• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

RAS SINGIDA, DKT. ANGELINA LUTAMBI, AMEZINDUA KAMPENI YA MAPAMBANO DHIDI YA SARATANI NA KUWATAKA WANANCHI KUWA NA UTARATIBU WA KUPIMA AFYA. .

Posted on: May 29th, 2019

Serikali mkoani Singida, imewataka wananchi kuwa na utaratibu wa kupima afya zao mara kwa mara ili kubaini magonjwa ambayo yanachukua muda mrefu kujitokeza, na kuacha tabia ya mtu kusubili hadi afya iwe na mgogoro ndipo akapime.

Agizo hilo limetolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt. Angelina Lutambi, wakati akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa kampeni ya mapambano dhidi ya Saratani mkoani Singida.
Dkt. Lutambi amesema, ugonjwa wa Saratani ukibainika katika hatua zake za awali, upo uwezekano wa kutibika endapo mgonjwa atazingatia kikamilifu ushauri wa wataalamu.
“Ni vema kila mmoja wetu kuwa na desturi ya kupima afya mara kwa mara ili kutambua hali ya kiafya. Endapo utatambulika una ugonjwa wa Saratani, hakikisha unapata huduma za afya kulingana na ushauri utakaopewa  na wataalamu wa Afya”.
Amesema, wale waliokwisha jitambua kuwa na saratani, waendelee kutumia  huduma za afya ili kuepuka athari zitokanazo na ugonjwa huo hatari wa saratani.

Akitaja baadhi ya vyanzo vya ugonjwa wa saratani, Dkt. Lutambi amesema, vyanzo vikubwa vya saratani ni pamoja na matumizi ya tumbaku na bidhaa za ugoro.

“Matumizi ya tumbaku ni kisababishi kikubwa cha magonjwa ya Saratani ya Matiti, mdomo, koo pamoja na ugonjwa wa moyo. Pia unywaji wa pombe  uliopitiliza kusababisha magonjwa ya Saratani ya Matiti, Ini, Utumbo mpana, pamoja na saratani nyingine.
Aidha, amewataka wananchi kujiepusha na visababishi vya ugonjwa huo wa Saratani kwa kuwa ni ugonjwa hatari kwa maisha ya binadamu.
Katibu Tawala huyo wa Mkoa wa Singida, kwaniaba ya wananchi wa mkoa wa Singida, ameishukuru taasisi ya Saratani ya hospitali ya Ocean Road ya jijini Dar es salaam kwa kutuma madaktari kuja kutoa huduma za kitabibu kwa wakazi wa mkoa wa Singida.
Awali, Meneja kitengo cha uchunguzi wa Saratani hospitali ya Ocean Road, Dk. Maguha Stephano, amesema pamoja na kutoa huduma ya afya, pia wametoa mafunzo ya awali  juu ya kutambua saratani kwa baadhi ya wataalamu wa afya mkoa wa Singida, lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wa kutambua saratani.


“Taasisi yetu ya Ocean Road inatembea kwa maono ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya TANO, Dkt John Magufuli na ya utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambayo ni Watanzania kuwa na afya njema”. Dk. Maguha Stephano.
Wakati huo huo mkazi wa Mtaa wa Munugh’una Manispaa ya Singida, Bi. Mwanaidi Kipandwa, ameishukuru taasisi ya Ocean Road, kwa uamuzi wake wa kusogeza karibu huduma ya utabibu kwa kuitoa bure kwa wakazi wa mkoa wa Singida.
“Wengi wetu hapa tulipo  kufika Dar es salaam ni mtihani mkubwa. Naiomba taasisi ya Ocean Road isichoke, ijenge utaratibu wa kuleta au kusongeza  huduma hii muhimu sana kwetu sisi tusio na  uwezo wa kufuata huduma za matibabu Dar es salaam”, Amesema Bi. Mwanaidi Kipandwa.


Kampeni hii inatekelezwa kwa siku tano mkoani Singida na timu ya wataalamu kutoka hospitali ya Ocean Road ya jijini Dar es salaam.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.