• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

Serikali kuendeleza kutoa matibabu Bure kwa Wazee

Posted on: October 1st, 2021

Serikali itaendelea kusimamia utoaji wa matibabu kwa Wazee bila malipo, upatikanaji wa dawa Hospitalini  na uwepo wa dirisha maalum kwa ajili ya Wazee ili kuwaenzi na kuwaondolea usumbufu.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mkuu wa  wilaya ya Singida Mjini Mhandisi Paskasi Muragili kwaniaba ya Mkuu wa mkoa wa Singida wakati wa Maadhimisho ya Siku ya wazee Duniani yaliyofanyika mjini Singida.

 Amesema Serikali itaendelea kutoa huduma kwa wazee pasipo kuchangia gharama za matibabu na kuboresha changamoto ambazo zimejitokeza katika utoaji wa huduma hiyo kwa kundi hilo.

 "Sisi sote ni mashahidi wa utolewaji wa huduma za Afya bila malipo kwa Wazee wote. Nitoe wito kwenu kufika kwenye vituo vya huduma za Afya vya Serikali ili kupatiwa huduma bila kuchangia gharama za matibabu".

Aidha Mkuu huyo wa wilaya amewaagiza Wakurugenzi wa halmashauri zote mkoani humo kuendelea kuwachangia wazee wasio na uwezo na kuwaunganisha kwenye Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa (iCHF) na wale wenye uwezo wa kujiunga wenyewe amewahamasisha wajiunge ili kuendelea kuboresha huduma za Afya.

Awali Mwenyekiti wa umoja wa Wazee hao SAWATA Bw. Ramadhani Juma Moghu ameishukuru Serikali kwa hatua walizoendelea kuzichukua katika kuimarisha Sekta hasa kwa wazee.

Akijibu hotuba ya wazee hao Mkuu huyo wa wilaya amewataka Maafisa maendeleo ya jamii wa kila Halmashauri kuwashauri wazazi  ambao watoto wao wanaolelewa na wazee kuona umuhimu wa mtoto kuishi na mzazi ili  kuwapunguzia majukumu.

Amesema Wazee wengi wameachiwa watoto na watoto wao au wajukuu. Malezi ya watoto hao ni jukumu la wazazi wao hivyo ni vema tukawaelimisha watoto na wajukuu zetu juu ya umuhimu wa malezi ya Wazazi kwa watoto. Alisistiza Muragili

 "Kwa kuwa kila Halmashauri kuna Ofisi za Ustawi wa Jamii niwaombe mfike ili wazazi hawa waweze kuwajibika kama Sheria ya Mtoto Na. 21 ya Mwaka 2009 inavyoelekeza".

“Nitoe shukrani kwa viongozi wa Baraza la Wazee mkoa na Viongozi wa SAWATA katika kufanya maandalizi na kufanikisha maadhimisho haya.  Aidha, nazishukuru Taasisi zote zilizoweza kutoa michango yao ya hali na mali katika kuwezesha maadhimisho haya”.  Alimalizia Muragili.

Mkuu wa Wilaya ya Singida mjini Mhandisi Paskasi Muragili (kulia) akitembalea banda la Wazee wajasiriamali katika 

maadhimisho ya siku ya Wazee Duniani yaliyofanyika leo mkoani Singida

Mwenyekiti wa umoja wa Wazee hao SAWATA Bw. Ramadhani Juma Moghu akisistiza jambo wakati wa maadhimisho hayo 

Mkuu wa Wilaya ya Singida mjini Mhandisi Paskasi Muragili (kulia) akikabidhi Mwongozo wa majukumu ya Mabaraza ya Wazee ngazi ya vijiji, mtaa, kata, wilaya na mkoa na Taifa kwa viongozi wa Mabaraza wakati wa madhimisho hayo

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Mwalimu Dorothy Mwaluko (wa pili kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa umoja wa Wazee hao (SAWATA) muda mfupi kabla ya kuanza kwa hafla ya maadhimisho ya siku ya Wazee Duniani yaliyofanyika leo mkoani Singida 

Burudani zikiendelea

Picha ya pamoja

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.