• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

KATIBU MKUU WA CCM BALOZI DKT. NCHIMBI AWAPA TANO VIONGOZI WA MKOA WA SINGIDA KWA UTEKELEZAJI BORA YA MIRADI YA MAENDELEO.

Posted on: May 29th, 2024

Serikali ya mkoa wa Singida imepongezwa kwa kusimamia na kutekeleza kikamilifu Ilani ya Chama ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi kwa kiwango cha juu ikiwemo miradi ya maji, afya, elimu na miundombinu mkoani humo.

Pongezi hiyo zimetolewa na Katibu Mkuu wa CCM Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi katika ziara yake ya kikazi ya Siku Mbili mkoani Singida wakati anazungumza na wananchi kwenye mikutano ya hadhara katika Wilaya ya Manyoni na Ikungi pamoja na kusikiliza na kutatua papo hapo kero ambazo zilitolewa na wananchi.

Balozi Nchimbi amesema ushirikiano imara kati ya Viongozi wa Serikali na wa CCM mkoani Singida umepelekea miradi mingi ya maendeleo kutekelezwa kwa wakati na kwa kiwango cha juu.

Amesema taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM aliyopatiwa na Mkuu wa mkoa wa Singida Mheshimiwa Halima Dendego, imeonyesha wazi kasi kubwa ya Maendeleo ambayo imepigwa mkoani Singida kwa kuboresha na kuimarisha huduma mbalimbali za Kijamii ikiwemo huduma za maji, afya, elimu,  miundombinu, umeme, pamoja na sekta kilimo kwa usalama wa chakula.

Naye, Mkuu wa mkoa wa Singida Mheshimiwa Halima Dendego, akitoa taarifa ya mkoa wa Singida kuhusu utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi amemhakikishia Katibu Mkuu huyo wa CCM wataendelea kusimamia kikamilifu fedha ambazo wanapatiwa na Serikali ya awamu ya Sita katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ili wananchi waweze kupata huduma bora na za uhakika za maendeleo karibu na maeneo yao.

Halima Dendego amesema mpaka sasa mkoa wa Singida tayari umepokea zaidi ya shilingi Trilioni Moja kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo hali ambayo imeufanya mkoa wa Singida kung’aa kimaendeleo katika sekta mbalimbali.

Mkuu huyo wa mkoa wa Singida amemwomba Katibu Mkuu huyo wa CCM kumfikishia Salamu za pongezi na shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendeleo kuupatia mkoa wa Singida fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya wananchi.

Amesema mkoa wa Singida kwa sasa unaendelea na mipango na mikakati ya kuwavutia wawekezaji katika sekta mbalimbali wa ndani na nje ya nje kuja kuwekeza mkoani humo ikiwa ni sehemu ya kuongeza pato la mkoa na la taifa kwa ujumla kupitia vivutio vya uwekezaji kwenye masuala mbalimbali ikiwemo kilimo na utalii.

MWISHO

====================

 

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • "SINGIDA IMEJIPANGA KUONGOZA UFAULU KITAIFA":RC DENDEGO

    June 04, 2025
  • MRADI WA TACTIC KULETA NEEMA MANISPAA YA SINGIDA.

    June 02, 2025
  • "WAHITIMU MSIBWETEKE,JIENDELEZENI KATIKA FANI ILI MJIAJIRI"-DKT.MGANGA

    May 30, 2025
  • DKT.MGANGA:"WATUMISHI MSIKUBALI KUTUMIKA VIBAYA,KUWENI NA UTAMBULISHO MZURI"

    May 27, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.