• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

RC SERUKAMBA ATANGAZA MSAKO WA KUKAGUA MIRADI BILA KUPANGIWA

Posted on: October 26th, 2023

MKUU wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba ametangaza rasmi msako wa kutembelea miradi yote ya  maendeleo inayotekelezwa na Serikali katika Mkoa huo kwa lengo la kujiridhisha na utekelezaji wa miradi hiyo bila kuchaguliwa mradi wa kukagua.

Mkuu huyo wa Mkoa wa Singida amesema hayo jana tarehe 25 Oktoba, 2023 mara baada kuhitimisha ziara yake ya ukaguzi wa miradi katika Wilaya ya Singida, hatua hiyo ya kutembelea mradi mmoja baada ya mwingine kila Wilaya ni kutaka kuhakikisha utekelezaji wa miradi hiyo unafanyika kwa kiwango kinachotakiwa pamoja na ubora kwa thamani ya fedha iliyotolewa katika mradi husika ili wananchi wapate huduma bora na ya kiwango kinachostahili.

Akizungumza na Watendaji wa Mkoa huo Serukamba amesema Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imekuwa ikitoa fedha nyingi na kwa wakati kwa ajili ya maendeleo hivyo ni lazima ikatekelezwa kwa muda uliokusudiwa kwa manufaa ya Watanzania.

"Nitangaze kuwa baada ya wiki moja nitaanza ziara ya kutembelea mradi mmoja baada ya mwingine na sitahitaji kupangiwa ni mradi gani wa kutembelea nitahakikisha nafika kwenye kila mradi ambao unatekelezwa na nitatembelea miradi yote katika Halmashauri zote za Mkoa wa Singida”

"Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri zote za Mkoa huu na Waandisi hakikisheni mnajipanga vyema ni lazima miradi yote itekelezwe kwa wakati na nyie Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na Waandisisi nawaeleza msipende kukaa maofisini na kusubiria taarifa fikeni kwenye maeneo ya kazi kwa lengo la kuona kazi zinaendeleaje”

"Na wakati mwingine siyo kufika tu na kukagua kagua na mpango kazi wa Mkandarasi anayefanya kazi na ikitokea ukarudi ukakuta hajatekeleza makubaliano unaweza kubadilisha Mkandarasi mwingine na mafundi wengine lengo kubwa ni kazi kufanyika kwa kiwango na kwa ubora unaohitajika ili ikamilike kwa wakati" ameeleza Serukamba.

Hata hivyo Mkuu huyo wa Singida ameeleza kuwa kwa hatua ya sasa miradi ya afya inaendelea vizuri na inaridhisha lakini miradi ya elimu inatakiwa kuharakishwa zaidi na ifikapo mwezi Desemba mwaka huu iwe imekamilika kwa lengo la wanafunzi watakaoingia shule ya awali na kidato cha kwanza wawe na uhakika wa miundombinu yote ya shule.

Singida ni kati ya Mkoa ambao umepokea fedha nyingi za miradi ya maendeleo na ni miongoni mwa Mikoa ambayo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amefurahishwa na utekelezaji wa miradi hiyo.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.