• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

*SINGIDA YA VIWANDA UHAKIKA WA AJIRA NA SOKO LA ALIZETI*

Posted on: October 25th, 2024

Ajira Zaidi ya 190 za moja kwa moja na ajira 400 zisizo za moja kwa moja zinatarajiwa kunufaisha wakazi wa Mkoa wa Singida huku wakulima zaidi ya 26000 kunufaika na mradi wa kiwanda cha mafuta cha Wild Flower Grains&Oil Mill Company Limited kupitia uwekezaji mkubwa wa kimkakati uliokamilika kwa asilimia 95 mpaka sasa.

  Mhe.Jerry Silaa Waziri wa habari na mawasiliano na teknolojia ya habari,alipotembelea kiwanda hicho leo hii amesema ni wakati sasa wa Tanzania kupunguza kuagiza bidhaa nje ya nchi kwani maendeleo ya viwanda yatarahisiaha uchakataji,na upatikanaji wa bidhaa mbali mbali ikiwemo mafuta ya kupikia ambayo yatainua maisha ya wengi katika mchakato wa kupata malighafi kutoka kwa wakulima wa mazao,wasafirishaji mazao,na wauzaji wa bidhaa za kiwandani.

             Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe.Halima Dendego akizungumza katika ziara hiyo amewakaribisha wawekezaji kuwekeza katika Mkoa wa Singida kwani ni mahali salama na upatikanaji wa umeme na mazao ya biashara kama alizeti na vitunguu.

Amesisitiza wawekezaji wa ndani kujitokeza kayika kuwekeza katika fursa hizo za biashara kwa kuiga mfano wa wawekezaji wazawa wa kiwanda hocho cha mafuta kwani wamethubutu na wameweza kuifanya Singida kupiga hatua katika maendeleo ya viwanda.

"Wawekezaji wa ndani waje kujifunza hapa kwetu Singida kwani wataalam wetu wote katika kiwanda hiki kuanzia ujenzi wa msingi wa kiwanda hiki ni vijana wetu wazawa wa hapa hapa Tanzania wakitengeneza bidhaa na kuendesha mashine"

Akiwasilisha taarifa ya mradi wa kiwanda hicho cha mafuta Jamal Shaban,amesema kuwa mipango ya baadae ya kiwanda hicho ni kufanya utanuzi wa kiwanda na kuongeza mashine za kusaga mahindi ili kupata unga na kuongeza mashine za kukoboa mpunga ili kupata mchele kwa lengo la kuongeza thamani ya mazao yanayozalishwa hapa nchini ili kuweza kuuza bidhaa zilizoongezwa thamani.

"Kwa kuongeza mashine za kusaga na kukoboa mahindi na mpunga tutaongeza thamani ya mazao yetu yanayozalishwa hapa nchini na kuuza bidhaa bora zilizoongezwa thamani".alisema Jamal

Wamiliki wa kampuni inayotekeleza nradi huo ni wazawa wenye uzoefu wa zaidi ya miaka 18 katika uwekezaji wa miradi ya kilimo na viwanda huku mradi huo ukiwa na thamani ya zaidi ya shilingi Bilioni 63 wakiwa na uwezo wa kusaga tani 225 za mbegu za alizeti kwa siku ikiwa matarajio ya uzalishaji wa mafuta kwa siku ni tani 75 na tani 2,250 kwa mwezi ambayo yatauzwa ndani na nje ya Mkoa wa Singida.


Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • "SINGIDA IMEJIPANGA KUONGOZA UFAULU KITAIFA":RC DENDEGO

    June 04, 2025
  • MRADI WA TACTIC KULETA NEEMA MANISPAA YA SINGIDA.

    June 02, 2025
  • "WAHITIMU MSIBWETEKE,JIENDELEZENI KATIKA FANI ILI MJIAJIRI"-DKT.MGANGA

    May 30, 2025
  • DKT.MGANGA:"WATUMISHI MSIKUBALI KUTUMIKA VIBAYA,KUWENI NA UTAMBULISHO MZURI"

    May 27, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.