• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

Mfumo wa Kufundishia Masomo ya Sayansi Shule Za Sekondari Wafanyiwa Majaribio.

Posted on: February 25th, 2022

Mkoa wa Singida umejipanga kuboresha elimu na kuongeza ufaulu wa wanafunzi na kuondoa daraja la mwisho (sifuri) katika shule za sekondari kwa kuanzisha mfumo wa kufundishia masomo ya sayansi kwa shule ambazo zina uhaba wa walimu wa masomo hayo. 

Akizungumza wakati wa majaribio ya kufundisha kwa kutumia mfumo huo wa kijiditali yaliyofanyika hivi karibuni katika Shule ya Sekondari Mitunduruni iliyopo Manispaa ya Singida, Katibu Tawala Mkoa huo Bi Dorothy Mwaluko amesema Mkoa umepanga kuongeza uelewa na ufaulu kwa wanafunzi wa Sekondari kwa kutumia video zilizohifadhiwa kwenye vifaa mbalimbali kama flash ili kufundishia mashule ambayo hayana walimu wa masomo hayo.

Katibu Tawala huyo amesema kufundisha kwa njia ya video kunamfanya mwanafunzi kuelewa kwa haraka kupitia njia tatu za ufahamu ambazo ni macho kuona, masikio kusikia na kuhisi kwa kugusa au kuandika na kuwataka walimu wa masomo hayo kujiandaa kutumia mfumo huo wakati marekebisho kadhaa ya kuuboresha yanafanyika.

Aidha Dorothy amebainisha kwamba jumla ya shule 142 za Serikali ndizo zitakazofaidika na mfumo huo  hasa zenye walimu wachache wa masomo ya sayansi kama hisabati phizikia na Kemia.

“Mfumo huo unatazamiwa kutumika mara tu mapendekezo ya maboresho ya mfumo yaliopendekezwa na walimu na wanafunzi wa shule hii na nyengine zitakazopata bahati yakufanyiwa majaribio”. Alisistiza Mwaluko.

Naye Mkuu wa Shule ya Sekondari Mitunduruni Mwalimu Victoria Calist akishukuru ujio wa programu na shule hiyo kuchaguliwa kuwa ya kwanza kufanyiwa majaribio hayo, amesema mfumo utawasaidia shule ambazo hazina walimu wa masomo husika na kukazia maarifa kwa shule ambazo tayari wanawalimu.

Amesema kwa mkoa wa Singida kuna upungufu mkubwa wa walimu wa masomo ya Sayansi yakiwemo hisabati na phizikia jambo ambalo lilikuwa likipunguza ufaulu wa wanafuzi hivyo uwepo wa mfumo huo utaondoa changamoto hiyo.

Aidha Mkuu wa Shule huyo akaomba   wataalamu wa TEHAMA kusaidia video kupatikana kwa njia ya  flashi au DVD ili wanafunzi waweze kujifunza wakiwa majumbani au mashuleni .

Hata hivyo Mwalimu Victoria alimshuku Afisa Tawala Mkoa pamoja na Mkuu wa Mkoa Dk. Binilith Mahenge kwa  ubunifu huo ambao utasaidia  kuondoa changamoto ya upungufu wa walimu wa sayansi mkoani Singida.

Silivanus Mputa ni mtaalamu wa TEHAMA ambaye alishirikiana na Afisa TEHAMA wa Mkoa Bw. Baraka Mhembano katika utengenezaji wa mfumo huo hapa anasema, utengenezaji wa mfumo huo wa kufundishia kwa kutumia video na sauti kwa sasa wamefanikiwa kutengeza vipinda vya masomo ya Hisabati Kiswahili na Baiolojia ambayo ndiyo yaliyotumika kufanyia majaribio.

Silivanus amefafanua kwamba vipindi hivyo vimegawanyika katika sehemu tatu (3) ikijumuisha  vilivyotengenezwa kwa kuonesha picha na sauti (real class) ambapo Mwalimu anafundisha kwa kuonekana, njia ya pili ni vilivyotengenezwa kwa njia ya wasilisho ambavyo vinakuwa na maandishi picha za mnato na sauti.

Njia nyingene ni video amabazo zimetengenezwa kwa njia ya uhuishaji (animation) ambazo zote zimetengenezwa na program mbalimbali ikiwemo adobe Premiere na Adobe photoshop. Alifafanua Silivanus.

Katika zoezi la kutumia mfumo wa kufundishia wanafunzi wa sekondari  umehusisha wanafunzi wa shule ya Mitunduruni iliyopo Manisiapaa ya Singida ambapo Aisha Haji Abdalah mwanafunzi wa kidato cha nne A akaishukuru Serikali ya mkoa ambayo imepanga kuboresha elimu.

Aisha ameeleza kwamba matumizi ya mfumo wa kufundishia masomo ya sayansi kwa shule za sekondari umeonesha wazi kwamba nchi ipo katika uchumi wa kati ambao unahitaji matumizi ya teknolojia katika kusambaza na kukuza maarifa kutoka mtu moja hadi mwingine.

https://www.blogger.com/blog/post/edit/6903235629886141782/128137890106155353

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.