• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

Health


OFISI YA RAIS

TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MKOA WA SINGIDA

TATHMINI YA HALI YA UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA, USTAWI WA JAMII NA LISHE MKOA WA SINGIDA

  

JUNI 2022

VIFUPISHO

AIDS                
ANC
Acquired Immunodeficiency Syndrome
Antenatal Care
AFSRH
Adolescent Friendly Sexual and Reproductive Health
APHTA
Association of Private Health Facilities in Tanzania
ART
Antiretroviral Therapy
BOQ
BCG
Bills of Quantities
Bacillus Calmette Guerin
CBHS
Community-Based HIV and AIDS Services
CBO
CECAP
Community-Based Organization
Cervical Cancer Prevention
CHMT
CT- SCAN
Council Health Management Team
Computerized Tomography SCAN
UVIKO -19
Ugonjwa wa Virusi vya Korona 2019
CTC
Care and Treatment Clinics
DM
Diabetes Mellitus
DMO
District Medical Officer
DOD
Department of Defense (America)
DOTS
Direct Observed Therapy short course
DTHO
District Tuberculosis and HIV/AIDS officer
DTLC
ECHO
LLIN
District Tuberculosis and Leprosy Coordinator
Electrocardiogram
Long Lasting Insecticidal Nets
FBO
FP
Faith-Based Organizations
Family Planning
HBC
Home-Based Care
HIV
KIHODOWE
KKKT
iCHF
ICU
IDSR
IPTp2
Human Immunodeficiency Virus
Kanisa la Kiinjili la Kilutheri
Improved Community Health Funds
Intensive Care Unit
Integrated Disease Surveillance and Response
Intermittent Preventive Treatment of Malaria
IPD
Inpatient Department
TPT
MD
Mrdt
MUAC
MRI
Tuberculosis Preventive Therapy
Medical Doctor
Malaria Rapid Diagnostic Tests
Mid- Upper Arm Circumference
Magnetic Resonance Imaging
MSD
MYA
OJT
OR- TAMISEMI
Medical Stores Department
Magonjwa Yasio ya Kuambukiza
On Job Training
Ofisi Ya Raisi- Tawala za Mikoani na Serikali za Mitaa
PMTCT
Prevention from Mother-to-Child Transmission
RCH
SACCOs
SP
TASAF
TEHAMA
TNNS
Reproductive and Child Health
Savings and Credit Cooperative Organization or Society
Sulfadoxine/Pyrimethamine
Tanzania Social Action Fund
Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
Tanzania National Nutrition Survey
UN
United Nations
UNFPA
WCD
WAVIU
United Nations Population Fund
Women Children Development
Watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI
W4SS
WHO – Recommended Four - Symptom’s screening
WHO
World Health Organization

 

 

 

 

 

 

 

 

 

TATHMINI YA HALI YA UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA, USTAWI WA JAMII NA LISHE MKOA WA SINGIDA

  • Utangulizi 

Mkoa wa Singida una wilaya tano (5) ambazo ni: Ikungi, Iramba, Manyoni, Mkalama, Singida na Halmashauri saba (7) ambazo ni: Halmashauri za Wilaya Ikungi, Iramba, Itigi, Manyoni, Mkalama, Singida na Halmashauri ya Manispaa ya Singida. Aidha, Mkoa una jumla ya Tarafa 21, Kata 136, Vijiji 441, Mitaa 53 na Vitongoji 2,298. Kwa mujibu wa taarifa ya makadirio ya idadi ya watu na makazi ya mwaka 2021, inakadiriwa Mkoa wa Singida kuwa na idadi ya wakazi wapatao 1,754,370 wanaojumuisha Wanaume 868,646 na Wanawake 885,724.

Huduma za Afya zimeendelea kutolewa kwa kuzingatia Sera, Miongozo na kanuni mbalimbali za Afya katika afua zote za Tiba na Kinga. Mkoa una jumla ya vituo 256 vya kutolea huduma za Afya ikiwa ni Hospitali 11 Vituo vya Afya 20, Zahanati 221 na kliniki 4. Rejea Kiambatisho Na 1(a) na 1(b)VIAMBATISHO 

 

 

Kiambatiusho Na 1(a) : Idadi ya Vituo vya kutolea huduma za Afya Mkoa wa Singida


Serikali

Mashirika

FBO/NGO

Binafsi

Jumla

Hospitali

5

0

6

0

11

Vituo vya Afya

18

0

1

1

20

Zahanati

189

0

25

7

221

Kliniki

0

0

1

3

4

Jumla 

212

0

33

11

256


Kiambatisho Na 1 (b): Idadi ya Vituo vya kutolea huduma za afya Mkoa wa Singida kwa umiliki 

Halmashauri
Hospitali

Vituo vya Afya 

Zahanati

Kliniki

Jumla

Serikali
Mashirika ya Dini (FBOs)
Binafsi
Serikali
Mashirika ya Dini (FBOs)
Binafsi
Serikali
Mashirika ya Dini (FBOs)
Binafsi
Serikali
Mashirika ya Dini (FBOs)
Binafsi
Iramba
1
0
0
4
0
0
33
6
1
0
0
0
45
Ikungi
0
2
0
3
0
0
37
3
0
0
0
1
46
Itigi
0
1
0
2
0
0
15
1
2
0
0
0
21
Manyoni
1
1
0
2
0
0
31
4
2
0
0
0
41
Mkalama
1
1
0
3
1
0
28
6
0
0
0
0
40
Singida DC
1
1
0
3
0
0
32
3
0
0
0
0
40
Singida MC
1
0
0
1
0
1
13
2
2
0
1
2
23
Jumla 
5
6
0
18
1
1
189
25
7
0
1
3
256

 

2.0 Hali ya Watumishi wa Afya katika Mkoa

Ikama ya Watumishi wa kada mbalimbali za Afya katika Mkoa haitoshelezi mahitaji yaliyopo katika Vituo vya kutolea huduma za Afya katika ngazi zote. Katika Mkoa kuna jumla ya Watumishi 1848 wa kada mbalimbali za Afya walioajiriwa na Serikali ambapo kada ya Uuguzi ni kada yenye watumishi wengi katika Sekta ya afya Mkoani kwani  idadi kubwa ya watumishi wakiwa 749 sawa na  40% ya Watumishi wote na hivyo kuwa ndio kada mhimili katika utoaji wa huduma za  Afya katika ngazi ya  Msingi. Aidha, kuna Madaktari Bingwa 8, Madakatari (MD) 75, Madaktari wa Meno 1,Madaktari Wasaidizi 15, Wafamasia 5, Wateknolojia dawa 10 katika Mkoa, Hali halisi ya mtawanyo wa baadhi ya Watumishi wa kada za Afya katika vituo vya kutolea huduma ni kama ifuatavyo. Rejea Kiambatisho Na 2(a) hadi 2(h)

 

  • Katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa kuna Madaktari Bingwa 7, Madaktari 26 Wauguzi 160 , Wafamasia 3, Wateknolojia Dawa 2 na Wateknolojia  Maabara  25
  • Katika ngazi ya Hospitali za Halmashauri kuna idadi ya Madaktari 23 na Madaktari Wasaidizi 15
  • Katika ngazi ya Vituo vya Afya kuna Madaktari 19 ambapo Madaktari 8 wapo Kituo cha Afya Sokoine na Madaktari 11 wapo katika Vituo vya Afya vinavyotoa huduma ya upasuaji wa dharura. Aidha vituo vya Afya 12 havina kada ya Madaktari hivyo huduma zinasimamiwa na kutolewa na Matabibu.

Pamoja na kuwepo kwa upungufu wa watumishi huduma za afya zimeendelea kutolewa vizuri ni watumishi waliopo ikiwa pamoja na Mkoa na Halmashauri kuendelea kufanya msawazo wa Watumishi katika vituo vya kutolea huduma za afya kulingana na uzito wa kazi na majukumu katika kuhudumia Wateja kwenye  kituo cha kutolea huduma za afya.

  •  HALI YA MIUNDOMBINU YA AFYA 
  •  

3.1 Miundombinu ya Utoaji wa Huduma za Afya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa.

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa inatoa huduma za rufaa kutoka kwenye hospitali za Wilaya na vituo vya kutolea huduma za Afya. Kwa sasa hospitali hii inatoa huduma za Kibingwa zifuatazo: Huduma za uzazi, Watoto, Upasuaji, Kinywa na Meno, huduma za uchunguzi (Radiolojia) na Upasuaji wa Mifupa. Katika kuiwezesha hospitali ya Rufaa ya Mkoa kutoa huduma zilizojitosheleza inatakiwa kuwa na miundombinu ifuatayo:- Jengo la wagonjwa wa nje, Wodi za Magonjwa ya Wanawake, Wodi za Magonjwa ya Wanaume, Wodi za Watoto, Jengo la Magonjwa ya dharura, Jengo la huduma za upimaji na uchunguzi, Jengo la Maabara, Jengo la mazoezi ya Viungo, Jengo la Bohari ya Dawa na Vifaa tiba, Jengo la huduma ya kinywa na meno, Jengo la huduma za afya ya macho, Jengo la upasuaji, Karakana ya matengenezo ya Vifaa tiba, Jiko la kupikia chakula cha wagonjwa

Jengo kwa ajili ya kufulia, Jengo la kuhifadhia maiti, Jengo la wagonjwa mahututi, Jengo la magonjwa ya mlipuko, Mfumo wa maji safi na maji taka na Jengo la Huduma ya Tiba na Maangalizi (CTC).

Katika miundombinu inayohitajika ili kuwezesha utoaji wa huduma za rufaa ngazi ya Mkoa, miundombinu ifuatayo inakosekana: Wodi za magonjwa ya wanaume, wodi za watoto, Jengo la mazoezi ya viungo, Jengo la Bohari ya Dawa na Vifaa tiba, Jengo la huduma ya kinywa na meno, Jengo la huduma za afya ya macho, Jengo la wagonjwa mahututi, Jengo la magonjwa ya mlipuko na Jengo la Huduma ya Tiba na Maangalizi (CTC).

Miundombinu inayojengwa kwa sasa ni pamoja: Jengo la wagonjwa Mahututi, jengo la Magonjwa ya Dharura, Bohari ya Dawa na vifaa tiba, Jengo la Maabara, Upasuaji, Wodi za magonjwa ya wanaume na wodi za watoto. Rejea Kiambatisho Na 3: (i)

 

3.2 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya katika hospitali za Wilaya

Hospitali za Wilaya pamoja na huduma zingine zinazotoa hutumika kama Hospitali za rufaa ngazi ya Wilaya. Kulingana na miongozo hospital ya ngazi ya Wilaya inatakiwa kuwa na Miundombinu ifuatayo:- Jengo la wagonjwa wa nje, Wodi za Magonjwa ya Wanawake, Wodi za Magonjwa ya Wanaume, Wodi za Watoto, Jengo la Magonjwa ya dharura, Jengo la huduma za upimaji na uchunguzi, Jengo la Maabara, Jengo la mazoezi ya Viungo, Jengo la Bohari ya Dawa na Vifaa tiba, Jengo la huduma ya kinywa na meno, Jengo la huduma za afya ya macho, Jengo la upasuaji, Karakana ya matengenezo ya Vifaa tiba, Jiko la kupikia chakula cha wagonjwa, Jengo kwa ajili ya kufulia, Jengo la kuhifadhia maiti, Jengo la wagonjwa mahututi, Jengo la magonjwa ya mlipuko, Mfumo wa maji safi na maji taka na Jengo la Huduma ya Tiba na Maangalizi (CTC). (Rejea Kiambatisho Na 3: (ii) hadi 3(vii) na kiambatisho  3b (i hadi vii)

 

3.2.1 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya katika hospitali ya Wilaya ya Manyoni

Katika miundombinu inayohitajika ili kuwezesha utoaji wa huduma za Afya kwa Hospitali ya Wilaya, miundombinu ifuatayo inakosekana: Jengo la Magonjwa ya Dharura, Jengo la mazoezi ya viungo, Jengo la wagonjwa mahututi, Jengo la magonjwa ya mlipuko, Karakana ya matengenezo ya Vifaa tiba, Jengo la wagonjwa mahututi (ICU), Kiteketeza taka (Incinerator) na Jiko la kupikia chakula cha wagonjwa.

Aidha miundombinu inayojengwa kwa sasa ni pamoja ni Jengo la Mgonjwa ya Dharura.

 

3.2.3 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya katika hospitali ya Wilaya ya Iramba

Katika miundombinu inayohitajika ili kuwezesha utoaji wa huduma za Afya kwa Hospitali ya Wilaya, miundombinu ifuatayo inakosekana: Jengo la Magonjwa ya Dharura, Jengo la mazoezi ya viungo, Jengo la wagonjwa mahututi, Jengo la magonjwa ya mlipuko, Karakana ya matengenezo ya Vifaa tiba, Jengo la huduma za Kinywa na Meno na Jiko la kupikia chakula cha wagonjwa.

Aidha miundombinu inayojengwa kwa sasa ni pamoja ni Jengo la Mgonjwa ya Dharura, Jengo la wagonjwa mahututi na Maabara.

 

3.2.3 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya katika hospitali ya Wilaya Ikungi

Hadi kufikia April, 2022 ujenzi wa miundombinu kwa hospitali ya Wilaya ilikuwa haijakamilika.  Miundombinu inayoendelea kujengwa kwa sasa ni: Jengo la Utawala, Jengo la wagonjwa wa nje, Jengo la huduma za upimaji na uchunguzi, Jengo la Maabara, Bohari ya Dawa na vifaa tiba, Jengo la huduma za Afya ya Macho, Jengo la kufulia na Jengo la Afya ya Uzazi na Mtoto.

 

3.2.4 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya katika hospitali ya Wilaya Mkalama

Katika miundombinu inayohitajika ili kuwezesha utoaji wa huduma za Afya kwa Hospitali ya Wilaya, miundombinu ifuatayo inakosekana: Jengo la Magonjwa ya Dharura, Jengo la mazoezi ya viungo, Jengo la wagonjwa mahututi, Jengo la magonjwa ya mlipuko, Karakana ya matengenezo ya Vifaa tiba, Jengo la wagonjwa mahututi (ICU), Jengo la huduma za Kinywa na Meno, Wodi za Magonjwa ya Wanaume, Wanawake na Watoto, Jengo la upasuaji, Kiteketeza taka na Jiko la kupikia chakula cha wagonjwa.

Miundombinu inayojengwa kwa sasa ni pamoja ni Jengo la Magonjwa ya Dharura, Jengo la huduma za Afya ya Macho, Wodi za Magonjwa ya Wanaume, Wanawake na Watoto.

 

3.2.5 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya katika hospitali ya Halmashauri ya Wilaya Singida

Katika miundombinu inayohitajika ili kuwezesha utoaji wa huduma za Afya kwa Hospitali ya Wilaya, miundombinu ifuatayo inakosekana: Jengo la Magonjwa ya Dharura, Jengo la mazoezi ya viungo, Jengo la wagonjwa mahututi, Jengo la magonjwa ya mlipuko, Karakana ya matengenezo ya Vifaa tiba, Jengo la wagonjwa mahututi (ICU), Jengo la huduma za Kinywa na Meno, Wodi za Magonjwa ya Wanaume, Wanawake na Watoto, Jengo la upasuaji, Kiteketeza taka na Jiko la kupikia chakula cha wagonjwa.

Miundombinu inayojengwa kwa sasa ni pamoja ni Jengo la Mgonjwa ya Dharura, na Jengo la huduma za Afya ya Macho, Wodi za Magonjwa ya Wanaume, Wanawake na Watoto.

 

 

3.2.6 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya katika hospitali ya Manispaa ya Singida

Katika miundombinu inayohitajika ili kuwezesha utoaji wa huduma za Afya kwa Hospitali ya Wilaya, miundombinu ifuatayo inakosekana: Jengo la Magonjwa ya Dharura, Jengo la mazoezi ya viungo, Jengo la magonjwa ya mlipuko, Karakana ya matengenezo ya Vifaa tiba, Jengo la wagonjwa mahututi (ICU), Jengo la Magonjwa ya Mlipuko, jengo la utawala na Kiteketeza taka (High Tech Incinerator).

 

3.3 Miundombinu ya Kutolea huduma kwenye Vituo vya Afya

Kulingana na mwongozo wa utoaji wa huduma za Afya, Kituo cha Afya kinatakiwa kuwa na Miundombinu ifuatayo: Jengo la wagonjwa wa nje, Jengo la huduma za Uzazi na Mtoto, Jengo la Maabara, Jengo la kufulia, Wodi za Magonjwa ya Wanawake, Wanaume na Watoto, Jengo la upasuaji, Jengo la mionzi, Jengo la kuhifadhia maiti, Kiteketeza taka na Miundombinu ya Maji safi na Maji taka. Rejea Kiambatisho Na 3: (viii hadi 3 xxv) na kiambatisho 3b (i hadi vii)

 

3.3.1 Miundombinu ya Kutolea huduma za Afya Vituo vya Afya Manispaa ya Singida

Katika miundombinu inayohitajika ili kuwezesha utoaji wa huduma za Afya ngazi ya Kituo, kituo cha Afya Sokoine kina upungufu wa miundombinu ifuatayo: - Wodi za magonjwa ya wanaume na watoto, Jengo la huduma za uchunguzi na Jiko la kupikia wagonjwa. Aidha Miundombinu ya jengo la huduma za uchunguzi linaendelea kujengwa.

Kituo cha Afya Mtisi kina jengo la wagonjwa wa nje ambalo linatumika kutolea huduma zote za Afya kwa wagonjwa wa nje.

Aidha kituo cha Afya Mwaja kinaendelea kujengwa baada ya kukamilika kutakuwa na miundombinu ifuatayo: jengo la wagonjwa wa nje, Maabara, jengo la Afya ya uzazi na upasuaji na kichomea taka.


3.3.2 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya Vituo vya Afya Halmashauri ya Wilaya ya Singida

Kituo cha Afya Mgori kina miundombinu yote inayohitajika kulingana na mwongozo isipokuwa: Jengo la huduma za uchunguzi (X-ray na Ultrasound), Jengo la kutunzia Dawa na vifaa tiba, Kiteketeza taka na Jiko la kupikia chakula.

Kituo cha Afya Msange kina upungufu wa miundombinu ifuatayo; Wodi za magonjwa ya wanaume na watoto, jengo la huduma za Kiuchunguzi (X-ray na Ultrasound), Kiteketeza taka, Jengo la kutunzia Dawa na Vifaa tiba na Jiko la kupikia chakula cha wagonjwa.

Kituo cha Afya Ilongero kina upungufu wa miundombinu ifuatayo; Jengo la huduma za Kiuchunguzi (X-ray na Ultrasound), Kiteketeza taka, Jengo la kutunzia Dawa na Vifaa tiba, Jengo la Upasuaji, Jengo la kufulia, Jengo la kuhifadhia maiti na Jiko la kupikia chakula cha wagonjwa.

 

3.3.3 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya Vituo vya Afya Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama

Kituo cha Afya Kinyambuli, miundombinu inayokosekana kwa ajili ya utoaji huduma za Afya ngazi ya kituo ni; Wodi za magonjwa ya wanaume na watoto, Jengo la huduma za uchunguzi (X-ray na Ultrasound), Kiteketeza taka na Jiko la kupikia chakula cha wagonjwa.

Kituo cha Afya Kinyangiri kati ya majengo yote yanayohitajika kwa ngazi ya kituo cha Afya kina majengo yafuatayo: Jengo la wagonjwa wa nje, Wodi ya magonjwa ya wanawake na Kiteketeza taka.

Kituo cha Afya Mkalama kati ya majengo yote yanayohitajika kwa ngazi ya kituo cha Afya kina majengo yafuatayo: Jengo la wagonjwa wa nje, Wodi ya magonjwa ya wanawake na Kiteketeza taka.


3.3.4 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya Vituo vya Afya Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni

Kituo cha Afya Nkonko kina upungufu wa miundombinu ifuatayo: Jengo huduma za uchunguzi, Jengo la kutunzia Dawa na Vifaa tiba, Kiteketeza taka na Jiko la kupikia chakula cha wagonjwa.

Aidha kituo cha Afya Kintinku kina upungufu wa miundombinu ifuatayo: Jengo huduma za uchunguzi, Kiteketeza taka na Jiko la kupikia chakula cha wagonjwa.

 

3.3.5 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya Vituo vya Afya Halmashauri ya Wilaya ya Itigi.

Kwa kituo cha Afya Itigi, miundombinu inayokosekana kulingana na mahitaji ni: Jengo la huduma za uchunguzi, Kiteketeza taka na Jiko la kupikia chakula cha wagonjwa.

Kituo cha Afya Mitundu kina Jengo la wagonjwa wa nje linalotumika kutoa huduma zote, Hata hivyo Miundombinu ifuatayo inaendelea kujengwa; Jengo la Maabara, Jengo la huduma ya Magonjwa ya wanawake na upasuaji, Jengo la kufulia na Jengo la kuhifadhia maiti.

 

3.3.6 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya Vituo vya Afya Halmashauri ya Wilaya ya Iramba.

Kituo cha Afya Ndago, miundombinu inayokosekana kulingana na mahitaji ni: Jengo la huduma za uchunguzi (X-ray na Ultrasound), Kiteketeza taka, Jiko la kupikia chakula cha wagonjwa. Chumba cha kuhifadhia maiti kinaendelea kujengwa.

Kituo cha Afya Kinampanda kinakosa miundombinu ifuatayo kulingana na mahitaji: Jengo la wagonjwa wa nje, Wodi za magonjwa ya wanaume na watoto, Jengo la huduma za uchunguzi na jiko la kupikia chakula cha wagonjwa.

Kituo cha Afya Kyengege kina Jengo la wagonjwa wa nje linalotumika kutolea huduma zote kwa wagonjwa wa nje, Kiteketeza taka na Mfumo ya Maji taka na maji safi.

Aidha Kituo cha Afya Mgongo, miundombinu inayokosekana kati ya inayohitajika ni: Jengo la uchunguzi, Jengo la Maabara, Jengo la kutunzia Dawa na Vifaa tiba, Jengo la kuhifadhia maiti, Jengo la kufulia na Kiteketeza taka.

 

3.3.7 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya Vituo vya Afya Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi.

Kituo cha Afya Ikungi, miundombinu inayokosekana kulingana na mahitaji ni: Jengo la huduma za uchunguzi (X-ray na Ultrasound), Kiteketeza taka chenye sifa ngazi ya kituo, Jiko la kupikia chakula cha wagonjwa, Jengo la kuhifadhia Dawa na vifaa tiba, Jengo la kufulia, Jengo la kuhifadhia.

Kituo cha Afya Ihanja, miundombinu inayokosekana kulingana na mahitaji ni: Jengo la kutunzia Dawa na vifaa tiba na Jiko la kupikia chakula cha wagonjwa. Aidha Jengo la huduma za uchunguzi (X-ray na Ultrasound) linaendelea kujengwa.

Kituo cha Afya Sepuka miundombinu inayokosekana kulingana na mahitaji ni: Jengo la huduma za Kiuchunguzi, Kiteketeza taka na Jiko la kupikia chakula cha Wagonjwa. Chumba cha upasuaji kipo lakini hakitumiki kutokana na kutokuwa na vifaa.

 

3.4 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya ngazi ya Zahanati

Huduma zinazotolewa ngazi ya zahanati kulingana na mwongozo ni: Huduma za wagonjwa wa nje, Afya ya uzazi na mtoto, chanjo na Maabara. Miundombinu inayotakiwa ili kuwezesha utoaji wa huduma hizo ni: Jengo la wagonjwa wa nje, Stoo ya kutunzia Dawa na vifaa tiba, Maabara na Jengo kwa ajili ya Afya ya Uzazi na Mtoto.

Kwa sasa huduma kwenye zahanati nyingi bado zinatolewa ndani ya Jengo moja ambalo linakuwa na huduma zote zinazotakiwa kutolewa ngazi ya zahanati. Aidha kuna baadhi ya zahanati ambazo zimeanza kujengewa miundombinu itakayowezesha kuwepo kwa mazingira mazuri ya utoaji wa huduma. Miundombinu inayoongezwa kwenye zahanati hizo ikiwa na majengo yanayojitegemea ni pamoja na: Jengo la wagonjwa wa nje, Jengo la Maabara, Jengo la Afya ya Uzazi na Mtoto, na Kiteketeza taka (De Montfort Incinerator).  Baada ya miundombinu inayoongezwa kukamilika zahanati hizi zitakuwa na uwezo wa kutoa huduma kama zinazotolewa na vituo vya Afya, hivyo zitatakiwa kuhuishwa usajili wake kufikia ngazi ya kituo cha Afya. Rejea kiambatisho  (3b i hadi vii)

 

3.4.1 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya ngazi ya zahanati Manispaa ya Singida

Kwa Manispaa ya Singida, zahanati zote zinatoa huduma za Afya ndani ya Jengo moja. Zahanati hizo pia vina vichomea taka ambavyo havina sifa. Aidha mfumo wa maji safi na maji taka una jengwa kwenye zahanati ya Unyambwa.

 

3.4.2 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya ngazi ya zahanati Halmashauri ya Singida

Halmashauri ya Wilaya ya Singida, huduma za Afya ngazi ya zahanati zinatolewa ndani ya jengo moja. Miundombinu mingine inayopatikana kwenye zahanati ni pamoja na: Vyoo vya watoa huduma, vyoo vya wagonjwa, Kichomea taka na shimo la kutupia kondo la nyuma.

 

3.4.3 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya ngazi ya zahanati Halmashauri ya Mkalama

Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama, huduma za Afya ngazi ya zahanati zinatolewa ndani ya jengo moja. Miundombinu mingine inayopatikana kwenye zahanati ni pamoja na: Vyoo vya watoa huduma, vyoo vya wagonjwa, Kichomea taka na shimo la kutupia kondo la nyuma.

Zahanati za Ilunda na Gumanga zinajengewa miundombinu itakayowezesha kutoa huduma kamili za dharura na upasuaji. Kwa sasa miundombinu inayojengwa kwenye zahanati ni pamoja na: Jengo la wagonjwa wa nje, Maabara, Kiteketeza taka (De Montfort Incinerator), na Jengo la Afya ya Uzazi na Mtoto.

 

3.4.4 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya ngazi ya zahanati Halmashauri ya Manyoni.

Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni, huduma za Afya ngazi ya zahanati zinatolewa ndani ya jengo moja. Miundombinu mingine inayopatikana kwenye zahanati ni pamoja na: Vyoo vya watoa huduma, vyoo vya wagonjwa, Kichomea taka na shimo la kutupia kondo la nyuma.

Zahanati za Chibumagwa na Sanza zinajengewa miundombinu itakayowezesha kutoa huduma kamili za dharura na upasuaji. Kwa sasa miundombinu inayojengwa kwenye zahanati ni pamoja na: Jengo la wagonjwa wa nje, Maabara, Kiteketeza taka (De Montfort Incinerator), na Jengo la Afya ya Uzazi na Mtoto. Aidha kwa zahanati ya Chibumagwa majengo yako kwenye hatua ya umaliziaji.

 

3.4.5 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya ngazi ya zahanati Halmashauri ya Itigi.

Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, huduma za Afya ngazi ya zahanati zinatolewa ndani ya jengo moja. Miundombinu mingine inayopatikana kwenye zahanati ni pamoja na: Vyoo vya watoa huduma, vyoo vya wagonjwa, Kichomea taka na shimo la kutupia kondo la nyuma.

Zahanati za Rungwa inajengewa miundombinu itakayowezesha kutoa huduma kamili za dharura na upasuaji. Kwa sasa miundombinu inayojengwa kwenye zahanati hiyo ni pamoja na: Jengo la wagonjwa wa nje, Maabara, Jengo la upasuaji na Jengo la Afya ya Uzazi na Mtoto.

 

3.4.6 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya ngazi ya zahanati Halmashauri ya Iramba.

Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni, huduma za Afya ngazi ya zahanati zinatolewa ndani ya jengo moja. Miundombinu mingine inayopatikana kwenye zahanati ni pamoja na: Vyoo vya watoa huduma, vyoo vya wagonjwa, Kichomea taka na shimo la kutupia kondo la nyuma.

Zahanati za Mwanduigembe, Mtekente, Mtoa, Tyegelo, Shelui na Kisiriri zinajengewa miundombinu itakayowezesha kutoa huduma kamili za dharura na upasuaji. Kwa sasa miundombinu inayojengwa kwenye zahanati hizo ni pamoja na: Jengo la wagonjwa wa nje, Maabara, Kiteketeza taka (De Montfort Incinerator), na Jengo la Afya ya Uzazi na Upasuaji.

 

 3.4.7 Miundombinu ya kutolea huduma za Afya ngazi ya zahanati Halmashauri ya Ikungi.

Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni, huduma za Afya ngazi ya zahanati zinatolewa ndani ya jengo moja. Miundombinu mingine inayopatikana kwenye zahanati ni pamoja na: Vyoo vya watoa huduma, vyoo vya wagonjwa, Kichomea taka na shimo la kutupia kondo la nyuma.

Zahanati za Iyumbu, Ntuntu, Misughaa na Iglansoni zinajengewa miundombinu itakayowezesha kutoa huduma kamili za dharura na upasuaji. Kwa sasa miundombinu inayojengwa kwenye zahanati hizo ni pamoja na: Jengo la wagonjwa wa nje, Maabara, Kiteketeza taka (De Montfort Incinerator), na Jengo la Afya ya Uzazi na Upasuaji

 

4.0 UPATIKANAJI WA DAWA, VIFAA TIBA, NA VITENDANISHI

Upatikanaji wa Dawa, vifaa tiba na vitendanishi vyenye ubora, kwa kiasi sahihi, kwenye kituo sahihi, kwa wakati sahihi na kwa gharama sahihi ni moja ya kiashiria cha ubora wa huduma zinazotolewa kwenye ngazi zote za vituo vya kutolea huduma za Afya. Katika kuhakikisha huduma za Bidhaa za Afya zinaboreshwa kwenye vituo, Serikali imeendelea kuwekeza kwenye eneo hili kwa kuweka mikakati mbalimbali ikiwa ni Pamoja kuongeza fedha za ruzuku kwa ajili ya kununulia bidhaa za Afya, kusimika mifumo ya kielektroniki kwa ajili ya usimamizi wa bidhaa za Afya, kutoa mafunzo ya usimamizi wa bidhaa za Afya kwa watoa huduma za Afya lengo ni kuhakikisha bidhaa za Afya zinapatikana kwa wakati wote kulingana na huduma zinazotolewa kwenye ngazi husika.

4.1 Hali halisi ya upatikanaji wa Dawa, Vifaa tiba, na vitendanishi hadi kufikia April, 2022

Hadi kufikia April, 2022 wastani wa upatikanaji wa Bidhaa za Afya Muhimu (Dawa, vifaa tiba na vitendanishi) kwa Mkoa ni 87.7%. Aidha upatikanaji wa Dawa, vifaa tiba na vitendanishi ulikuwa wa juu kwa Halmashauri ya Manispaa ya Singida 90.7% na ulikuwa chini kwa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba 85.7% kwa taarifa iliyotolewa April, 2022. (Rejea Kiambatisho Na 4A hadi 4H)  

 

 

5.0 HALI YA HUDUMA ZA TIBA 

Huduma za Tiba katika Mkoa zinatolewa na Vituo vyote vya kutolea huduma za afya vilivyopo ngazi ya Mkoa kuanzia ngazi ya Kliniki, Zahanati, Vituo vya Afya, Hospitali na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa. Rejea Kiambatisho Na: 5A 

5.1 Hospitali ya Rufaa ya Mkoa

Katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa huduma za Tiba za Kibingwa zinatolewa isipokuwa huduma za Kibingwa za Magonjwa ya ndani, Macho, Masikio, Koo na Pua, Upasuaji wa Watoto, mfumo wa Mkojo, huduma za Wagonjwa mahututi na dharura, upimaji wa CT Scan, MRI, ECHO.

Hali halisi ya utoaji wa huduma za tiba ngazi ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa

  • Huduma za Matibabu ya Kibingwa katika ubobezi wa Upasuaji, Magonjwa ya Watoto, Magonjwa ya Akinamama, Radiolojia, Kinywa na meno
  • Huduma za matibabu ya ujumla kwa wagonjwa wa nje na wagonjwa waliolazwa

Huduma ya upimaji na uchunguzi

Huduma za dawa

Huduma ya mazoezi ya Viungo (Phyisiotherapy)

Huduma ya Uuguzi na Ukunga

Huduma za Afya ya uzazi Salama

Huduma za Kliniki za Kibingwa katika Hospitali za Halmashauri

Huduma za Kliniki mbalimbali za Afya (Afya ya Macho, Kisukari, Kifua Kikuu, UKUMWI)

Huduma za kupokea na kutoa rufaa za Wagonjwa

5.2 Hospitali za Halmashauri

Katika Hospitali za halmashauri za Iramba na Manyoni huduma muhimu za Tiba zinapatikana isipokuwa huduma za Kibingwa, huduma za Wagonjwa mahututi na dharura. Hali halisi ya utoaji wa huduma Tiba katika Hospiatli  za Iramba na Manyoni ni kama ifuatavyo

  • Huduma za matibabu ya ujumla kwa wagonjwa wa nje na wagonjwa waliolazwa
  • Huduma za uzazi salama

Huduma ya upimaji na uchunguzi

Huduma ya Uuguzi na Ukunga

Huduma za dawa

Huduma za Kliniki mbalimbali za Afya (RCH, Kisukari, Kifua Kikuu, UKUMWI)

Huduma za kupokea na kutoa rufaa za Wagonjwa

Huduma za Kliniki mbalimbali za Afya (Afya ya Macho, Kisukari, Kifua Kikuu, UKUMWI)

Huduma za kupokea na kutoa rufaa za Wagonjwa

Aidha, katika Hospitali mpya za Halmashauri huduma za Tiba zinazotolewa ni kwa Wagonjwa wa Nje na Kliniki za RCH kwa sababu miondombinu inaendelea kujengwa na ununuzi wa vifaa tiba.

5.3 Huduma za Tiba ngazi ya Vituo vya Afya 

Hali halisi ya utoaji wa huduma Tiba katika Vituo vya Afya ni kama ifuatavyo

  • Huduma za matibabu ya ujumla kwa wagonjwa wa nje kwa Vituo vya Afya 20
  •  Huduma za matibabu kwa wagonjwa waliolazwa katika vituo vya afya 18 kati ya 20
  • Huduma kamili za dharura na upasuaji kwa Akinamama wajawazito katika Vituo vya afya 7 kati ya 20 vya Serikali
  • Huduma za uzazi salama katika vituo vyote

Huduma ya upimaji na uchunguzi

Huduma za dawa

Huduma za  afya ya Uzazi na Mtoto (RCH)

Huduma shirikishi za Mkoba

Huduma za kupokea na kutoa rufaa za Wagonjwa

5.4 Huduma za Tiba ngazi ya Zahanati 

Hali halisi ya utoaji wa huduma Tiba katika Zahanati ni kama ifuatavyo

  • Huduma za matibabu ya ujumla kwa wagonjwa wa nje
  • Huduma za uzazi salama katika vituo vyote

Huduma ya upimaji

Huduma za dawa

Huduma za  afya ya Uzazi na Mtoto (RCH)

Huduma shirikishi za Mkoba

Huduma ya Uuguzi na Ukunga

Huduma rufaa za Wagonjwa

Aidha pamoja na utoaji wa huduma za tiba kuna mambo mbalimbali yanayoathiri huduma hizo kama vile;

  • Uchache na uchakavu wa magari ya kubebea wagonjwa (Ambulance) kwa ajili ya rufaa ya tiba kuanzia ngazi ya Kituo cha Afya hadi hospitali za ngazi ya Wilaya. Rejea Kiambatisho 5B
  • Kutokuwepo kwa uwiano katika utoaji wa huduma za afya kwa wananchi, kuwa si kila kijiji kina Zahanati na si kila Kata ina kituo cha Afya kama Sera ya Afya inavyotaka.
  • Ukosefu na Upungufu mkubwa wa Wataalam wa Afya na raslimali kwa lengo la kupunguza idadi, aina na gharama za kutibu wagonjwa nje ya Mkoa.
  • Usimamizi usiokamili katika eneo la Tiba unaofanywa na Bodi za Afya za Hospitali na Kamati za Afya katika ngazi ya kituo cha Afya na Zahanati
  • Huduma za kusuasua za tiba ngazi ya kaya kwa magonjwa sugu na yenye kuhitaji matibabu ya muda mrefu kama ugonjwa wa Saratani, Kupooza/Kiharusi.
  • Ushiriki hafifu wa jamii kwenye huduma za utambuzi wa awali na utengamao unaosababishwa na magonjwa mbalimbali na ajali.

 

5.5 Hali halisi huduma za tiba kinywa na meno katika halmashauri.

Muongozo wa afya ya kinywa na meno wa 2020 wa utoaji wa huduma za afya ya kinywa na meno kuwa jumuishi katika vituo vya kutolea huduma za afya nchi nzima. Lengo kuu likiwa ni huduma za afya ya kinywa na meno inatolewa kuanzia ngazi ya hospitali za mikoa, halmashauri na baadhi ya vituo vya afya vya kimkakati.

Kwa mkoa wa Singida utekelezaji wa muongozo huu bado hata robo hatujaweza kuutekeleza kwa kuwa katika ngazi ya halmashauri, huduma zinatolewa katika halmashauri tatu (3)  sawa na 57% kati ya halmashauri saba (7) zinazounda mkoa wa Singida. Sababu kubwa inayosababisha baadhi ya wilaya kutokutoa huduma hizi ni kutokuwepo kwa miundombinu, wataalam wa eneo husika na vifaa vya matibabu.

Huduma zinazotolewa katika vituo hivi ni matibabu ya dharura ya maumivu (64 %), uzibaji wa meno (11.4%), huduma za kuondoa maumivu bila kung’oa (0%) upasuaji mdogo (0.2%) na utengenezaji wa meno ya bandia (0%). Huduma nyingine kama usafishaji wa meno (scalling), urekebishaji wa taya na uso, upasuaji mkubwa hazifanyiki kutokana na kutokuwepo kwa miundombinu na wataalam katika maeneo hayo. Rejea Kiambatisho 5C

 

6.0 UDHIBITI WA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA, MLIPUKO NA YASIYOKUWA YA KUAMBUKIZWA

6.1 Hali ya maambukizi ya UKIMWI 

Kiwango cha maambukizi ya UKIMWI Mkoa wa Singida ni asilimia 3.6% chini ya maambukizi ya Taifa ambayo ni 4.7%. Waviu waliogundulika na kuwepo kwenye dawa jumla yao ni 24,636 ambayo ni asilimia 0.01% ya waviu wote nchini.katika Mkoa asilimia ya waviu wanaojua hali zao ni 86%, wanaotumia dawa za ARV ni 99.5% na makali ya VVU yamefubaa kwa asilimia 97% hivyo kwenda sawa na mpango wa 95%,95%,95% wa kupambana na virusi vya UKIMWI nchini.

Mkoa una jumla ya vituo 101 vinavyotoa huduma za uangalizi na matunzo ya waviu kati ya vituo 256 vya mkoa wa Singida.Hili ni ongezeko la vituo 7 vya kutolea huduma ukilinganisha na vituo 94 kwa mwaka 2020.huduma mkoba kwa waviu nje ya vituo hivi imeendelea kutolewa kuwafikia waviu wote kwenye maeneo yao. Kati ya vituo vyote 101 ni vituo 94 tu ndivyo vinasaidiwa na Mdau (USAID-AFYA YANGU) katika shughuli mbali mbali za kliniki ya VVU. 

Katika Kipindi cha Januari 2022 hadi June 2022 jumla ya Watu 46,021 walipimwa na watu 1,369 kukutwa kuwa na maabukizi mapya. Kati ya waliokutwa na maabukizi mapya jumla ya waviu 1540 walianzishiwa huduma ya dawa za kufubaza virusi vya UKIMWI (ARV) ukilinganisha na waviu 778 walioanzishiwa huduma katika robo ya mwisho wa mwaka 2021. Waviu waliogundulika na kuwepo kwenye dawa jumla yao ni 24,636 ukilinganisha na waviu 24,021 mwaka 2021.

Hali ya Maabukizi ya Virusi kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto yameendelea kupungua kila mwaka. Mwaka 2020 ilikuwa 0.75% na 2021 ikashuka kufikia 0.73% huku mwaka huu ikitegemewa kushuka Zaidi.

 

6.2 Kifua Kikua na Ukoma 

6.2.1 Hali halisi ya utoaji wa huduma za Kifua Kikuu 

Mkoa  Singida kupitia Idara ya Afya, umeendelea kutoa huduma za Kifua  Kikuu na Ukoma ikiwa ni pamoja na  uibuaji  wa wagonjwa wa Kifua Kikuu wakiwemo wagonjwa wa Kifua Kikuu sugu na watoto chini ya miaka 15.

Mkoa unatoa huduma za uelimishaji, uchunguzi, upimaji, utoaji wa dawa kwa wagonjwa wanaogundulika kuwa na Kifua Kikuu na Ukoma. Huduma ya Kinga Tiba ya Kifua Kikuu inatolewa kwa watoto na WAVIU ambao wapo kwenye hatari ya kupata ugonjwa wa kifua Kikuu, pia kinga tiba ya Ukoma utolewa kwa wateja ambao wana hatari ya kupata ugonjwa wa Ukoma. Mkoa una jumla ya vituo vya kutolea huduma za afya 133 (51%) kati ya vituo 256 vinatoa huduma za kufuatilia matibabu ya wagonjwa wa Kifua Kikuu, asilimia 22 vinatoa huduma za upimaji wa sampuli za makohozi kwa hadubini na kati yake asilimia 11.3 vinapima kwa teknologia ya kisasa “Gene Xpert”, pia asilimia 48 vinatoa huduma za Kifua Kikuu na UKIMWI chini ya mwanvuli mmoja. Huduma hizi zote utolewa kwa wananchi bila gharama yeyote.

Kuanzia Januari hadi Desemba 2021 jumla ya wagonjwa wa Kifua Kikuu 2,600 (80%) waliibuliwa na kuanzishiwa tiba kati ya walengwa 3,230 waliotarajiwa kwa mwaka. Halikadhalika kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2022 jumla ya wagonjwa 595 (81%)  wa Kifua Kikuu waliibuliwa na kuanzishiwa matibabu kati ya walengwa 732. Rejea Kiambatisho Na: 6 (i)

Huduma za Kifua Kikuu zimeendelea kutolewa katika vituo vya kutolea huduma na kwa njia ya Mkoba na Kliniki Tembezi kwenye Maeneo ambayo hakuna vituo vya kutolea huduma.  Hali kadhalika, chanjo ya kuzuia Kifua Kikuu kwa watoto (BCG) inaendlea kutolewa kwa watoto wote.  

6.3 UKOMA

Mkoa wa Singida ni miongoni wa Mikoa ambao bado unaibua wagonjwa wa Ukoma.  Katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Desemba 2020 jumla ya wagonjwa wa Ukoma 8 waliibuliwa, mwaka 2021 wagonjwa 18 waliibuliwa na kuanzishiwa tiba. Kwa kipindi cha Januari hadi Aprili, 2022 jumla ya wagonjwa watano  (5) wa  Ukoma aliibuliwa pia wapo katika matibabu. Jumla ya wagonjwa wa Ukoma ni 31. Wote wanaendelea na matibabu na hakuna mgonjwa alieathirika na ulemavu utokanao na ugonjwa wa Ukoma. Kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo hakuna mgonjwa chini ya miaka 15 aliegundulika kuwa na Ukoma. Mkoa una jumla ya watu 340 waliopata ulemavu kutokana na makali ya ugonjwa wa Ukoma. Rejea Kiambatisho Na: 6 (ii)

6.4 MALARIA

Hali halisi ya utoaji wa huduma za Malaria

Katika kutekeleza mpango Mkakati wa Taifa wa Kudhibiti ugonjwa wa Malaria wa mwaka 2021-2025 unaolenga kuondoa maambukizi ya ugonjwa wa Malaria. Kwa sasa kiwango cha Maambukizi ya Malaria Mkoa wa Singida 2.3%, Kiwango hiki ni kidogo ukilinganisha na wastani wa kitaifa (asilimia 7.3) wa maambukizi ya malaria. Kwa Mkoa kiwango kikubwa cha malaria kipo Halmashauri ya wilaya ya Itigi (asilimia 7.7) na kiwango kidogo cha malaria kipo katika Halmashauri ya wilaya ya Singida (asilimia 0.3). Kwa sasa huduma za upimaji wa malaria zinapatikana bila malipo kwenye vituo vyote vya umma kwa kutumia kipimo cha haraka cha Malaria (mRDT). Wastani wa upatikanaji wa dawa na vitendanishi vya Malaria ni wa kuridhisha kwa asilimia 93.5 katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya hadi kufikia 30 Aprili 2022 Kwa kipindi cha Januari hadi Aprili, 2022 jumla ya wagonjwa wateja 92,751 walipimwa malaria ambapo kati yao 6,826 Waligundulika kuwa na vimelea vya malaria na walipatiwa matibabu. Rejea Kiambatisho Na. 6 (iii)

Huduma ya chandarua Kliniki inapatikana kwenye vituo vyote vya Umma na Binafsi vinavyotoa huduma za RCH vinatoa Vyandarua vyenye Viuatilifu vya muda mrefu kwa akina mama wajawazito hudhurio la kwanza na kwa watoto wenye umri wa kupata chanjo ya kwanza ya Surua. Kipindi cha Aprili, 2022 vyandarua vyenye viuatilifu 23,916 (95%) Viligawiwa kwa wajawazito na vyandarua 18,421 (94%) kwa watoto chini ya mwaka 1. Rejea Kiambatisho Na. 6 (iv)

Halmashauri za Iramba, Itigi, Manyoni na Manispaa ya Singida zimeweza kuwagawia kina mama wajawazito wote walihudhuria Kliniki hudhurio la kwanza na Halmashauri za Ikungi na Manispaa ya Singida zimeweza kuwagawia watoto wote waliopata chanjo ya Surua Rubella ya kwanza (MR1) kwa kuwa Halmashauri nyingine hazijaweza kugawa vyandarua kwa walengwa wote imepelekea Mkoa kugawa vyandarua kwa akina mama wajawazito kwa 96% na watoto 98%

6.5 UDHIBITI WA MAGONJWA YA  MLIPUKO 

Mkoa unaendelea ya kutekeleza Afua mbalimbali za udhibiti wa magonjwa ya mlipuko na kuambukizwa ambapo kwa kipindi cha mwaka 2021/2022 Mkoa umepata mlipuko wa ugonjwa mmoja (UVIKO-19) kati ya magonjwa 35 yanayotolewa taarifa kwa siku au wiki kupitia mfumo wa ufuatiliaji wa magonja ya mlipuko (IDSR)

6.6 UGONJWA WA VIRUSI VYA KORONA (UVIKO-19)

Mkoa unaendelea kutoa elimu na tahadhari za kuchukua dhidi ya Maambukizi ya UVIKO-19 ikiwa pamoja na kuzihimiza mamlaka za Halmashauri kufanya ufuatiliaji wa karibu kwenye jamii juu ya ugonjwa huu pamoja kuhamasisha wananchi kupata chanjo ya UVIKO-19. Kwa kipindi cha kuanzia 1 Mei hadi 31 Mei, 2022 kuna idadi ya wagonjwa 10 waliothibitika na kati yao mmoja (1) ni mtumishi wa Afya. Hakuna kisa cha kifo kilichoripotiwa na hadi sasa hakuna mgonjwa yeyote aliyelazwa.

6.7 MAGONJWA YASIO YA AMBUKIZA (MYA)

Hali halisi ya utoaji wa huduma kwa wagonjwa wa MYA

Mkoa una jumla ya vituo 31 vinavyotoa  huduma za  dharura na kliniki za magonjwa yasio ya ambukiza. Mkoa unategemea kuanzisha huduma za kupima na kutibu MYA kutumia mionzi  CT- SCAN, MRI, Miyonzi katika Hospitali ya rufaa ya Mkoa. Vifaa hivi vitaongeza wigo wa kufanya uchunguzi wa kina kwa wagonjwa wa MYA. Hali kadhalika Hospitali za wilaya zote zinategemea kuanzisha kliniki za ugonjwa wa selimundo. Hatua hizi ni katika kutekeleza Mpango Mkakati wa Taifa wa kukinga na kupunguza MYA nchini wa mwaka 2021 – 2026 unaoelekeza kuelimisha jamii, kuibua, kuwatibu, na kuwafuatilia wagonjwa wa magonjwa yasio ya kuambukiza.               

Kuanzia Januari hadi Desemba 2021 Jumla ya wagonjwa wa MYA 107,239 waliibuliwa na kuanzishiwa tiba katika idara ya wagonjwa wa nje. Kati yao wagonjwa wa shinikizo la damu ni 19,729, kisukari 9,138, magonjwa mengine 78,372. Wagonjwa wa ndani walikuwa 46,960(Shinikizo la damu 205, ugonjwa wa moyo 762, kisukari 750, magonjwa mengine 45243) walihudumiwa. Jumla ya vifo 1696 vilitokana na MYA. Halikadhalika kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2022 jumla ya wagonjwa 12,758 wa MYA walipewa huduma katika vituo vya afya, 4725 wakiwa wagonjwa wa kisukari. Rejea Kiambatisho Na 6 (v)

6.8 UDHIBITI WA MAGONJWA YALIYOKUWA HAYAPEWI KIPAUMBELE

Mkoa unaenendelea kutakaleza program ya utoaji wa dawa za kinga tiba kwa magonjwa yaliyokuwa Hayapewi kipaumbele kwa watoto wenye umri wa kuwa shule za Msingi ambayo inahusisha dawa za Kichocho na dawa ya Minyoo ya Tumbo. Kwa mwaka 2021 Jumla ya watoto 417642 (94.8%) kati ya watoto 440434 walipatiwa dawa za kingatiba ya minyoo ya tumbo na kichocho. Rejea Kiambatisho Na 6 (vi)

7.0 HALI HALISI YA UTEKELEZAJI AFYA YA UZAZI, MTOTO NA VIJANA

Mkoa wa Singida unalenga kuboresha huduma za Afya ya Uzazi na Mtoto kupitia idara zake za RCH. Uwekezaji katika eneo hili na mikakati mbalimbali inawekwa na Mkoa katika kupunguza magonjwa na vifo vya uzazi, watoto wachanga, watoto chini ya miaka mitano na vijana. Kwa kuzingatia "Malengo ya Maendeleo Endelevu" yanayohusiana na afya lengo namba 3, namba 5, kuhusu usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake na lengo namba 17, kuhusu ushirikiano; Mkoa umeweka mkazo katika utoaji wa huduma bora za Afya ya Uzazi kwa usawa na wakunga wenye ujuzi katika mazingira wezeshi na kwa kuiunganisha jamii na kituo cha huduma.

 

7.1 Huduma Rafiki za Kijamii na Afya ya Uzazi kwa Vijana:

Vituo vya huduma rafiki kwa Vijana vimeongezeka kutoka vituo 97 (42%) mwaka 2020 hadi kufikia vituo 221 (88.4%) mwaka 2021. Aidha, kuna ongezeko la huduma ya mkoba ya Elimu ya Afya ya uzazi, Ushauri, Stadi za Maisha na Habari katika Shule za Msingi, Sekondari, Vyuo, Kwenye Jamii  na kupitia vyombo vya habari kutoka asilimia 43 hadi kufikia asilimia 84. Huduma hii imesaidia kupunguza kiwango cha mimba na uzazi kwa Vijana kutoka asilimia 12.2(2020) hadi 11.4(2021). Rejea Kiambatisho Na 7 (i)

6.2 Huduma za Uzazi wa Mpango:

Kati ya vituo 256, ni vituo 233 sawa na asilimia 91 vinatoa huduma  ya uzazi wa mpango ambapo kiwango cha wateja wapya kimeongezeka kutoka 34% (2020) hadi 35% (2021) na wateja wa njia za muda mrefu pia kimeongezeka kutoka 37.3% (2020) hadi 56.4 % (2021). Aidha, Uzazi wa Mpango baada ya mama kujifungua (Postpartum Family Planning) unatolewa na watoa huduma 32 tu kutoka katika vituo 24 tu (10.3%) kati ya vituo 233 vinavyotoa huduma ya Uzazi wa Mpango. Huduma inajumuisha elimu ya uzazi salama ndani ya kituo na huduma za mkoba kwa kushirikiana na wadau. Rejea Kiambatisho Na: 7 (ii)

 

6.3 Afya ya Mama

  • Hali halisi ya Kliniki ya Ujauzito na kupunguza maambukizi ya VVU
  • Akina mama wajawazito wenye mimba chini ya wiki 12, walihudhuria kliniki kwa asilimia 37 (2021) kutoka 34 (2020) na waliomaliza mahudhurio yote manne wameongezeka kufikia asilimia 86 (2021) kutoka asilimia 76 (2020).
  • Kiwango cha Maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto kimepungua kutoka 0.75% (2020) hadi 0.73%(2021) na kiwango cha ushiriki wa wanaume Kliniki ya ujauzito kimebakia palepale asilimia 84.1.
  • Huduma za dharura na Uzazi salama
  • Kuna ongezeko la wajawazito waliojifungua katika vituo kufikia 88% (2021) kutoka 84% (2020) na waliozalishwa na watoa huduma wenye ujuzi kufikia 92%.
  • Kuongezeka huduma ya Msingi ya dharura (Basic Emergence Obstetric and Neonatal Care) kwenye zahanati kufikia 22% (2021) kutoka 3% (2020). Rejea Kiambatisho Na 7 (iii)
  • Kuongezeka huduma Kamili ya dharura na upasuaji (Comprehensive Emergence Obstetric and Neonatal Care) kwa vituo vya Afya kutoka 20% (2020) hadi 32% (2021) na kwa Hospitali imebakia asilimia 82 mpaka sasa. ). Rejea Kiambatisho Na 7 (iii)
  • Pamoja na huduma hizi, hali halisi inaonesha kuwa kiwango cha vifo vitokanavyo na Uzazi vimepungua kiasi kutoka vifo 46 (2020) hadi 44 (2021) na kipindi cha Januari hadi Machi, 2022 kumekuwa na jumla ya vifo 13 ambapo vifo 3 vilitokea ngazi ya Jamii. Rejea Kiambatisho Na 7(iv) na 7 (v)

6.4 Afya ya Mtoto na huduma ya Watoto wachanga:

Kiwango cha vifo vya watoto wachanga vimepungua kutoka 12.8 (2020) hadi 10.8 (2021) kati ya watoto 1000 waliozaliwa hai na vifo vya watoto chini ya miaka mitano vimepungua kufikia 7(2020) kutoka 9.2(2021) kati ya vizazi hai 1000 (Rejea Kiambatisho Na 7(iv) na 7 (v)). (ripoti ya RCH). Aidha, kiwango cha vituo vinavyotoa huduma kwa watoto wachanga sana (NICU) kimefikia asilimia 36.3. Rejea Kiambatisho Na 7 (vi) 

6.5 Saratani ya Mlango wa Kizazi:

Kipindi cha Jan-Mac, 2022 kiwango kimefikia asilimia 86 kutoka 28.9 ya wanawake walengwa wenye miaka 30-50 na wanawake 30 walidhaniwa kuwa na Saratani ya Mlango wa Kizazi ambapo walipewa rufaa kwenda Ocean Road na Bugando kwa matibabu zaidi. Huduma za uchunguzi wa saratani ya Mlango wa Kizazi hufanyika katika vituo 33(13.2%) kati ya vituo vyote 250 vinavyotoa Afya ya Uzazi na Mtoto. (Rejea Kimbatisho Na )


Masuala mtambuka katika huduma za Afya ya Uzazi

Kiwango cha vijiji vyenye watumishi 2 wa afya ya jamii wanaotoa huduma ya uzazi na mtoto na lishe katika ngazi ya jamii kimeongezeka kutoka 75% hadi 89%. Ushiriki mdogo wa jamii katika afya ya uzazi na mtoto kupitia “Jiongeze Tuwavusha Salama”.

 

 

8.0 HUDUMA ZA CHANJO 

Kwa mwaka 2021 Mkoa ulitoa huduma ya chanjo kwa watoto 69,782 sawa na 111.5% ya watoto 62,605 lengwa. Aidha, Hali ya utoaji wa huduma za chanjo kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2022 ni watoto 16,999 sawa 105.9% ya watoto 16,048 waliotakiwa kupatiwa chanjo Kimkoa. Lengo kuu la Mkoa ni kuwakinga watoto dhidi ya Magonjwa yanayozuilika kwa chanjo kama Kifua Kikuu, Dondakoo, Kifaduro, Surua, Rubella, Polio, Pepopunda, Homa ya Ini, Homa ya Uti wa Mgongo, Kuhara, Kichomi na Saratani ya Mlango wa kizazi.

Aidha, upatikanaji wa chanjo ya Surua kwa kipindi cha Januari hadi Desemba, 2021 ni 79%, kwa kipindi cha Januari hadi Machi, 2022 chanjo ya Surua ni 80% kutokana na kutokupatikana kwa chanjo za kutosha ngazi ya Taifa, na upatikanaji wa chanjo dhidi ya Kifua Kikuu kwa kipindi cha Januari hadi Desemba, 2021 ni 155% ambapo kwa  kipindi cha Januari hadi Machi, 2022 watoto waliopatiwa chanjo ya BCG ni  71% kutokana na ukosefu mkubwa wa Mabomba ya Sindano ya BCG (Rejea Kiambatisho Na 8 (i) . Muitikio wa chanjo ya wasichana dhidi ya Kansa la mlango ya mlango wa kizazi (HPV) wenye umri wa miaka 14 kwa chanjo ya Pili kwa kipindi cha Januari hadi Desemba, 2021 ni 82% na kwa kipindi cha Januari hadi Machi, 2022 kwa chanjo ya HPV ya dozi ya Pili ni 52%.

Kwa mwaka 2020 hadi 2021 huduma za chanjo zimetolewa katika vituo 218 sawa na 88% ya vituo 246, ambapo kwa mwaka 2022 Mkoa wa Singida umefanikiwa kusajili vituo vipya 12 kwa ajili ya utoaji wa huduma za chanjo kwa wananchi. Kati ya vituo 256 kwasasa vinavyotoa huduma mbalimbali za Afya ni vituo 230 sawa na 90% ya vituo vinavyotoa huduma za chanjo kwa watoto na watu wazima.

8.1 HALI HALISI YA UTOAJI WA HUDUMA YA MKOBA 

Kwa kipindi cha Januari hadi Desemba, 2021, Hali ya Utoaji wa huduma za Mkoba ni 57% na kwa kipindi cha Januari hadi Machi, 2022,hali halisi ya utoaji wa Huduma ya mkoba  ni 77%.   Aidha, kwa kipindi cha Mwaka Jana ukilinganisha na sasa hivi Mkoa umeongezeka kwa 20% ya utoaji wa huduma ya Mkoba. Rejea Kiambatisho Na 8 (ii)

 

8.2 CHANJO YA UVIKO-19

Mkoa wa Singida ni miongoni mwa Mikoa 31 nchini ambao ulianza kutoa chanjo dhidi ya UVIKO-19 tarehe 4 Agosti, 2021 katika vituo 232. Mkoa ushatoa chanjo kwa watu 116,497 (Wanawake 66,819 na Wanaume 49,678) sawa na 13% ya watu 892,060 wenye umri wa miaka 18+ na kuendelea.  Aidha, kufikia 31 Mei, 2022 watu 73,289 sawa 8% ya watu 892,060 waliokamilisha kinga kamili dhidi ya UVIKO-19 kimkoa. (Rejea Kiambatisho Na 8 (iii)

 

9.0 HALI YA UTOAJI WA HUDUMA ZA LISHE KATIKA MKOA.

Lishe bora huimarisha kinga ya mwili na huongeza uwezo wa mwili kupambana na maambukizi ya magonjwa mbalimbali. Utafiti wa Kitaifa wa masuala ya Lishe (TNNS 2018) ulionyesha kuwa; Asilimia 45.6 ya watoto chini ya miaka 5 katika Mkoa wa Singida wana hali nzuri ya lishe, asilimia 29 wana udumavu, asilimia 5.2 wana ukondefu, asilimia 18 wana uzito pungufu na asilimia 2.2 wana uzito mkubwa. Aidha kwa upande wa wanawake walio katika umri wa kuzaa; asilimia  68.1 wana hali nzuri ya lishe, asilimia 10.8 wana ukondefu na asilimia 21.1 wana uzito mkubwa. (Rejea Kiambatisho Na: 9 

Aidha,vituo vyote vya kutolea huduma za Afya  vinafanya tathmini ya hali ya lishe kwa watoto. Vituo 164 kati ya 256 sawa na asilimia 64  vinatoa huduma na matibabu ya utapiamlo, mfumo wa rufaa hutumika pindi Kituo kisichotoa huduma hiyo kinapopata mgonjwa wa utapiamlo. Mkoa una kituo maalum cha Kuhudumia watoto wenye utapiamlo, kwa kipindi cha  Oktoba 2020 hadi Juni 2022 jumla ya watoto 204 wenye utapiamlo wamehudumiwa kwenye kituo hicho. Ili kuimarisha uhakika wa chakula katika ngazi ya kaya, uhamasishaji wa upandaji na matumizi wa mazao yaliyoongezwa virutubishi (mahindi lishe, viazi lishe na maharage Lishe) pamoja na ulimaji wa mbogamboga inatolewa katika jamii. Jumla ya Shule 55 (Ikungi-19, Iramba-7, Itigi -4, Singida DC 19 na Mkalama 6) zimepata mbegu za maharage Lishe.

Elimu ya lishe inatolewa kupitia majukwaa mbalimbali  ikiwa ni pamoja na kutumia redio standard, kufikisha jumbe tofauti tofauti za lishe; kufanya mapishi darasa kwenye ngazi ya kituo na  jamii ili kufikisha ujumbe kwa makundi mbalimbali yaliopo kwenye jamii juu ya   ya umuhimu wa lishe bora. Aidha vijiji pia huadhimisha siku ya afya na lishe kila robo na kwa kipindi cha Januari-Machi 2022, vijiji/ mitaa 383 (74.8%) kati ya 512 viliadhimisha siku ya afya na Lishe ya kijiji.

10.0 HALI YA UJENZI NA MATUMIZI YA VYOO KATIKA KAYA KUFIKIA MACHI 2022

Mkoa kupitia Halmashauri unaendelea na uhamasishaji wa ujenzi na matumizi ya vyoo bora  kwa kila kaya na taasisi katika jamii ikiwa ni Pamoja na kuhamasisha jamii  kunawa mikono kwa maji safi tiririka na sabuni baada ya kutoka chooni ili kupunguza Magonjwa ya kuambukiza ambayo yanaweza kuathiri jamii kama Kipindupindu, Kuhara, Kuhara damu, Homa ya Matumbo, Minyoo na Trakoma. Hadi kufikia Machi, 2022, kaya zenye vyoo katika Mkoa ni 329,818 (99.2%) na kaya ambazo hazina vyoo ni 2,656 (0.8%) na kaya zenye vifaa vya kunawia mikono nje ya choo ni 70,630 (21.2%). Hali ya uwepo wa vyoo kwa kila Halmashauri inaonekana kwenye kiambatisho Na: 10 (i). Aidha kiwango cha kaya zenye vyoo kimeongezeka kutoka asilimia 79.9 (2015) hadi asilimia 99.2 (2022) na kaya zenye vyoo bora zimeongezeka kutoka asilimia 27.6 (2015) hadi asilimia 62.1 (2022).

Aidha, Hali ya Upatikanaji miundombinu ya udhibiti wa taka na maji safi katika vituo vya kutolea huduma za Afya ni; vichomea taka vinavyokubalika katika Mkoa ni asilimia 4, mashimo ya kutupia kondo la nyuma ni asilimia 63 na upatikanaji wa vifaa vya kudumu vya kunawia mikono katika vituo ni asilimia 32 na vituo vilivyounganishwa katika mtandao wa maji ya bomba ni asilimia 33. Halmashauri za Wilaya zinaendelea kutekeleza mradi wa uboreshaji miundombinu ya maji na usafi wa mazingira katika vituo 37 kwa mwaka 2021/2022. Rejea Kiambatisho Na 10( iii)

Hali ya Uwepo wa Vyoo katika Shule si ya kuridhisha, Mahitaji ya matundu ya vyoo kwa wanafunzi katika Shule 659 ni 19,198 na hali halisi ya idadi ya matundu ya vyoo vilivyopo ni 8,275 (43%). Aidha kwa upande wa vyoo vya walimu, mahitaji ni 1212 na uhalisia ni vyoo 658 (54%) kama inavyoonekana kwenye Kiambatisho Na 10 (ii). Mkoa unaendelea kusimamia mradi wa uboreshaji wa miundo mbinu ya maji na Vyoo kwenye Shule za Msingi, ambapo kwa mwaka 2021/2022, jumla ya shule 4 kutoka Halmashauri za Manyoni zimepata fedha kwa ajili ya ujenzi wa vyoo na miundombinu ya maji na kwa mwaka wa fedha 2022/2023 jumla ya shule 73 zinatarajiwa kupata fedha kwa ajili ya ujenzi wa choo na miundo mbinu ya maji. Aidha kwa upande wa maji safi na salama, shule 315 kati ya 658 zina vyanzo vya maji safi na salama  na shule 169 (26%) zinatoa chakula cha mchana mashuleni. Rejea Kiambatisho Na 10  ( iv)

11.0 HALI YA UTEKELEZAJI WA MFUKO WA AFYA YA JAMII, BIMA YA AFYA NA MAKUSANYO YA PAPO KWA PAPO

Mkoa wa Singida ni miongoni mwa Mikoa ambayo Wananchi wake wanaendelea kuitikia vizuri kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa (iCHF) kwa kiwango cha uchangijaji wa wanachama kwa kiasi cha (shilling 30,000 kwa kila kaya) na kupata huduma za Afya kwenye vituo vya serikali na binafsi kwa wanachama waliojiunga bila sharti la kituo waliposajiliwa.

Kwa kipindi cha Januari hadi Mei 2022 jumla ya kaya 2,341 kati kaya 6476 sawa na asilimia 6% wamejiunga na mfuko wa afya ya jamii ulioboreshwa katika halmashauri zote saba (07). Hali ya utoaji huduma za ichf/NHIF katika katika Mkoa unaendelea vizuri kwani wananchi waliojiunga na mifuko hii ya Bima wanapofika katika vituo vya kutolea huduma za afya wanapata huduma za afya kwa kulingana na huduma zinazopatikana katika kituo husika, kuanzishwa kwa mfumo wa ukusanyaji wa malipo ya wanachama wa iCHF kwa njia ya kielekloniki (GePG). Mkoa wafanikiwa kutoa mafunzo kwa maafisa uandikishaji wapatao 296 kati ya maafisa uandikishaji 528 wanaohitajika katika mkoa sawa na asilimia 56% na kuwepo na upungufu wa maafisa uandikishaji wapatao 232 sawa na asilimia 44%

Hali ya ukusanyaji wa mapato kutokana na uchangiaji wa huduma za Afya sio wa kuridhisha katika Mkoa wa Singida kama inavyoonekana katika Kiambatisho Na: 11.

  • Katika bajeti ya mwaka 2021/2022  Halmashauri zilipanga kukusanya kiasi cha Tsh 773,510,000 kutoka mapato ya User fees ( Papo kwa Papo) ambapo hadi kufikia tarehe 4 Juni 2022 jumla ya Tsh 625,056,296 sawa na 81% zimekusanywa na Halmashauri kupitia vituo vya kutolea huduma za Afya sawa
  • Katika bajeti ya mwaka 2021/2022  Halmashauri zilipanga kukusanya kiasi cha Tsh 638,944,996 kutoka mapato ya iCHF ambapo hadi kufikia tarehe 4 Juni 2022 jumla ya Tsh 154,846,517 sawa na 24% zimekusanywa na Halmashauri kupitia vituo vya kutolea huduma za Afya sawa
  • Katika bajeti ya mwaka 2021/2022  Halmashauri zilipanga kukusanya kiasi cha Tsh 807,255,837 kutoka mapato ya NHIF ambapo hadi kufikia tarehe 4 Juni 2022 jumla ya Tsh 479,116,585 sawa na 59% zimekusanywa na Halmashauri kupitia vituo vya kutolea huduma za Afya sawa

12.0 HUDUMA ZA USTAWI WA JAMII

Huduma za Ustawi wa Jamii hutolewa kwa wananchi hususani kwa makundi maalumu zenye uwiano, haki na usawa ili kufikia maendeleo ya Makundi yote kwenye jamii ambapo hutolewa kwa kuzingatia Sera, Sheria,  kanuni ,miongozo na taratibu. Hali halisi ya utoaji huduma kwa makundi hayo ni kama ifuatavyo

 

  • Hali halisi ya  wazee

 Wazee wenye umri kuanzia miaka 60 na kuendelea Kitaifa wanakadiriwa kuwa Jumla 2,507,568 ambapo Ke 1,307,358 na Me 1,200,210 Mkoa kwa mwaka 2020/21 umetambua Wazee 65,454 ( Ke. 30,851 na Me 34,603) kati ya hao Wazee 9,432 (Me. 5,307 na Ke 4,125) wamepatiwa vitambulisho vya matibabu sawa na 14% kama ilivyoainishwa katika Kiambatisho Na 12 (i).Aidha Mabaraza ya Wazee ya ushauri yameundwa katika ngazi zote mabaraza hayo huwasaidia Wazee kujadili masuala mbalimbali yanayowahusu katika maisha yao.

Pia Mkoa una Makazi ya kulelea Wazee wasiojiweza ya Sukamahela yaliyopo Halmashauri ya Manyoni, Makazi yana jumla ya Wazee 16 Me 12 na Ke 04 ambao hupatiwa mahitaji ya Chakula, Malazi, Afya na msaada wa kisaikolojia  Aidha  Makao ya Wazee yaliyopo Chaberereko katika Halmashauri ya Mkalama yana Wazee 18 ( Me 11 na Ke 07) ambayo yalianzishwa  na Kanisa la KKKT, kwa sasa Wazee hao wanahudumiwa Chakula na Matibabu na Mkurugenzi wa Halmashauri kwa kushirikiana na Masista wa Kanisa Katoliki wa Mwanga.  Idadi ya Wazee na Makazi ya Wazee imeambatishwa kwenye Kiambatisho Na 12 (ii)

12.2 Hali halisi ya  watu wenye ulemavu

Mkoa kwa Mwaka 2020/21 umetambua Watu wenye Ulemavu wapatao 12,804  kati ya hao walemavu wa viungo ni 5,814(45.% )  walemavu wa akili 2,599 (20.2%) viziwi 1799( 14%) na Watu wenye ualbino 442 (3.4%)  huduma zitolewazo kwa Wenye Ulemavu ni Vifaa vya kujimudu, Afya, Elimu na uwezeshwaji kiuchumi kupitia 2% ya mapatao ya ndani ya Halmashauri pamoja na Elimu ya Ufundi Stadi    Kamati za Kuhudumia Watu wenye Ulemavu zimeundwa Ngazi ya Mkoa 1(100%) Ngazi ya  Wilaya 7 ( 100%), Ngazi ya Vijiji/Mitaa 494(  ) Kamati hizi husaidia kujadili changamoto za Watu wenye ulemavu katika ngazi husika na kuzitafutia ufumbuzi.

Mkoa una Chuo cha mafunzo ya Ufundi Stadi kinachowezesha Watu wenye ulemavu kupata elimu ya ufundi stadi na Jumla ya walemavu 89 (Me 37, Ke 52 )  wasio na ulemavu  7 ( Me 6 Ke 1) .Rejea Kiambatisho Na 12 (iii, iv&vi) 

 

12.3 Hali halisi ya watoto walio katika mazingira hatarishi

 Kwa mwaka 2020/21 jumla ya Watoto 15,859 (Me 7,454 na Ke 8,405) walio katika mazingira hatarishi wametambuliwa kati ya hao Watoto 8,231 sawa 52% walipatiwa huduma za Afya, kuunganishwa na Familia zao, Ushauri nasaha, Msaada wa kisheria, Elimu. Aidha sababu kubwa ya kuongezeka kwa watoto walio katika mazingira hatarishi kimkoa ni pamoja na Umasikini, Malezi yasio chana kutoka kwa Wazazi au Walezi pamoja na  maambukizi ya VVU na UKIMWI.

Aidha Jumla ya Watoto 186 ( Me 82 na Ke 104) wanalelewa katika Makao ambapo  Watoto hao   hupatiwa mahitaji yote ya msingi .Rejea Kiambatisho Na 12 (v& vi)

 

13.0 SEKTA BINAFSI

Ili kuwezesha utoaji wa huduma bora za afya, Ustawi wa jamii na Lishe na zinazofikika kirahisi kwa watu wote, Serikali inaendelea kutoa huduma kwa ubia na Sekta Binafsi. Katika kufanikisha Mashirikiano hayo, Serikali imeingia Mikataba ya utoaji wa huduma na Mashirika ya Dini. Kupitia ubia kati ya Serikali na Sekta Binafsi huduma zifuatazo zinatolewa bila malipo; Afya ya Uzazi na Mtoto, VVU/UKIMWI, Kifua Kikuu na Ukoma, Malaria. Kati ya vituo 44 vya Sekta Binafsi vituo tisa (9) tu ndiyo vyenye mikataba na Halmashauri.

Kwa ngazi ya Mkoa,Wizara ya Afya imeingia Mkataba na Hospitali ya Mt. Gaspar kwa ajili ya kutoa huduma za Kibingwa na rufaa ngazi ya Mkoa. Kwa ngazi ya Wilaya Serikali imeingia Mikataba na Hospitali ya Mt. Carolus Mtinko kwa ajili ya kutoa huduma za Afya ngazi ya Wilaya kwa Halmashauri ya Singida, na Hospitali ya Makiungu kwa ajili ya kutoa huduma kama Hospitali teule ya Wilaya kwa Halmashauri ya Ikungi.

Serikali inalipa mishahara kwa baadhi ya watumishi kwenye hospitali za Mt Gaspar, Mt Carolus Mtinko, Makiungu, Iambi na Kilimatinde.

Aidha huduma za Afya zinazotolewa na Hospitali za Malikia wa Ulimwengu, IAMBI na Kilimatinde ni za kusuasua, kunakosababishwa kwa kiasi kikubwa na kushindwa kulipa Mishahara ya watumishi, hii inapelekea watumishi wenye sifa na ujuzi kuhama katika hospitali hizo.

Huduma zinazotolewa na Hospitali ya Mt. Gaspar ni pamoja na: Huduma za Kibingwa

Magonjwa ya kina mama, Upasuaji na magonjwa ya watoto. Hospitali ya Makiungu inaendelea kufanya maboresho ya miundo mbinu itakayowezesha utoaji wa huduma za rufaa ngazi ya Mkoa, miundombinu inayojengwa ni: Jengo la Magonjwa ya Dharura, Jengo la mazoezi ya viungo, Jengo la magonjwa ya mlipuko, Karakana ya matengenezo ya Vifaa tiba, Jengo la wagonjwa mahututi (ICU) na huduma za uchunguzi za mionzi (CT-Scan).

Pia Sekta binafsi imekuwa ikitoa huduma katika jamii kwa kuendesha Kliniki za magonjwa mbalimbali, Famasi, Maduka ya Dawa Muhimu na Maabara.

 

  • CHANGAMOTO ZINAZOATHIRI UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA 
  • Kutokuwepo kwa Nyumba za Makazi ya Watumishi kwa baadhi ya Vituo vya Afya na Zahanati zinazojengwa hasa katika maeneo ya vijijini ambako hata kupata Nyumba za kupangisha hazipatikani.
  • Idadi kubwa ya Zahanati kutokuwa na Watumishi wa Kada za Tabibu/Tabibu Msaidizi, Wateknolojia Wasaidizi wa Maabara na Dawa katika ngazi ya Zahanati
  • Kuchelewa kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa Hospitali Mpya ya Rufaa ya Mkoa katika eneo la Mandewa ulionza mwaka 2009 na hivyo kusababisha huduma za Hospitali ya Rufaa kutokutolewa katika eneo moja.
  • Hospitali Kutokuwa na Mfumo wa kisasa wa kuzalisha Oksijeni “Oxygen Plant” hali inayosabisha kutokuwepo na uhakika wa 100% wa upatikanaji wa Gas ya Oxygen kwa wagonjwa wanaohitaji hasa kipindi cha mlipuko mkali wa homa ya UVIKO-19
  • Kutokuwepo kwa miundombinu ya kutengeneza maji tiba “Infusion unity” katika Hospitali.
  • Majengo ya Hospitali kutokuwa na “Ramp” na korido za kuunganisha majengo na hivyo kusababisha usumbufu kwa wagonjwa na watoa huduma
  • Uchakavu wa mindombinu ya Majengo, mifumo ya maji safi na maji taka katika Hospitali ya Kiomboi Iramba na Hospitali ya Halmashauri ya Manyoni baada ya kukaa kwa kipindi kirefu bila kufanyiwa matengenezo/ukarabati mkubwa.
  • Kutotumika kikamilifu kwa majengo ya Hospitali ya awamu ya kwanza yaliyokamilika katika Hospitali za Mkalama na Singida kutokana na kutokuwepo kwa Vifaa Tiba na watumishi wa Afya wa kuwezesha huduma kamilifu kuanza kutolewa.
  • Ukosefu wa kitengo cha wagonjwa mahututi wa watoto wachanga katika Hospitali, Upungufu wa vituo vinavyotoa huduma za dharura (BEmONC na CEmONC),
  • Baadhi ya Vituo vya Afya vilivyofanyiwa upanuzi na ukarabati kuchelewa kuanza kutoa huduma za upasuaji wa dharura kwa akinamama wajawazito kama ilivyokusudiwa kutokana na kutokuwepo kwa Vifaa Tiba na Watumishi, vituo hivyo ni: Kituo cha Afya Nkonko, Chibumagwa, Sepuka, Msange, Mitundu na Mgori.
  • Kutokuwepo kwa Miundombinu ya majengo ya Mionzi, kuhifadhia maiti, jengo la  kufulia na viteketezea taka katika vituo vingi vya Afya
  • Uchakavu wa Miundombinu hususani majengo ya zahanati yaliyojengwa muda mrefu..
  • Zahanati nyingi kuwa na Jengo dogo na finyu la wagonjwa wa nje na hivyo kusabibisha huduma zote za Zahanati kutolewa katika eneo moja. Hii inasabibisha kukosekana kwa Usiri kwa wagonjwa hasa kwa Akinamama wanaojifungua, kuwepo kwa msongamano wa vifaa mbalimbali kwenye jengo la Zahanati.
  • Zahanati nyingi kutokwa na Miundombinu inayowezesha utoaji wa huduma za Maabara
  • Zahanati nyingi kutokuwa na Miundombinu ya Mfumo wa maji safi na maji taka
  • Baadhi ya vituo vya kutolea huduma za Afya kutokuwa na Mfumo wa kielektroniki unaotumika kusimamia bidhaa za Afya.
  • Vituo vya kutolea huduma kutokuwa na orodha ya dawa “Hospital formulary” zinazotakiwa kuwepo kwenye kituo.
  • Kutokupatikana kwa chanjo za kutosha za MR, BOPV na PCV13 katika ngazi ya Taifa, Mkoa na Halmashauri
  • Ukosefu wa Mabomba ya 0.05ml ya kutolea chanjo ya BCG katika ngazi ya Taifa kwa kipindi kirefu
  • Magari mengi ya Chanjo ni chakavu hasa ya Mkoa, Ikungi, Manyoni na Manispaa ya Singida hali inayochangia kuwa mzigo wa kufanya matengenezo mara kwa mara
  • Usambazaji hafifu wa Kondomu kwenye jamii unaosababishwa na kutopatikana kwa mahitaji halisi ya kondomu ngazi ya jamii, uhalibifu wa miundombinu ya kuwekea kondomu.
  • Wagonjwa ambao washaanza huduma, kuacha dawa hivyo kusababisha usugu wa dawa na kupelekea kwenda kwenye hatua nyingine ya UKIMWI “Advanced HIV”.
  • Unyanyapaa kwa WAVIU kwenye jamii, hivyo kusababisha wanachi wengi kutopima afya zao kwa kuogopa kujulikana na wale wanojua afya zao kutojiunga na huduma ya  dawa ya kufubaza virusi vya UKIMWI.
  • Ugawaji hafifu wa vyandarua vyenye viuatilifu vya muda mrefu (LLIN) kwa akina mama wajawazito na Watoto wenye umri wa kupata chanjo ya Surua -Rubella
  • Ukosefu wa watumishi wenye uelewa wa utoaji wa matibabu ya utapiamlo kwa wagonjwa wan je na ndani.
  • Ukosefu wa Vifaa vya kufanyia tathmini ya hali ya lishe katika vituo vya kutolea huduma.
  • Kubadilika kwa mwongozo wa utoaji wa matibabu mara kwa mara inayopelekea kupunguza baadhi ya huduma za NHIF zinazotolewa kwenye vituo
  • Mapato hafifu ya vituo katika vyanzo vya NHIF na iCHF
  • Mwitikio mdogo wa Jamii kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (iCHF)
  • Watumishi kutokufuata miongozo ya utoaji wa matibabu kupelekea makato makubwa ya madai ya fedha
  • Kuwepo kwa changamoto za mfumo wa kielekitroniki wa uendeshaji na usimamizi wa Mfuko wa Afya ya Jamii hali inayopelekea kuzorota kwa shughuli za uandikishaji wa Wanachama wa iCHF na Malipo kwa Vituo vinavyotoa huduma
  • Kuendelea kuwepo kwa asilimia 0.8(2656) ya kaya ambazo hazina 9 vyoo ndani ya Mkoa kufikia Machi, 2022
  • Upungufu  wa matundu ya vyoo kwa watoto wa shule za Msingi ndani ya Mkoa kwa asilimia 56.9 kufikia Machi 2022
  • Upungufu wa vichomea taka zitokanazo na huduma za Afya katika vituo vya kutolea huduma za Afya vinavyokubalika.
  • Mwitikio hafifu wa Jamii kuhusiana na chanjo za UVIKO-19 zinazoendelea kutolewa.
  • Upungufu wa Maafisa Ustawi wa Jamii ngazi ya Halmashauri na Kata
  • Kutotekelezwa/kuimarishwa  kwa Mfumo jumuishi wa Kitaifa wa usimamizi wa mashauri ya watoto ngazi ya Jamii katika Halmashauri zote za Mkoa wa Singida
  • Kutokuwepo kwa nyumba salama kwenye Mkoa
  • Kutokuwepo kwa Kituo cha huduma ya Mkono kwa Mkono (One stop center ) kwa ajili ya waathirika wa vitendo vya Ukatili wa Kijinsia na Ukatili dhidi ya watoto
  • Matukio mengi ya ukatili wa kijinsia hayatolewi taarifa hivyo kusababisha madhara makubwa kwa wahanga kama vile ulemavu wa kuduma n.k
  • Baadhi ya vituo vya kutolea huduma vya Sekta binafsi Kutopokea na kutoa huduma kwa wanachama wa Mfuko wa Afya ya Jamii.
  • Baadhi ya wamiliki wa Vituo vya kutolea huduma vya Sekta Binafsi kutokuwa tayari kuingia mikataba na Halmashauri
  • Kuwepo kwa Zahanati, Maabara na Maduka ya dawa bubu yabnayotoa huduma za afya
  • Upungufu wa mkubwa magari ya kubebea wagonjwa (Ambulance)

15.0 USHAURI NA MAPENDEKEZO

  • Kuainisha mahitaji halisi ya watumishi wa Kada za Afya na kuomba kibali cha kupatiwa watumishi wapya katika bajeti za mishahara za Halmashauri kila mwaka
  • Kuzisimamia Halmashauri kuajiri watumishi wa muda kupitia mpango na mwongozo wa kujitolea Watumishi ili kupunguza uhaba wa Watumishi uliopo
  • kuzisimamia Halmashauri kuainisha, kuandaa na kutekeleza mpango wa ujenzi wa nyumba za watumishi hasa katika maeneo ya vijijini
  • Kusimamia Halmashauri kufanya uhamisho wa ndani wa watumishi (Redistribution) hasa kwenye vituo ambavyo vimeboreshewa miundombinu na kupandishwa hadhi kuwa CEmONC na vituo vyenye idadi kubwa ya wateja  hasa eneo la afya ya uzazi na mtoto.
  • Kusimamia kwa ukaribu ujenzi wa majengo mbalimbali yanaendelea kujengwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ili yakamilike na kuanza kutumika kwa wakati.
  • Kufanya tathmini na uandaji wa Michoro /BOQ kwa ajili ya ukamilishaji wa majengo yote muhimu yanayohitajika kujengwa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa ikiwa pamoja na ujenzi wa Ramp, korido za kuunganisha majengo yote ili kupunguza usumbufu kwa wagonjwa.
  • Kuomba fedha maalum Wizara ya Fedha na Wizara ya Afya kwa ajili ya ukamilishaji wa ujenzi wa majengo,uzio,Korido/ramp na miundombinu yote inayohitajika katika Hospitali Mpya ya Rufaa ya Mkoa ili kuwezesha huduma zote za Afya ngazi ya Mkoa kutolewa katika eneo moja la Hospitali na majengo ya zamani ya Hospitali kukabidhiwa kwa Manispaa ili yatumike kama Hospitali ya Manispaa
  • Kuwasiliana na Wizara ya Afya na Wizara ya fedha kwa ajili ya kupata fedha kwa ajili ya ujenzi na kusimika mfumo wa Oxygen Plant katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa.
  • Kukumbushia mahitaji ya vifaa vinavyohitajika kutoka kwenye Mamlaka zinazohusika (OR-TAMISEMI na MSD) ili kuviwezesha vituo viliyokamilika kuanza kutoa huduma za dharura za upasuaji.
  • Kuzishauri ma kusimamia Halmashauri kutenga bajeti kwa ajili ya ujenzi wa Miundombinu ya huduma ya mionzi, jengo la kuhifadhi maiti na viteketeza taka vyenye sifa.
  • Kuomba fedha maalum Wizara ya Fedha na OR-TAMISEMI kwa ajili kufanya ukarabati mkubwa wa majengo na miundombinu chakavu katika Hospitali za halmashauri ya Manyoni na Iramba (Kiomboi)
  • Kuomba fedha maalum Wizara ya fedha na OR- TAMISEMI kwa ajili ya ununuzi wa vifaa Tiba na kuomba kupangiwa watumishi kwa ajili ya kuwezesha huduma kamilifu kuanza kutolewa katika majengo mapya ya Hospitali yaliyokamilika katika Halmashauri za Mkalama, Singida DC na Ikungi.
  • Kusimamia Halmashauri kutenga bajati ya ukarabati wa zahanati zenye miundombinu chakavu ya majengo , ikiwa ni pamoja na kuziombea fedha Serikali Kuu
  • Kushauri na kusimamia Halmashauri kutenga fedha kila mwaka katika Mipango na bajeti ya Zahanati kwa ajili ya ukarabati mdogomdogo ikiwa ni pamoja na kujenga kwa awamu jengo la kutolea huduma za Afya ya Mama na mtoto.
  • Kuendelea kusimika mifumo ya kielektroniki kwa ajili ya usimamizi wa Dawa, vifaa tiba na vitendanishi. Vituo vipya ujenzi uende sambamba na usimikaji wa miundombinu ya TEHAMA.
  • Vituo vya kutolea huduma za Afya viwezeshwe kuandaa orodha ya dawa “Hospital formulary” zinazotakiwa kuwepo kwa kila kituo.
  • Kuimarisha usambazaji wa Kondomu kwenye jamii kwa kushirikiana na Serikali za vijiji ili waweze kuainisha  mahitaji halisi ya kondomu ngazi ya jamii.
  • Kutoa elimu na unasihi kwa WAVIU ambao washaanza huduma, ili wasiache matibabu.
  • Kuendelea kutoa elimu kwenye Jamii ili kuondoa unyanyapaa kwa WAVIU kwenye jamii, hii itasaidia wanachi wengi kupima afya zao ili waweze kujua hali zao za Kiafya na hivyo kujiunga na Tiba na Maangalizi.
  • Halmashauri kuhamasisha ujenzi wa vyoo bora kwenye kaya zisizokuwa na vyoo.
  • Halmashauri kutenga bajeti kwa ajili ya kujenga miundo mbinu ya vyoo kwenye shule zenye changamoto.
  • Halmashauri kutenga bajeti ya kujenga vichomea taka zitokanazo na huduma za Afya katika vituo vya kutolea huduma za  Afya vinavyokubalika.
  • Mkoa utaendelea kuhakikisha unafuatilia upatikanaji wa chanjo na mabomba ya sindano ya BCG 0.05ml kutoka ngazi ya Taifa.
  • Kuendelea kutafuta wadau mbalimbali wa kusaidia kuongeza kasi ya uchanjaji kwa chanjo za watoto (Routine) na chanjo za UVIKO-19
  • Mkoa utaendelea kufuatilia maombi yaliyowasilishwa ya Kuhakikisha Halmashauri za Singida Manispaa, Ikungi, Manyoni na MKoa wanapatiwa magari mapya ya kusambaza chanjo kutoka TAMISEMI na Wizara ya Afya kupitia mpango wa taifawa Chanjo (IVD)
  • Kuimarisha ugawaji wa vyandarua vyenye viuatilifu vya muda mrefu (LLIN) kwa akina mama wajawazito na Watoto wenye umri wa kupata chanjo ya Surua -Rubella
  • Kusimamia Halmashauri kuratibu utoaji wa mafunzo ya utoaji wa matibabu ya utapiamlo kwa waumishi wasio  na mafunzo hayo.
  • Kusimamia Halmashauri kuhamisha vifaa vya kufanyia tathmini ya hali ya lishe (Mizani, tepe za MUAC na Vibao vya kupimia urefu kwa watoto) kutoka kwenye vituo vilivyo na ziada kwenda kwenye vituo visivyo navyo
  • Halmashauri kwa kushirikiana na Mfuko wa Bima ya Afya kuendelea kutoa mafunzo kazini kwa watumishi juu ya ujazaji wa mifumo ya madai itakayopunguza makato kwa vituo..
  • Kuimarisha huduma za Afya zinazotolewa kwenye ngazi zote ikiwemo huduma za Dawa na Maabara ili kuwezesha wateja  wa NHIF na iCHF kupata huduma stahiki.
  • Kuishauri OR-TAMISEMI kuchukua hatua za haraka za kuimarisha na kuboresha mfumo wa Kielekitroniki wa uendeshaji na usimamizi wa iCHF ili kuwezesha shughuli za uandikishaji wa Wananchama na malipo kufanyika kwa haraka na bila vikwazo
  • Kutoa elimu kwa makundi yanayopata matibabu kwa njia ya msamaha wa matibabu pia kuweza kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii  ili kupunguza idadi ya wanufaika wa msamaha wa  matibabu
  • Kuendelea kutoa elimu ya bima sambamba na kufanya uhamasishaji kupitia viongozi ngazi ya vijiji, Kata, Tarafa na Viongozi maarufu na Viongozi wa dini ndani ya halmashauri ili kutoa hamasa kwa Wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii.
  • Kusimamia ujenzi wa vituo viwili  vya huduma za Mkono kwa mkono kwenye Hospitali ya Wilaya ya Ikungi na Hospitali ya Mkoa wa Singida kwa kushirikiana na Shirika la KIHOWEDE kwa ufadhili wa Shirika la UN – WOMEN, KOICA na UNFPA.
  • Kuendelea kutoa mafunzo kwa watoa huduma juu ya utoaji bora wa huduma kwa waathirika wa vitendo vya ukatili na kuendelea kutoa taarifa ya matukio yote.
  • Maafisa Ustawi wa Jamii ngazi za Halmashauri kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo  kukutoa elimu kwenye jamii  juu ya  masula ya ulinzi wa watoto, masuala ya ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto, malezi na makuzi ya awali ya watoto.
  • Halmashauri ziwaelimisha wamiliki wa Vituo vya kutolea huduma za Afya vya Sekta binafsi kuhusu umuhimu wa kuingia mikataba ya huduma na Halmashauri.
  • Halmashauri kuwaelimisha wamiliki kutoa huduma za afya kwa wanachama wa Mfuko wa Afya ya Jamii, hii itasaidi pia kuongeza wanachama wanaojiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii.
  • Kuimarisha usimamizi na ukaguzi kwa kushirikiana na vyombo vya Dola ikiwa pamoja na kuchukua hatua stahiki kwa wale wote watakaopatikana kuendesha na kutoa huduma za  afya bila kuwa na usajili
  • Kuwasilisha Wizara ya Afya na OR – TAMISEMI maombi maalum ya kuwekwa katika Mpango wa kupatiwa Magari ya kubeba Wagonjwa (Ambulance) hasa katika Vituo vya Afya ambavyo vimejengwa/vinajengwa na kuboreshewa Miundombinu ili viweze kutoa huduma za upusuaji kamili wa dharura kwa Wajawazito.

16.0 HITIMISHO

  • Kupitia tathimin iliyofanyika imetoa picha ya hali ya utoaji wa huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lisje katika ngazi ya Mkoa, Halmashauri na vituo vya kutolea huduma za Afya. Timu ya Usimamizi wa Masuala ya Afya Mkoa itajikita katika kutatua changamoto zilizobainika baada ya taarifa hii ya tathmini ikiwa ni pamoja na kuandaa mpango mkakati kabambe wa kuimarisha na kuboresha utoaji wa huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe katika ngazi zote.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • DKT.MGANGA ASISITIZA MADAKTARI BINGWA KUTOA HUDUMA BORA

    May 05, 2025
  • WATUMISHI NA WAAJIRI HODARI MKOANI SINGIDA WAPOKEA TUZO

    May 02, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.