• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

NMB IWASAIDIE WAFANYABIASHARA SINGIDA KUANZISHA KIWANDA CHA VIFUNGASHIO; DKT NCHIMBI.

Posted on: September 18th, 2017

  Benki ya NMB imetakiwa kuwasaidia wafanyabiashara Mkoani Singida kuanzisha kiwanda cha kutengenea vifungashio, ili waweze kuhifadhi bidhaa zao katika ubora unaokubalika kitaifa na kimataifa.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi ametoa rai hiyo mapema leo wakati akifungua warsha ya siku moja ya klabu ya wafanyabiashara wateja wa NMB, katika ukumbi wa Kanisa Katoliki mjini Singida.

Dkt Nchimbi amesema klabu hiyo ya wafanyabiashara itaweka alama kubwa katika maendeleo endapo watajipanga na kuanzisha kiwanda cha kutengeneza vifungashio hivyo kuliko kuendelea kuvifuata nje ya Singida au nje ya nchi.

“Uzoefu usipotumika vizuri unaweza ukawa kikwazo cha kuendelea, msizoee kufuata vifungashio na label nje ya singida wakati fursa ipo ya kuanzisha kiwanda hicho Singida”, amesema na kuongeza kuwa,

“Wafayabiashara mzipende biashara zenu na kuziweka katika hali ya usafi na yenye kuvutia, wengine wanapenda kujisafisha na kujipendezesha wenyewe lakini ukiangalia biashara zao hazivutii, zimewekwa tu bila kufungashwa vizuri”, amesisitiza.

Aidha amewataka wafanyabiashara wasiogope kukopa kwakuwa sio jambo la aibu wala fedheha, ila kinachotakiwa ni kuwa na nidhamu ya mkopo na malengo ili waweze kufanikiwa.

“Akina mama jifunzeni kuwa na nidhamu ya mkopo, sio unakopa leo mara unasikia kapu la mama, jifikirie hayo ndio malengo ya huo mkopo hata kama ni jambo muhimu?, nidhamu ya mkopo inatakiwa ianze kabla ya kukopa na iendelee kuwepo.

Dkt Nchimbi pia ameishukuru benki hiyo kwa kushirikiana na serikali katika mambo mbalimbali ya kielimu na afya, pia amewashukuru kwa kutoa mikopo kwa watumishi wa umma jambo ambalo linawasiadia katika mambo mbalimbali.

Naye Meneja wa NMB Kanda ya kati Straton Chilongola amesema klabu za wafanyabiashara nchini ziko 34 ambazo zimekuwa zikipatiwa mafunzo mikopo kutoka katika benki hiyo.

Chilongoloa amesema benki hiyo imekuwa ikitoa mafunzo juu ya ulipaji kodi, ujasiriamali, masuala ya mitaji, leseni na ardhi ili wafanyabiashara hao waweze kukuza mitaji yao.

Amesema benki hiyo imefanikiwa kuwakuza wafanyabiashara wengi ambazo wameanza nao wakiwa wafanyabiashara wadogo ambapo sasa wamekuwa wakubwa na wakati huku wakiajiri wengine na hivyo kukuza uchumi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa klabu ya wafanyabiashara wateja wa NMB Singida Emmanuel Rweyemamu Kyoma amesema wazo la kuanzisha kiwanda cha kutengeza vifungashio wamelipokea vizuri huku wakijipanga kuandaa andiko kwa ajili ya kiwanda hicho.

Kyoma amesema kwa ushirikiano na NMB kiwanda hichokitaweza kujengwa Singida huku wakimuahidi Mkuu wa Mkoa kuwa Mkoa wa Singida utazalisha chakula cha kutosha kulisha Mkoa wa Dodoma.

Amesema benki ya NMB imekuwa ikishirikiana na wafanyabiashara hao hivyo mipango ya kukuza uchumi kama huo wa kuanzisha viwanda utatekelezeka bila matatizo yoyote.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.