• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

*WAKULIMA NA WAFANYABIASHARA SINGIDA, WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA STAKABADHI ZA GHALA KWA TIJA*

Posted on: September 6th, 2024

Serikali ya Mkoa wa Singida imewataka wakulima na wafanyabiashara kuendelea kutumia mfumo wa stakabadhi za ghala kwa tija kubwa ili kuwaepusha na walanguzi wa mazao ya biashara na kuimarisha biashara yao.

Akizungumza na Waandishi wa habari, tarehe (6 Septemba, 2024), Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mheshimiwa Halima Dendego, amesema kuwa mfumo huu umeanza kutekelezwa rasmi katika msimu wa 2024/2025 mkoani humo.

Aidha ameeleza kuwa utekelezaji wa mfumo huo unafuatia maagizo yaliyotolewa na serikali kupitia mwongozo wa biashara ya mazao kama dengu, mbaazi, na ufuta, ambao umetolewa chini ya usimamizi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA), Tume ya Ushirika, Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala na Soko la Bidhaa kupitia toleo la tatu la mwaka 2024.

Mkuu wa Mkoa pia alibainisha kuwa mwongozo huu mpya unalenga kudhibiti biashara ya mazao na kuwahakikishia wakulima na wafanyabiashara masoko ya uhakika ndani na nje ya nchi. Kupitia mfumo huu, wakulima watapata bei nzuri kwa mazao yao ikilinganishwa na miaka iliyopita, na hivyo kuongeza mapato yao.

Amefafanua kuwa, bei ya zao la dengu ambayo ilikuwa inauzwa kati ya TZS 900 hadi 1300 kwa kilo katika msimu wa 2023/2024, sasa inauzwa kati ya TZS 1,670 hadi 2,060 kwa kilo katika msimu wa 2024/2025 kupitia mfumo wa stakabadhi za ghala.

Faida nyingine za mfumo huu ni pamoja na ongezeko la mapato kwa halmashauri, udhibiti wa utoroshaji wa mazao, na kutoa uhakika wa takwimu kwa serikali. Mfumo huu pia umewezesha upatikanaji rahisi wa mikopo kwa wakulima na kuongeza masoko ya uhakika ya ndani na nje ya nchi.

Hata hivyo, amesema, ubora wa mazao umeimarika kwa kiasi kikubwa kutokana na mfumo huu ambao unazingatia taratibu na viwango bora vya usafirishaji na uhifadhi wa mazao, pia mfumo wa stakabadhi za ghala umeleta mapinduzi makubwa katika biashara ya mazao mkoani Singida.

Serikali ya Mkoa wa Singida inaendelea kushirikiana na wadau wote muhimu ili kuhakikisha mfumo huu unatekelezwa kikamilifu na kuleta matokeo chanya kwa wakulima na wafanyabiashara. Hii ni hatua muhimu katika kukuza uchumi wa mkoa na taifa kwa ujumla kupitia sekta ya kilimo, ambayo inabaki kuwa uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.