• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

RAS Singida atembelea Hospitali, vituo vya Afya

Posted on: November 8th, 2022

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Mwl. Dorothy Mwaluko leo tarehe 8.11.2022 ametembelea Hospitali, vituo vya Afya na Zahanati vilivyopo Wilaya ya Singida vijijini na Mkalama ili kuona huduma za afya zinavyotolewa katika maeneo hayo.

 Akiwa katika ziara hiyo amekagua Watumishi na utendaji kazi wao vitendea kazi pamoja na usafi wa mazingira yanayozunguka maeneo hayo.

Dorothy akiwa katika Kituo cha Afya cha Kinyangiri kilichopo kata ya Kinyangiri Wilayani Mkalama  amewaagiza Waganga wafawidhi katika Hospitali, Zahanati na vituo vya Afya kusimamia huduma stahiki kwa wagonjwa, maadili ya kazi na utunzaji wa mazingira ya nje na ndani ya Hospitali ili kuboresha mandhari ya maeneo hayo.

"Nataka mpande miti katika maeneo yenu na pia nataka kuwe na utaratibu wa upangaji wa vitu Hospitalini (classification) kama ulivyo utaratibu" alisema Mwaluko

Katibu Tawala huyo akiwa Kinyangiri akamuagiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida Daktari Victorina Ludovick kuhakikisha gari la wagonjwa aina ya landrova linafanyiwa matengenezo haraka ili liweze kutumika kwa ufanisi mkubwa.

Hata hivyo Mwaluko akaagiza kuanza kutumika majengo yote ambayo fedha za umma zimetumika zikiwemo nyumba za wafanyakazi wa sekta ya Afya kuanza kutumika haraka iwezekavyo.

Aidha akawataka viongozi wa Idara ya Afya Mkoani hapo kutafuta miradi mbalimbali ambayo itawasaidia kuendesha shughuli mbalimbali badala ya kutegemea fedha za Serikali.

Aidha ameiagiza timu ya  usimamizi na uendeshaji wa huduma za Afya ya Mkoa huo  (RHMT) kuwatembelea watumishi wa Afya mara kwa mara ili kuwafariji na kuona na kutatua changamoto zinazowakabili.

Naye Mganga mfawidhi wa Kituo cha Kinyangiri Daktari Anna Kimonga akamueleza Katibu Tawala Mkoa kwamba  Kituo hicho kinapokea  Wagonjwa kati ya 30 mpaka 50 na wanawake wanaojifungua ni kati ya 25 mpaka 30 kwa mwezi ambapo ameeleza kwamba ni muhimu kuwa na gari la Wagonjwa lenye uwezo wa kufanya kazi kulingana na mazingira.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mkalama  Daktari  Dorisila John amesema  upatikanaji wa dawa na vifaa tiba katika Wilaya hiyo unaridhisha huku akibainisha kwamba kwa mujibu wa muongozo bado Kkna uhitaji wa madaktari na wauguzi katika vituo vingi vya Afya na Zahanati Wilayani hapo.

Dorisila amesema katika Hospitali ya Wilaya ya Mkalama mpaka kufikia tarehe 16 Novemba, 2022 ufungaji wa vifaa vya X-Ray utakuwa umekamilika jambo ambalo wanategemea kwamba huduma za mashine hiyo zitaanza hivi karibuni.

Ziara hiyo ya Katibu Tawala Mkoa wa Singida aliambatana na timu ya usimamizi na uendeshaji wa huduma za Afya Mkoa (RHMT) ambapo walitembelea Zahanati ya Kanisa Katoliki Iguguno, Kituo cha Afya Kinyangiri, Hospitali ya Wilaya ya Mkalama, Hospitali ya rufaa ya Iambi, Hospitali ya Wilaya ya Singida na Kituo cha afya Ilongero.

Mwisho

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.