla ya uzindu wa Zahanati katika Kijiji cha Sagara Mkoani humo.

Mwisho.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.