• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

Takwimu za wananchi wanaopata chanjo mkoani Singida zaongezeka kwa kasi

Posted on: October 6th, 2021

Takwimu za wananchi wanaopata chanjo ya Uviko19 mkoani Singida zimeendelea kuongezeka kwa kasi kufuatia jitihada za utolewaji wa elimu na ushawishi kwa jamii kwa njia ya  nyumba kwa nyumba.

Akiongea wakati wa kikao kazi cha Kamati ya Afya ya msingi (PHC) kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mkuu wa Mkoa, RC Dkt. Binilith Mahenge amesema wiki mbili kabla ya kuanzishwa Mpango Shirikishi na Harakishi kwa ajili ya utoaji wa chanjo ya Uviko 19 idadi ya watu waliokuwa wakijitokeza kuchanja ilikuwa 5800 mpaka 6000 kwa Halmashauri zote za Mkoa wa Singida kabla ya tarehe 22 Septemba mwaka huu.

Dkt. Mahenge amesema Mpango Shirikishi na Harakishi ambao uelimishaji ulikuwa unafanywa nyumba kwa nyumba  ulianza tarehe 22 Septemba  2021 katika Halmashauri zote saba 7 za Mkoa wa Singida ambapo ulisaidia kuongezeka idadi ya watu wanochanja  mpaka kufukia 11,847 ilipofika tarehe 5.10.2021 kwa Mkoa mzima.

Aidha Huduma ya mkoba na kliniki tembezi zimesaidia kuwafikia wananchi wengi katika minada mbalimbali mashuleni na maeneo ambayo hayakuwa na vituo vya kutolea huduma ya chanjo. Alibainisha Dkt. Mahenge.

Hata hivyo Dkt. Mahenge ametumia Kikao hicho kuendelea kuwaomba wadau na taasisi mbalimbali kusaidia upatikanaji wa usafiri wa kuwafikisha watoa huduma ya chanjo vijijini ili kuendeleza kutoa Kinga ya ungonjwa huo.

Amewataka wahudumu wa Afya na watumishi mbalimbali wanaohamasisha jamii kuhusu kuchanja na kuendeleza kufanya hivyo Mara kwa Mara kwa kuwa wananchi  wanakawaida ya kusahau.

Pamoja na mambo mengine wadau walikuwepo katika mkutano huo wamemuomba RC kushirikiana na wadau mbalimbali na mashirika yasiyo ya Kiserikali kuendelea  kusaidia mapambano dhidi ya Ugonjwa huu.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida Victorina Ludovick katika taarifa yake amesema  kikao kilichopita waliadhimia kuendelea kutoa elimu ya chanjo na namna ya kujikinga na Ugonjwa wa Uviko 19.

Dkt. Ludovick amebainisha kwamba wataendelea kuwatumia viongozi wa dini na  wanasiasa katika kupambana na Ugonjwa wa Uviko 19 kwa kuwa imeonekana kukubalika zaidi katika jamii zinazowazunguka.

Aidha uuzaji holela wa barakoa umeendelea kufanyiwa kazi hasa katika maeneo ya karibu na hospitali ambapo wapo wanaojaribisha kwa kuvaa barakoa hizo  kabla ya kununua hivyo kuweza kusababisha maambukizi. Alisema Victorina Ludovick.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mkalama  mkoani hapa Mhe. Sophia Mfaume Kizigo amewataka wataalamu hao wa Afya kuongeza jitihada katika kutoa elimu maeneo ya mijini kwakuwa idadi kubwa ya waliochanja ipo Vijijini na sio mjini.

Hata  hivyo DC huyo alitoa wito kwa kila mwananchi aliyepata chanjo kuwa balozi wa kusaidia uhamasishaji kwa wengine.

Mwisho.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.