• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

"MABIBO YAMEANZA KUANGUKA NA WATU WANAYAOKOTA NI DALILI NZURI YA MAENDELEO YA SHAMBA LETU LA MASIGATI MANYONI" - RC SINGIDA

Posted on: November 13th, 2019

MKUU wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi amekagua shamba la mfano la korosho lenye ukubwa wa ekari 12,000 lililopo Kijiji cha Masigati, Halmashauri ya wilaya Manyoni mkoani Singida na kueleza kuwa linaendelea vizuri.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukagua shamba hilo wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku moja ya kukagua shamba hilo Dkt. Nchimbi alisema kuwa linaendelea vizuri na linaleta matumaini makubwa.

“Hivi sasa mabibo yameanza kuanguka na watu wanayaokota ni dalili nzuri ya maendeleo ya shamba letu na kazi inayoendelea katika shamba hili ni kufanya usafi tayari kwa msimu huu” alisema Nchimbi.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi, akionesha mabibo aliyoyaokota kwenye shamba la mfano la korosho lenye ukubwa wa ekari 12,000 lililopo Kijiji cha Masigati, wilayani Manyoni wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku moja ya kukagua shamba hilo.

Dkt. Nchimbi aliongeza kuwa katika msimu huu wanatarajia kupanda ekari zote 12,000 kwani mbegu zipo tayari na zipo za kutosha.

Akizungumza na wananchi na baadhi ya watumishi wa Halmashauri hiyo waliokuwepo katika shamba hilo wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Singida Oktoba 4, 2019, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alimpongeza Dkt. Nchimbi kwa kulibeba wazo la kuanzisha shamba hilo na kuhakikisha linatimia.

“Nimpongeze Mkuu wa Mkoa kwa kulibeba jambo hili, lakini nikuombe wewe na viongozi wenzako mhamasishe wengine walime zaidi zao hili kwa sababu korosho ni zao kubwa duniani na lina bei nzuri kimataifa,” alisema.

Alisema anatambua kwamba timu ya wataalamu kutoka kituo cha utafiti wa kilimo cha Naliendele mkoani Mtwara imeshawasili Manyoni ili kufanya utafiti wa zao hilo na jinsi linavyoweza kuzaa mara mbili kwa mwaka.

“Kwa kawaida, mkorosho mmoja unatoa kilo 40 za korosho kwa msimu mmoja, kwa hiyo kwa misimu miwili mtapata kilo 80. Ninawasii limeni korosho kwa ajili ya watoto wenu ambao wako darasa la pili au la tatu. Mkulima ukianza kuvuna, utaendelea kuvuna kwa miaka 20 mfululizo na kwa hiyo hao watoto hawatahitaji kulipiwa ada wakiwa chuo kikuu sababu korosho itakuwa inawalipia,” alisema.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu aliwataka wakulima wanaolima zao hilo wilayani Manyoni, waunde Ushirika wao ambao utawasaidia kuagiza dawa kwa pamoja ama kuuza kwa pamoja.

Hivyo, alimwagiza Afisa Ushirika wa Wilaya hiyo, Yusta Philipo ahakikishe anasimamia jambo hilo kuanzia sasa.

Akitoa taarifa juu ya mradi huo mbele ya Waziri Mkuu, Meneja wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) Kanda ya Kati, Ray Mtangi alimweleza Waziri Mkuu kwamba mradi wa kilimo cha korosho unajumuisha mashamba makubwa mawili ambapo shamba la Misigati lina ukubwa wa ekari 7,000 na lile la Mikwese lenye ukubwa wa ekari 5,000.

Alisema watu mbalimbali wakiwemo viongozi wa kitaifa wamekuwa wakifika shambani hapo ili wajifunze mbinu mpya za kuzalisha korosho kwenye maeneo yao. “Wiki mbili zilizopita, Mheshimiwa Spika na madiwani wa Kongwa walipita hapa ili kujifunza zao hili,” alisema.

Pia alisema Halmashuri yao imetenga eneo la ujenzi wa viwanda na kwamba hadi sasa wanazo ekari 50 kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vya kubangua korosho.

Mapema, Waziri Mkuu alikagua shamba hilo na kujionea hali halisi ya shambani ikoje. Pia alioneshwa mabibo na korosho ambazo zimevunwa kutoka kwenye shamba hilo la mfano, kutoka

kwenye mashamba ya wakulima ambao walipanda miche tangu januari mwaka jana.

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi (kulia) akiwa na Mkaguzi wa Ndani wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni, Aderaide Rweikiza wakiokota mabibo katika shamba hilo. 

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.