• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

MIZAHA KATIKA MIRADI YA MAJI HAITAVUMILIWA MKOANI SINGIDA.

Posted on: November 20th, 2017

  Ofisi ya Mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Singida imedhamiria kusimamia uboreshaji wa huduma za maji mkoani hapa huku mizaha itakayofanywa na mtu yeyote katika miradi ya maji, kutovumiliwa.

Kaimu Katibu Tawala Sehemu ya Maji Mkoa wa Singida Mhandisi Lyidia Joseph amebainisha hayo leo wakati wa kikao maalumu na Timu ya usimamizi wa sekta ya maji ya halmashauri ya Wilaya  ya Manyoni, kwa ajili ya kufuatilia usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maji.

Mhandisi Lydia amewaeleza wataalamu hao kuwa uongozi wa mkoa hautavumilia endapo kuna mtumishi yeyote atafanya mzaha katika kusimamia miradi ya maji kwakuwa mkoa umekuwa ukitoa ushirikiano wa kutosha hivyo hakuna sababu ya kushindwa kufanya vizuri.

“Sisi katika ngazi ya mkoa hatutavumilia mzaha katika masuala ya maji, tupo tayari kutoa ushirikiano popote mnapoona mnakwama ili tu tufikie malengo yetu ya kutoa huduma bora za maji kwa wananchi, hali ilivyo sasa hairidhishi kabisa, tufanye kazi kwa kasi zaidi”, ameongeza Mhandisi Lydia.

Amesema, halmashauri hiyo inapaswa kuhakikisha inatekeleza agizo la Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi la kuongeza asilimia ya upatikanaji wa maji katika halmashauri hiyo kutoka 45 hadi 72 ifikapo mwezi Juni, 2018 pamoja na kuandaa takwimu sahihi za upatikanaji wa maji ifikapo Disemba mwaka huu.

Mhandisi Lydia amefafanua kuwa halmashauri hiyo itaweza kuongeza asilimia ya upatikanaji maji na kufikia lengo la asilimia 72 endapo watendaji wote hasa wajumbe wa timu ya usimamizi wa sekkta ya maji, watashirikiana kusimamia ujenzi wa miradi mitano pamoja na ukarabati wa miradi minne iliyopo kwenye bajeti.

“Kila Mjumbe hapa ana kazi ya kufanya katika miradi hii ya Makanda, Nyaranga, Kikombo, Makutopola na Kicheho inayojengwa pamoja na ile ya Sanza, Mkwese, Londoni na Sorya inayokarabatiwa, Kitengo cha ugavi kisimamie taratibu za manunuzi zinafuatwa pamoja na kuhakiki ubora wa mkandarasi, mwanasheria aelekeze taratibu za kisheria, Maendeleo ya jamii ahakikishe wananchi wanaujua mradi vizuri, kila mmoja akitekeleza jukumu lake ipasavyo tutafikia lengo”, ameeleza na kuongeza kuwa,

“Idara ya maji msifanye siri miradi ya maji na kujifungia wenyewe hakikisheni timu hii ya usimamizi wa sekta yenu inafahamu vizuri miradi yote ya maji pamoja na kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo, mkifanya hivyo mtaenda kwa kasi na kazi itafanyika kwa ufanisi, sio kila kitu mfanye wenyewe tu”, ameongeza Mhandisi Lydia.

Aidha Mhandisi Lydia amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Charles Fussi kwa kujitoa kwake katika kusimamia na kutoa fedha za kusaidia miradi ya maji akitoa mfano wa kiasi cha milioni 16 zilizotolewa na mkurugenzi huyo kutoka katika makusanyo ya ndani kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa maji.

Naye Mhandisi wa Maji kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Athanas Nziku ameieleza timu hiyo kuwa usimamizi wa jumuiya za watumia maji ni jambo muhimu kwakuwa takwimu zimeonyesha jumuiya hizo zimekuwa zikikusanya pesa nyingi sambamba na matumizi makubwa ya fedha wanazokusanya.

Mhandisi Nziku amewafafanulia kuwa jumuiya hizo za watumia maji zinapokusanya fedha nyingi sambamba na kutumia fedha nyingi ni moja ya kiashiria kuwa miradi hiyo ya maji inaweza kufa hivyo wazitembelee na kuona tatizo liko wapi endapo liko ndani ya uwezo wa halmashauri liweze kutatuliwa mapema.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Mkwese na Mwenyekiti wa huduma za Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Robert Kenze amesema, halmashauri hiyo imedhamiria kuboresha huduma za maji ambapo ajenda ya maji imewekwa kipaumbele katika vikao vyote muhimu.

Kenze amesema wakuu wa Idara wa halmashauri hiyo watashirikiana na Idara ya maji wilayani humo huku wanasiasa wakiwa tayari kutoa elimu na kusimamia utekelezaji wa miradi ya maji.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.