• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

MADIWANI LIMENI ILI MUWE MFANO WA KUIGWA; RC NCHIMBi.

Posted on: September 14th, 2017

  Madiwani Mkoani Singida wametakiwa kulima mazao ya biashara kama vile Pamba na Korosho ambapo mazao hayo ni ya kipaumbele Mkoani hapa, ili kuonyesha faida za kilimo hicho kwa wananchi.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amewaeleza hayo madiwani mapema leo katika mkutano wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (Alat)-Mkoa, tawi la Singida uliofanyika katika ofisi za halmashauri ya Wilaya ya Mkalama.

Dkt Nchimbi amesema madiwani wanapo hamasisha kilimo cha korosho na pamba kwa vitendo hasa kwa wao kuwa na mashamba yanayoonyesha zao hilo linastawi vizuri, wananchi wengi watahamasika na kujifunza kutoka kwao.

Ameongeza kuwa mkutano huo ulenge hasa katika kuangalia namna bora ya kumtumikia mwananchi na kuangalia njia mbalimbali za kumuokoa katika umaskini ili katika kuelekea Tanzania ya Uchumi wa kati na viwanda, asiwe mtazamaji bali mshiriki mkuu.

Dkt Nchimbi amesisitiza kuwa mkutano huo utumike pia kubainisha rasilimali zilizopo Mkoani Singida pamoja na fursa ambazo zinaweza kupatikana kutokana na uwepo wa rasilimali hizo.

“Singida tunazalisha ngozi na kuiuza ikiwa ghafi hivyo faida inakuwa ndogo, tumieni mkutano huu kuangalia uwezekano wa kuanzishwa kwa kiwanda kikubwa cha ngozi, ili tuanze sasa kuuza bidhaa za ngozi pamoja na kununua ngozi kutoka mikoa mingine nchini”, ameeleza Dkt Nchimbi.

Ameongeza kuwa ili kuboresha utendaji unaolenga kumsaidia mwananchi, maafisa utumishi wanapaswa kuwasimamia watumishi ili waweze kufanya kazi kwa bidii na uadilifu huku akiwataka wawapende watumishi wao.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (Alat)-Mkoa, tawi la Singida James Mkwega amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa nasaha zake na kumuahidi kuwa mkutano huo utaweka malengo ya kuendeleza mkoa.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amewaomba wananchi wa Singida kumuombea Mbunge wa Singida Mashariki Mhe. Tundu A. Lissu aliyejeruhiwa kwa risasi nyumbani kwake Dodoma.

Dkt Nchimbi amesema Lissu ni mwanasingida mwenzetu hivyo tunatakiwa kumuombea ili arejee katika afya yake na kuweza kuendelea na majukumu yake ya kuwatumikia wana Singida na Taifa kwa ujumla.

Aidha ameongeza kuwa hakuna anayefurahishwa kwa kitendo alichofanyiwa Lissu na kuwataka wanasingida na taifa kwa ujumla kuendelea kuliombea taifa liendelee kuwa kisiwa cha amani na utulivu.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.