• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

WAZAZI WASIOPELEKA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM SHULENI KUCHUKULIWA HATUA

Posted on: August 14th, 2025

Viongozi wa elimu na wadau mkoani Singida wametoa wito wa mshikamano na ushirikiano katika kusimamia fedha na miradi ya elimu ili kuhakikisha ubora wa shule na mazingira salama ya kujifunzia kwa wanafunzi wote sambamba na kuhakikisha watoto wote wanapelekwa shuleni kupata elimu bila kuwaacha nyuma wale wenye mahitaji maalum wakiwemo walemavu wa viungo ili kuhakikisha makundi yote yanapata elimu iliyo bora.

Hayo yamejiri katika kikao cha tathimini ya mradi wa Shule bora kwa mwaka 2024/25 Mkoani Singida katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Singida leo Agosti 14,2025 ambacho kimehusisha Wakurugenzi wa Halmashauri,Wadhibiti ubora wa Shule,Maafisa elimu,wahasibu na Maafisa mipango kutoka Halmashauri za Mkoa wa Singida.

Akizungumza kwenye kikao cha tathmini ya utekelezaji wa programu ya Shule Bora, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Bi.Anastazia Tutuba amewataka wakurugenzi wenzake kushirikiana na wataalamu wa elimu, wahasibu, na wadhibiti ubora ili kuhakikisha fedha zinazotolewa zinapangiwa mpango kazi wenye vipaumbele na kutekelezwa kwa wakati. Amesisitiza kuwa kila mtoto ana haki ya kupata elimu bora katika mazingira salama, na kwamba mpango wa Shule Bora hauwezi kubagua jinsia wala changamoto za kimaumbile.

Kwa upande wake, Afisa Elimu wa Mkoa wa Singida Dkt.Elpidius Baganda ametoa wito kwa wazazi wenye watoto wenye mahitaji maalumu kuhakikisha wanawapeleka shule ili wapate haki yao ya msingi ya elimu. Amesema kuwa kuwatenga au kuwafungia ndani watoto hao ni kosa la jinai na hatua za kisheria zitachukuliwa kwa watakaokiuka. Amesisitiza pia kuwa shule zimeboreshwa ili kuwa rafiki kwa watoto wenye mahitaji maalumu kwa kujengwa madarasa yanayokidhi mahitaji yao.

Aidha, alieleza kuwa vipaumbele vya Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Elimu chini ya utekelezaji wa Shule Bora ni pamoja na kuimarisha uandikishaji wa wanafunzi, kuongeza idadi ya wanafunzi wanaomaliza elimu ya msingi, kuimarisha ufundishaji wa Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK), kuongeza idadi ya wanafunzi wanaoingia sekondari, kuimarisha mbinu za ufundishaji na ujifunzaji, pamoja na kusaidia serikali kufikia vigezo vya EPforR II ili kupata fedha za motisha kutoka kwa wahisani wa maendeleo.

Awali akiwasilisha mada katika kikao hicho,mratibu wa Shule Bora Mkoa wa Singida Bw. Fredrick Ndahani amewasilisha baadhi ya  matokeo ya muda mfupi yaliyokusudiwa na mradi wa Shule Bora ikiwa  ni pamoja na wazazi na jamii kushiriki kikamilifu katika kuboresha ujifunzaji, walimu kusaidiwa kufundisha elimu bora, jumuishi na katika mazingira salama, shule kusimamiwa kwa uwajibikaji kwa wadau, tawala za mikoa na mitaa kusimamia shule vizuri, pamoja na taasisi za kitaifa kusimamia utoaji wa elimu bora kwa ufanisi.

Bw. Ndahani alihitimisha kwa kusisitiza kuwa utekelezaji wa Shule Bora mkoani Singida unaendelea kuleta mabadiliko chanya katika elimu, huku akiwataka wadau wote kuendelea kushirikiana ili kuhakikisha malengo yaliyowekwa yanafikiwa.

Nae Mdau wa elimu, Bi. Zipora Semwanza, amesema matarajio baada ya kikao hicho ni kufanya maboresho pale ambapo hapakuwa na ufanisi na kuimarisha maeneo yanayoendelea vizuri huku akiahidi kuwa kutakuwa na maboresho ya miundombinu ya elimu, kuimarishwa kwa stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK), pamoja na mafunzo kwa walimu ili kuongeza ujuzi, ubunifu na mshikamano wa kiutendaji.

 Shule Bora ni programu ya kitaifa inayolenga kuboresha ubora wa elimu, ushirikishwaji, na kuhakikisha mazingira salama ya ujifunzaji kwa wanafunzi wa shule za msingi za serikali nchini Tanzania. Programu hii inafadhiliwa na Shirika la Misaada la Uingereza (UKAID) kwa idhini ya Serikali ya Uingereza na inatekelezwa katika mikoa tisa ya Tanzania Bara ikiwemo Mkoa wa Singida kwa kushirikiana na mashirika ya Cambridge Education, ADD International, International Rescue Committee (IRC) na Plan International.Kadhalika mradi huo pia unaunga mkono utekelezaji wa mpango wa Elimu wa Kitaifa wa Lipa Kulingana na Matokeo (EPforR II).

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • SINGIDA YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA KUFIKIA VIWANGO VYA JUU VYA USAFI WA MAZINGIRA

    August 15, 2025
  • WAZAZI WASIOPELEKA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM SHULENI KUCHUKULIWA HATUA

    August 14, 2025
  • SINGIDA YAADHIMISHA SIKU YA VIJANA DUNIANI – VIJANA WAASWA KUCHANGAMKIA FURSA

    August 12, 2025
  • "ARDHI NI MAISHA – TUIKUMBATIE KAMA URITHI WA VIZAZI VYETU" : RC HALIMA DENDEGO

    July 21, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.