• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

RC DENDEGO AWAAHIDI NEEMA WALIMU, AHIMIZA KUENDELEA KUFANYA KAZI KWA BIDII ILI KUONGEZA UFAULU NCHINI

Posted on: May 16th, 2024

Mkuu wa mkoa wa Singida Mheshimiwa Halima Dendego, amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya mkoani humo kuhakikisha wanatatua changamoto na matatizo mbalimbali yanayowakabili Walimu katika maeneo yao ili kuongeza ari katika ufundishaji na ufaulu wa wanafunzi mashuleni.

Dendego, ametoa maagizo hayo (tarehe 16 Mei, 2024) katika ufunguzi wa Kongamano la Siku Mbili la Walimu kutoka mikoa ya Kanda ya kati na Kaskazini ambao wamekutana mjini Singida kujadili masuala mbalimbali yanayoikabili sekta hiyo ikiwemo namna bora ya kutetea maslahi yao na kuweka mipango na mikakati madhubuti ya kuongeza maradufu ufundishaji na ufaulu katika maeneo yao ya kazi.

Aidha, Mkuu huyo wa mkoa amesisitiza kuwa matatizo mengi yanayowakabili Walimu yanaweza kutatuliwa na Viongozi waliopo ngazi za Wilaya kwa kukaa pamoja na kujadili kwa kina namna bora ya kutafuta majawabu sahihi ambayo yataongeza ari ya Walimu kufundisha na kupandisha ufaulu kwa wanafunzi.

Amesema Serikali ya awamu ya Sita imefanya mambo makubwa katika sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya Elimu hivyo ni muhimu kwa Walimu kote nchini kumuunga mkono Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuhakikisha wanafanya kazi kwa bidii na kwa ubunifu mkubwa ili kutengeneza Wanafunzi bora ambao watalisaidia Taifa kusonge mbele Kimaendeleo haraka.

Kuhusu maadili ya Wanafunzi, Mheshimiwa Halima Dendego, amewahimiza Walimu kuhakikisha wanawalea wanafunzi katika njia sahihi kwa kuzingatia mila na desturi za kitanzania ili kuwaepusha na matatizo ya utovu wa nidhamu.

Hata hivyo, Dendego, amewataka Walimu kutoa adhabu stahiki kwa wanafunzi wanaoenda kinyume na taratibu za shule kwa kuzingatia kanuni na taratibu zilizopo nchini ili kuhakikisha wanafunzi wanaomaliza shule au vyuo wanakuwa na maadili mazuri yanayompendeza Mwenyezi Mungu, Jamii na Taifa kwa ujumla.

Naye, Katibu Tawala wa mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga, amewataka Walimu kuzingatia kanuni na taratibu katika malezi ya wanafunzi ili kukabiliana na tatizo la mimba kwa wanafunzi jambo ambalo amesema halipendezi hata kidogo.

Dkt. Fatuma Mganga, amewahimiza Walimu kuongeza bidii na ubunifu katika ufundishaji ili kuhakikisha Taifa la Tanzania linapata Watalaamu wazuri na wabobezi ambao watasaidia nchi kusonga mbele kimaendeleo haraka.

Kwa upande wake, Rais wa Chama cha Walimu Tanzania -CWT- Leah Ulaya, ameiomba Serikali kuendelea kushughulikia matatizo yanayowakabili Walimu ikiwemo ulipaji wa madeni na upandishaji wa vyeo kwa wakati jambo ambalo amesema litasaidia Walimu kufanya kazi zao kwa ufanisi na kuongeza ufaulu kwa wanafunzi.

Rais huyo pia amewahakikishia Viongozi wa mkoa wa Singida na Taifa kwa ujumla kuwa wataendelea kufanya kazi kwa bidii kwa sababu wanaimani na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na mwanamama shupavu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, inafahamu kilio chao na itaendelea kutatua changamoto zinazowakabili kwa haraka.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.