• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

MAJARIBIO YA MBEGU CHOTARA YATOA MATUMAINI MAPYA KWA WAKULIMA NA WASINDIKAJI WA ALIZETI SINGIDA.

Posted on: November 19th, 2017

  Wakulima na wasindikaji wa zao la Alizeti Mkoani Singida wameonekana kufurahia na kupata matumaini mapya mara baada ya kushuhudia matokea ya majaribio ya usindikaji wa mbegu chotara ya Alizeti mkoani Singida.

Wakulima na wasindikaji hao wameshuhudia majaribio ya usindikaji wa mbegu chotara ya alizeti yakifanyika katika kiwanda cha kukamua mafuta ya Alizeti cha Nuru mjini Singida, kwa kukamua mbegu chotara na zile za zamani kisha kulinganisha kiwango cha mafuta na mashudu yaliyopatikana.

Mbegu chotara zilizofanyiwa majaribio zimepandwa na wakulima mkoani hapa ikiwa ni sehemu ya majaribio hayo, ambapo matokeo yameonyesha kuwa mbegu chotara zinatoa mazao mengi, mafuta na mashudu mengi, zinatumia muda kidogo shambani mpaka kuvunwa, zinatumia maji kidogo na hazishambuliwi na magonjwa ikilinganishwa na mbegu za zamani.

Mmoja kati ya wakulima aliyeshiriki majaribio ya kulima mbegu hizo Kutoka Ihanja Wilayani Singida John Thomasi alihudhuria pia majaribio ya usindikaji wa mbegu hizo na kusema kuwa sasa wakulima wa alizeti wamepata mwanga kwa kuona namna ambavyo kilimo cha alizeti kwa kutumia mbegu chotara ya alizeti kitawakomboa.

“Mimi ni mmoja kati ya waliolima hizo mbegu chotara kama sehemu ya majaribio na tuliona kwa kuanzia shambani hazisumbui, zinatumia maji kidogo, na mavuno ni mengi, kilichobaki ilikuwa ni kujua ubora wake katika kutoa mafuta na mashudu jambo ambalo tumeshuhudia leo kuwa mbegu hizi zinatoa mafuta mengi kuliko zile za zamani”, amesema Thomasi

Meneja Msimamizi Maarifa na Mawasiliano kutoka shirika la AMDT Al-amani Mutarubukwa amesema shirika hilo linalojikita katika Kilimo cha alizeti nchini hasa katika kuboresha mfumo wa masoko, uzalishaji na usindikaji lilifanya utafiti ulioonyesha kuwa changamoto kubwa ya wakulima wa alizeti ni kutokuwa na mbegu bora.

Mutaburukwa amesema kwakuwa mbegu zilizokuepo zimekuwa hazitoi mazao ya kutosha Shirika hilo lilifadhili majaribio ya mbegu chotara Mkoani Singida kupitia mradi wa Faida Market link kwa kuwezesha wakulima kupanda mbegu hizo.

Ameongeza kuwa matokeo ya majaribio hayo yamekuwa mazuri ambapo kwa upande wa mavuno mbegu chotara zimethibitika kutoa mazao mengi ambapo kwa ekari moja mkulima mmoja ameweza kuvuna gunia 16 ambapo kwa mbegu za zamani angeweza kuvuna gunia 3 mpaka tano.

Mutaburukwa amesema “Mara baada ya kuvunwa kwa alizeti hiyo AMDT pia imefanya majaribio ya kusindika mbegu hizo ambapo kilogram ishirini za mbegu chotara zimetoa mafuta lita sita ambapo mbegu za zamani zimetoa lita tano kwa kilo hizo hizo, huku mashudu yakipatikana kilogram 14 kwa mbegu chotara tofauti na kilogram 13 za mbegu za zamani.

Ameongeza kuwa Sifa ya mbegu hizo chotara ni kutoa mazao mengi, kutumia maji kwa ufanisi, zinastawi katika udongo wa aina zote, na pia hazikai shambani mda mrefu kabla ya kuvunwa ambapo hutumia siku 84 mpaka kuvuna tofauti na siku 97 kwa mbegu za zamani.

Naye Mwakilishi wa Meneja wa Faida Mali Mary Daniel amesema majaribio ya mbegu chotara yalianza mwenzi wa nne na yalihusisha halmashauri nne ambazo ni Mkalama, iramba, ikungi na Singida, ambapo mbegu ziliyotumika katika kufanya majaribio ya usindikaji zililimwa Kijiji cha ihanja wilaya ya ikungi.

Mary amesema wakulima waliofika kushuhudia majaribio ni 25 na wasindikaji 12 kutoka katika wilaya ya singida na ikungi ambao kwa pamoja wameazimia kutumia mbegu ya chotara na kuwaelimisha wakulima wenzao faida ya mbegu hizo.

Ameongeza kuwa makampuni mawili ya SDC na BYTRADE wamejiandaa kusambaza mbegu chotara kwa wakulima wa mkoa wa Singida huku akiwahakikishia wakulima kuwa wasambazaji hao wataleta mbegu kwa wakati ili wapande ndani ya msimu wa kilimo.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.