• Wasiliana Nasi |
    • Malalamiko |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Blog |
Singida Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na dhima
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • Halmashauri
    • H/W Ikungi
    • H/W Iramba
    • H/W Itigi
    • H/W Manyoni
    • H/W Mkalama
    • H/W Singida
    • H/M Singida
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda na Biashara
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
      • Madaktari Bingwa
      • Huduma za Tiba
      • Huduma za Kinga
      • Ustawi wa Jamii
      • Afya ya Mazingira
      • Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba Wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Investment Guide
  • Kituo Cha Habari
    • Picha
    • Video
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma

"WAUMINI TUTUNZE AMANI NA UTULIVU TULIO NAO":RC DENDEGO

Posted on: June 7th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe.Halima Dendego amesisitiza umuhimu wa kutunza amani na utulivu katika Taifa letu,akisisitiza waumini kuendelea kutunza umoja na ushirikiano walio nao kama nyanja muhimu ya kuwaweka pamoja na kufanya shughuli za maendeleo yao binafsi na Taifa kwa ujumla.

Ameyasema hayo leo Juni 7,2025 katika kanisa la Unyankindi Mkoani Singida wakati alipoalikwa kama Mgeni rasmi wa Harambee ya ujenzi wa kanisa hilo  ambapo pia amewahimiza wananchi kutumia jukwaa la Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu vema kwa ajili ya kuchagua viongozi bora watakaowaletea maendeleo na kuitunza amani iliyopo hapa nchini.

“Tunaenda kwenye uchaguzi mwaka huu. Tuendelee kuomba amani. Suala hilo litufikie na liishe salama. Tuwe wamoja – iwe Waislamu, Wakristo, KKKT au dhehebu lolote – tuwe wamoja katika kulinda amani,” amesema Mhe. Dendego

Aidha, Mkuu wa Mkoa amesisitiza kuwa kusaidia kwenye ujenzi wa nyumba za ibada ni sehemu ya maandalizi ya safari ya kiroho ya kila mwanadamu hivyo ni vema kila mmoja kushiriki ili kuwezesha kazi ya Mungu kusonga mbele kadhalika na kumpa kila mmoja baraka.

“Msafiri bora ni yule aliyefunga mizigo yake sawasawa.. na mizigo hiyo ni kama hii ya ujenzi wa kanisa, kusaidia maskini, kuwajali yatima. Haya yote yanatuandalia safari njema ya kesho,” 

Naye Mchungaji Livingstone kutoka nchini Kenya,akizungumza qakati wa harambee hiyo,amewaasa Watanzania kuilinda na kuitunza vizuri amani waliyonayo kwqni ni hazina kubwa kwa nchi ya Tanzania kutokana na utulivu uliopo nchini Tanzania ambao unawapa wananchi nafasi ya kushiriki vema katika shughuli za uzalishaji ambazo  zimekua kichocheo kikubwa cha maendeleo ya mwananchi mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

“Nimesafiri nchi nyingi sana, lakini amani ya Tanzania ni ya kipekee. Tanzania mna amani sana chini ya uongozi huu. Ithaminini hiyo amani yenu,” amesema.

Kwa upande wake, Mchungaji Dr. David, Askofu Mkuu wa Kanda ya Kati wa Kanisa la Waadventista Wasabato, amemshukuru Mgeni rasmi wa Shughuli hiyo- Mkuu wa Mkoa na waumini wote wa ujumla kwa kukubali kushiriki katika harambee hiyo iliyogusa mioyo yao na kufanikiwa kufikia lengo lililotarajiwa.

Katika harambee hiyo iliyokua na lengo la kukusanya jumla ya Shilingi Milioni mia moja,imefanikisha kupata zaidi ya shilingi milioni mia moja na kuvuka lengo lililopangwa hapo awali huku Mkuu wa Mkoa akichangia kiasi cha Milioni 15.

Matangazo

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • "HAKUNA KUACHA KIPORO": RC DENDEGO AHITIMISHA MABARAZA YA MADIWANI SINGIDA AKISISITIZA UWAJIBIKAJI

    June 18, 2025
  • RC DENDEGO: “MKURUGENZI BANANA NA WANAOZALISHA HOJA MPYA – TUNATAKA KUWAWAJIBISHA KWA MATOKEO”.

    June 17, 2025
  • HALMASHAURI ZAAGIZWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI ILI KUFUTA HOJA ZA CAG

    June 16, 2025
  • WAZEE MKALAMA WAPATIWA KADI ZA MATIBABU BILA MALIPO

    June 15, 2025
  • Angalia Zote

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
Video zaidi

Viungio vya Haraka

  • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • MPANGO WA MANUNUZI MKOA WA SINGIDA
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Tovuti Muhimu

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Mkoa

Wasiliana Nasi

    SINGIDA

    Anuani: P O BOX 5 SINGIDA

    Simu: 2502170, 2502089

    Simu: 2502170, 2502089

    Barua Pepe: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.