• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

TOENI USHIRIKIANO KWA MAKARANI WA SENSA WAKATI WA KUHESABIWA.- RC SERUKAMBA

Posted on: August 17th, 2022

Wananchi Mkoani Singida wametakiwa kutoa ushirikiano mkubwa kwa Makarani na Wasimamizi wa Sensa za watu na makazi ya mwaka 2022 zoezi litakalo anza usiku wa Agosti 23 mwaka huu ili kila mtu aweze kuhesabiwa.

Hayo yamesemwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba wakati akifungua Kongamano la wadau wa Sensa lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Uhasibu Mkoani hapo.

Amewataka wananchi hao kuhakisha wanajiandaa kuhesabiwa na kuandaa taarifa za kila mmoja huku Mkuu wa Kaya akihakikishia anatoa ushirikiano kwa Makarani wa Sensa ili kuwapatia taarifa hizo.

Aidha Serukamba amewataka viongozi Mkoani hapo kila mtu kwa nafasi yake ahakikishe zoezi hilo linafanikiwa kwa kiwango kikubwa, ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha viongozi wa vitongoji na mabalozi ili waweze kuwasadia Makarani kufika maeneo yao ya Utawala.

"Kama mlivyofanya wakati wa anwani za makazi kama mlivyofanya wakati mlipotenga maeneo ya majaribio ya Sensa, basi mkafanye hivyo hivyo wakati wa zoezi la kuhesabu watu. Alisema

Hata hivyo RC Serukamba  amewataka viongozi hao wa kisiasa na kijamii kuendelea kuhamasisha  wananchi kuhusu umuhimu wa kujitokeza kuhesabiwa na kushirikiana na Makarani wa Sensa watakapokuwa wanafanya kazi yao.

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Mwl. Dorothy Mwaluko akizungumza wakati wa kikao hicho

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Singida Mwl. Dorothy Mwaluko akimkaribisha mgeni rasmi amewataka watendaji kuhakikisha wanafuata maagizo na maelekezo yatakayotolewa katika kikao hicho ili kuboresha zoezi hilo.

Aidha Serikali iliamua kuunda kamati hizo zenye mchanganuo wa Wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi watendaji na wakuu wa Wilaya ili kukumbusha wajibu wa kila mmoja katika kutekeleza zoezi la Sensa ya watu na makazi katika maeneo yote ya utendaji na uongozi.

Mratibu wa Sensa Mkoa wa Singida Naing'oya Kipuyo

Awali akitoa taarifa ya utanguli pamoja na utambulisho Mratibu wa Sensa Mkoa wa Singida Naing'oya Kipuyo amesema fedha zote kwa ajili ya kuwalipa Makarani zilishafika na kutumwa kwenye Halmashauri husika ili waweze kuwalipa Makarani na Wasimamizi katika maeneo yao.

Hata hivyo Kipuyo amesema zoezi la ulipaji limekamilika ambapo mpaka jana usiku Halmashauri zilikuwa zinalipa mkononi "cash" walikuwa wameshamaliza kulipa ila wachache ambao malipo yao yalipitia kwenye mabenki waliendelea kupata.


Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.