• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

AZIMIO LA DAR ES SALAAM KUCHOCHEA UWEKEZAJI NCHINI

Posted on: January 29th, 2025

Rais Samia Suluhu Hassan amesema Tanzania ina uwezo wa kuuza umeme nje ya nchi kwa sababu mahitaji ya umeme nchini hadi kufikia mwezi Novemba mwaka 2024 yalikuwa  megawati 1,888 wakati uzalishaji ulikuwa megawati 3,431.

Rais Samia ameyasema hayo Januari 28, 2025 alipokuwa akihutubia mkutano wa wakuu wa nchi za Afrika kuhusu nishati, katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) mkoani Dar es Salaam. 

Aidha, ameweka bayana kuwa moja ya mipango ya Tanzania hivi sasa ni kuunganisha mtandao wa umeme uliopo nchini na nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika ili biashara ya umeme iwezeshwe kutoka Afrika Kusini hadi Misri ambapo tayari imekwishaunganishwa miundombinu ya umeme kwa nchi za Burundi, Kenya na Rwanda huku kwa nchi za Zambia na Uganda utaratibu wa kuziunganisha ukiendelea.

Mkutano huo uliofanyika Dar es Salaam, Tanzania umewakutanisha Marais na Wakuu wa nchi barani Afrika ili kuja na azimio la pamoja la kuwafikishia nishati ya umeme waafrika zaidi ya milioni 300 ifikapo mwaka 2030.

Kadhalika,Viongozi mbalimbali wa Kimataifa wamesema wanaunga mkono jitihada za kusambaza nishati ya umeme barani Afrika kupitia ajenda ya Mission 300 itakayopeleka umeme kwa watu milioni 300 ifikapo mwaka 2030.

Wakizungumza wakati wa mkutano wa nishati Afrika,viongozi hao wameeleza mipango ya taasisi zao katika kuchangia kufanikishwa kwa ajenda hiyo huku  wakichangia mjadala maalumu uliokuwa ukiangazia mchango wa taasisi na Jumuiya za kimataifa katika kuleta mapinduzi ya nishati barani Afrika.

Baadhi ya viongozi hao ni Bjorg Sandkjer ambaye ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway anayeshughulikia Maendeleo ya Kimataifa, Rachel Kayte ambaye ni Mwakilishi wa masuala ya tabianchi kutoka nchini Uingereza na Woohchong Um ambaye ni Mtandaji Mkuu wa Taasisi inayoshughulikia  masuala ya nishati ya Global Energy Alliance for people and Planet.

       Pia,Wakuu wa Nchi za Afrika ikiwemo serikali ya Tanzania wamepitisha Azimio la Dar es Salaam lenye malengo mbalimbali ikiwemo kutatua changamoto ya Nishati na kutekeleza mpango wa matumizi ya nishati safi pamoja na ajenda ya ‘Mission 300’ inayolenga kupeleka umeme kwa Waafrika milioni 300 ifikapo mwaka 2030.

Azimio hilo ni mkataba wa pamoja wa Wakuu hao wa nchi na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa kuleta mageuzi makubwa katika sekta ya nishati kwa kuhakikisha nishati inakua toshelevu katika mataifa ya Afrika jambo ambalo litachochea uwekezaji katika sekta mbalimbali na kuleta maendeleo.

Aidha, malengo mengine ya azimio hilo ni kuimarisha na kuboresha miondombinu ya nishati pamoja na kufikisha umeme kwa waafrika kwa gharama ndogo, kuwekeza katika vyanzo mbalimbali vya umeme ikiwemo jua, maji, jotoridi, kuhakikisha mikakati ya kikanda na kimataifa ya nishati inatekelezeka kwa wakati, kuweka mazingira wezeshi ikiwemo kufanya marekebisho ya sera na miongozo kwa wawekezaji wa sekta binafsi ili wawekeze katika sekta ya nishati. 



(Picha kwa hisani ya TBC)


Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.