• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

MADAKTARI BINGWA NA BOBEZI 40 WA RAIS SAMIA WATUA SINGIDA KUTOA HUDUMA ZA MATIBABU YA KIBINGWA KWA SIKU 6.

Posted on: May 13th, 2024

Serikali ya Mkoa wa Singida imewaagiza Waganga Wakuu wa Halmashauri za Wilaya mkoani humo kuhakikisha wanapanga Wauguzi na Watalaamu wa afya kada nyingine wa kutosha ambao watashirikiana na Madaktari Bingwa na Bobezi 40 wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika utoaji wa huduma mbalimbali za kiafya mkoani humo.

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga, ametoa kauli hiyo wakati akiwakaribisha madaktari bingwa na bobezi wa Rais Samia ambao wamekuja mkoani Singida kusaidia matibabu ya kibingwa na bobezi kwa wananchi wa mkoa wa huo kwa muda wa Siku Sita (6) kuanzia leo tarehe 13 Mei hadi 18 Mei, 2024.

Katibu Tawala huyo amesema kazi ya utoaji wa matibabu ya kibingwa na bobezi itaenda haraka iwapo Madaktari hao wanapata wasaidizi wazuri katika kila kada kwenye maeneo ambayo watatoa huduma za afya hizo.

“Nichuku fulsa hii kuwaalika Wananchi wa Mkoa wa Singida kwa wenyeuhitaji wa huduma za kibingwa kujitokeza kwenye hospitali zote za Wilaya, Sitegemei Mwananchi yeyote kukosa huduma hizi za matibabu ya kibingwa na bobezi huduma ambazo huwa wanazifuata mbali na kwa gharama kubwa, hivyo lazima Wananchi wapewe taarifa ili wapate matibabu karibu na maeneo yao,” Amesisitiza Dkt. Fatuma Mganga.

Amewahakikishia ushirikiano Madaktari hao Bingwa na Bobezi katika kila jambo wanalofanya lengo ni kuhakikisha wananchi wa mkoa huo wanapata matibabu ya uhakikika kupitia madaktari hao wa Rais Samia.

Katibu Tawala pia amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuanzisha huduma hiyo ambayo imekuwa mkombozi kwa Watanzania wengi ambao baadhi yao wanashindwa kumudu gharama za kwenda kupata matibabu hayo kwenye Hospitali kubwa nchini na kwa sasa wanaipata karibu na maeneo yao.

Naye, Afisa Programu kutoka Wizara ya Afya, Idara ya Uzazi, Mama na Mtoto Joachim Masunga, amesema mpango huo wa kutoa matibabu ya kibingwa na bobezi utafanyika nchi nzima nia ni kuona Mtanzania anapata huduma hizo karibu na maeneo yao na kuondoa tatizo la kufuata huduma hizo mbali na kwa gharama kubwa.

Masunga amesema kwa sasa Serikali imewekeza kwa kiasi kikubwa katika ujenzi wa Hospitali na Vituo vya afya pamoja na kupeleka vifaa vya kutosha vya afya lengo likiwa ni kusaidia Watanzania kupata huduma bora na za uhakika katika maeneo yao ikiwemo mpango wa kupeleka Madaktari bingwa na bobezi kwa kila Wilaya ili kusaidia wananchi kupata huduma hizo kwa njia rahisi.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Victorina Ludovick, akizungumza wakati wa kuwakaribisha Madaktari bingwa wa Rais Samia, katika Mkoa wa Singida.

Timu ya Uongozi wa Huduma za Afya Mkoa wa Singida (RHMT) wakati wa mapokezi wa Madaktari bingwa ndani ya ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.


Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.