• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WAZIRI MKUU AHITIMISHA ZIARA MKOANI SINGIDA, AWAAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIMAMIA FEDHA ZA MAKUSANYO

Posted on: August 6th, 2022

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, amewaagiza Wakuu wa Wilaya kuhakikisha wanasimamia Watumishi wote katika Halmashauri za Mkoa wa Singida ambao walikusanya fedha za mapato lakini hawakuzipeleka benki wanazirudisha haraka.

Ametoa agizo hilo leo kwenye kikao cha majumuisho ya ziara yake ya siku mbili mkoani hapa wakati akizungumza na Watumishi wa Halmashauri za Wilaya ya Singida, Ikungi na Halmashauri ya Manispaa ya Singida.

Alisema kumekuwa na tatizo kubwa kwenye Halmashauri nyingi nchini katika ukusanyaji wa mapato ya ndani ambapo baadhi ya Watumishi wanapokusanya fedha haziingizwi kwenye mfumo wa Serikali jambo ambalo limekuwa kero kubwa.

"Wakuu wa Wilaya hakikisheni Watumishi wanaodaiwa fedha wazirudishe haraka, Iramba, Manyoni na hata Ilongero (Halmashauri ya Wilaya ya Singida) nimepewa orodha ya Watumishi ambao wanadaiwa fedha za makusanyo," alisema.

Majaliwa alisema Rais Samia Suluhu Hassan amekuwa akisisitiza suala la ukusanyaji wa mapato na hata majuzi wakati anawaapisha wakuu wa mikoa lakini cha kushangaza baadhi ya Watumishi wa umma wamegeuka kuwa wabadhirifu.

Alisema ujanja unaofanywa na baadhi ya Watumishi kufuja fedha za makusanyo ni kwamba wanapokusanya fedha hasa wanapobaini ni nyingi wanazima mashine ili zisiingie kwenye mfumo wa Serikali.

Aidha, Waziri Mkuu amewataka Watumishi kuacha urasimu katika utendaji wa kazi kwani mambo hayo ndio yanakaribisha vitendo vya rushwa chini.

Kuhusu idara za manunuzi, alisema limekuwa ni tatizo kubwa ambapo Idara hizo zimekuwa zikiweka makadirio makubwa ya bei za manunuzi ya vifaa vya ujenzi kwenye miradi hususani inayotumia 'force account'.

Aliongeza kuwa kwenye Halmashauri kumekuwa na tatizo kubwa la usimamizi wa miradi inayotekelezwa na kwamba kuna umuhimu kwa Watumishi kuhakikisha suala hili linapewa umuhimu wa juu.

Alisisitiza suala la mahusiano kwa Watumishi wa Umma mahali pa kazi kwani kufanya hivyo kutaboresha utendaji kazi na kuleta ufanisi mkubwa katika kuwatumikia wananchi.

Aidha, alizitaka Halmashauri kuratibu vizuri suala la wafanyabiashara wadogo maarufu wamachinga ili wapewe maeneo ya kufanyia biashara zao bila usumbufu.

Waziri Mkuu (kushoto) akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Singida

Awali Waziri Mkuu aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Singida linalojengwa Ilongero katika kijiji cha Mwahango kwa thamani ya Sh. 2.7 bilioni.

Akizungumza na wananchi wa eneo hilo, alimwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Ester Chaula, kuisimamia idara ya manunuzi ili ujenzi wa jengo hilo uweze kukamilika na kuanza kutumika.

"Nimeridhishwa na ujenzi unavyoendelea, DED (Mkurugenzi wa Halmashauri) isimamie idara ya manunuzi, wasikuvuruge, mkandarasi alipwe fedha zake, " alisema.

Akiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Singida inayojengwa kwa Sh. bilioni 19.5 Waziri Mkuu, alisema ujenzi wa hospitali hiyo itakuwa mkombozi mkubwa kwa wananchi wa mkoa huu na mikoa jirani.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,(kushoto) akimpa mkono wa pongezi Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba mara baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Singida

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.