• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

RC Mahenge atembele ujenzi wa Barabara ya Rungwa, Itigi na Mkiwa, awataka wananchi kutunza Mazingira.

Posted on: November 10th, 2021

Wananchi wa Halmashauri ya Itigi katika Kata ya Rungwa wametakiwa kutunza Mazingira kwa kupanda miti ambayo itasaidia kupunguza uharibifu wa Mazingira na kulinda  barabara  ambayo inaendelea kutengenezwa.

Kulingana na Mazingira ya Rungwa Barabara zimekuwa zikiharibika kutokana na kukatwa  miti  na kusababisha mmomonyoko wa ardhi na maji kuhama katika mikondo yake.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge ameyasema hayo tarehe 9.11.2021 alipofanya ziara ya kukagua barabara ya Rungwa, Itigi na Mkiwa yenye urefu wa Kilomita zaidi ya 200.

Akiongea akiwa katika daraja la Rungwa ambalo ni mpaka kati ya Singida na Mbeya Mkuu wa Mkoa amesema barabara hiyo ni muhimu katika kukuza uchumi kwa kuwa inaunganisha mikoa mitatu ya Mbeya, Singida na Tabora ambapo itasaidia kuongeza mzunguko wa kibiashara katika  mikoa hiyo.

Amesema kukamilika kwa Barabara hiyo kunatoa fursa ya kuunganisha Tanzania, Zambia na Malawi ambazo zote zinatumia nchi za maziwa makuu kufanya Biashara ikiwa ni pamoja na  nchi nyingine za Afrika mashariki ambapo zitaongeza muingiliano wa shughuli za kibinamu.

Amesema utunzaji wa Mazingira utasaidia kulinda kingo za mito zisiweze kuvunja barabara ambapo amesema kwa kutunza Mazingira kutasaida kupata fedha za kigeni kwa kupunguza hewa ya ukaa Nchini.

Akimnukuu Rais wa Jamuhuri ya Muungano Mama Samia Suluhu, MKuu wa Mkoa wa Singida amesema  Tanzania imeingia makubaliano ya kutunza na kuhifadhia Mazingira ambapo mikataba mbalimbali imesainiwa hivyo ni jukumu la kila mtanzania kutunza na kuhifadhia mazingira.

Amewakumbusha wananchi kutuza Mazingira  kwa kupanda miti katika maeneo yote ili kuzuia uchepushaji wa maji ya mvua ambayo yamekuwa yakiharibu Barabara.

Aidha ametoa wito kwa wakandarasi hao kuhakikisha kila mmoja anamaliza kazi yake kabla ya kuingia katika kipindi cha mvua nyingi  ili kutozuia shughuli mbalimbali za wafanyabiashara na wasafiri.

Awali akieleza Hali ya mradi huo Mhandisi Matare Masige, Meneja wa TANROAD Mkoa wa Singida amesema Mradi unagharimu kiasi cha sh.Bilion 1.5 na unatekelezwa na wakandarasi watatu na utawasaidia wananchi wa mikoa ya Sikonge, Manyoni na Mbeya pamoja na mikoa ya jirani.

Amesema barabara hiyo imegawanywa katika vipande vitatu kulingana na idadi ya wakandarasi ambao ni M/s Jam Engineers ambayo italipwa kiasi cha sh.milioni 348.3 na M/s Madata In.Ltd ambayo imeingia mkataba wa Milioni 592.7 wakati Kampuni ya M/S JP Treders Ltd imeingia mkataba wa Sh. Milioni 567.93

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge (kushoto) akizungumza Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida Alhaji Juma Kilimba wakati wa ziara ya ukaguzi wa barabara ya Rungwa - Itigi iliyofanyika hivi karibuni

Meneja wa TANROAD Mkoa wa Singida Mhandisi Matare Masige (kushoto) akielezea jambo wakati wa ziara.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.