• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

Msikii na Munkhola watakiwa kumaliza mgogoro wa ardhi kwa majidiliano.

Posted on: February 3rd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge amewataka wananchi wa kijiji cha Msikii Kata hiyo na Munkhola Kata ya Mgori wilaya Singida vijijini kutumia njia ya majadiliano na maridhiano katika  kutatua mgogoro wa matumizi ya ardhi unaowakabili.

Dkt. Mahenge ameyasema hayo hivi karibuni wakati alipofanya ziara ya kujifunza na kujionea eneo lenye mgogoro baina ya vijiji hivyo ambapo kijiji cha Munkhola wanataka eneo hilo libaki kama hifadhi ya Msitu wakati kijiji cha Msikii wakita litumike kwa ajili ya kilimo.

Aidha Dkt. Mahenge akiwa eneo hilo akawataka madiwani wa Munkhola na Msikii kukutana ili kujadili kwa kina athari zinazoweza kutokea endapo eneo hilo likitumika kwa kilimo au kwa hifadhi ya msitu ambapo watashirikiana na kamati iliyoundwa ili kupata suluhisho.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa akawasihi wananchi wa vijiji hivyo kuendelea kutunza amani utulivu na mshikamano wakati viongozi wao wakitafuta suluhisho la mgogoro huo huku akisisitiza mazao na miti iliyopandwa eneo hilo kuendelea kubaki mpaka muafaka utakapopatikana.

 “Sitapenda kusikia watu wamegombana au miti na mazao yameng’olewa wakati Serikali ipo, atakaye thubutu kuvunja amani sitakuwa na urafiki katika hilo.” Alisisitiza Dkt. Mahenge

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Singida vijiji  William Nyalandu akawasisitiza viongozi wa vijiji hivyo kufuata maagizo yaliyotolewa na Serikali ya kuhakikishi amani na utulivu vinakuwepo.

Hata hivyo Nyalandu akasisitizia kwamba mazao yaliyopo kutong’olewa na viongozi wahakikishe hakuna mkulima mwingine atakayeanzisha shamba jipya katika eneo hilo mpaka hapo Serikali itakapotoa muongozo.

Diwani wa Kata ya Munkhola Mhe. Dhuma Said akamuhakikishia RC Mahenge kwamba mgogoro huo utaisha kwa kutumia mijadala ya kawaida baina yao viongozi na hauwezi kwenda hatua za juu.

Hata hivyo Diwani huyo alieleza kwamba shughuli za kilimo na ufugaji zinazofanywa katika hifadhi ya msitu huo zinahatarisha maisha ya wananchi wanaozunguka eneo hilo na Mkoa kwa ujumla kwa kusababisha mmomonyoko wa udongo, jangwa na ukosefu wa mvua.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Msikii Mhe. Mchaga Mtegagufa akatumia muda huo kumueleza Mkuu wa Mkoa kwamba kutokana na mgogoro huo ng’ombe Sita kutoka katika kijiji cha Msikii wamekamatwa, majembe Mawili yakukokotwa na ng’ombe hayajulikani yalipo mpaka sasa.

Hata hivyo Diwani Mchaga akamuomba Mkuu wa Mkoa waachiliwe huru watu wawili wa kijiji hicho waliokamatwa ambapo Mkuu wa Mkoa alimwagiza Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa kuwaachia huru watu hao kwakuwa viongozi watakutana kwa ajili ya muafaka.

Ziara hiyo iliwahusisha Kamati ya Usalama ya Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Singida, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Mwenyekiti wa Halmashauri, Kamati maalum ya utatuzi wa migogoro na viongozi wa Chama cha Mapinduzi.

Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskas Muragili akimuonesha Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge mpaka wa msitu huo

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge akisikiliza maoni ya wananchi katika kijiji cha Munkhola

Wanachi wa kijiji cha Munkhola na Msikii wakiwa katika eneo la msitu wenye mgogoro wa matumizi ya ardhi

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.