• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

WANAFUNZI NI SALAMA CHINI YA MRADI WA SHULE BORA .

Posted on: May 26th, 2025

Waalimu na wahandisi wametakiwa kutumia vizuri rasilimali zinazotolewa na Serikali katika kukamilisha ujenzi wa madarasa mapya na ambayo ujenzi wake unaendelea kwa viwango vilivyo bora ili kuwawezesha wanafunzi kujifunzia katika mazingira mazuri na wezeshi kwa waalimu kufundishia.

Hayo yamezungumzwa leo Mei 26,2025 Mkoani Singida katika Mafunzo ya siku mbili ya waalimu na Wahandisi kujengeana uwezo juu ya ukamilishaji wa ujenzi wa madarasa katika mradi wa 'Shule Bora' wakijadili juu ya mbinu,taratibu za kutumia kukamilisha ujenzi wa vyumba vipya vya madarasa vilivyosalia kadhalika na suala la mazingira ya Shule za Msingi.

Akifungua kikao hicho,Mwalimu Winfred Chilumba ambae ni mratibu wa Shule Bora kutoka TAMISEMI amewaasa Waalimu na Wahandisi kuhakikisha wanatumia mafunzo hayo katika kuketa tija kwa thamani ya pesa kuonekana kwa lengo la kuhakikisha shule zote zinakua vizuri kwa majengo mazuri yenye viwango zingativu.

"Katika fedha hizi za serikali tunazopokea tuhakikishe tunaonyesha uthamani wake kwa kumuunga mkono Rais wetu katika utekelezaji"amesema Mwl.Chilumba.

Naye Mratibu wa Program hiyo Mkoani Singida,Bwana Fredrick Ndahani amefafanua kuhusu Shule Bora akisema kuwa Programu hiyo inajikita katika maeneo makuu matatu ambayo ni ujifunzaji katika kuhakikisha watoto wanapata nafasi ya kuanza na kuhitimu elimu ya msingi,kadhalika katika ufundishaji katika kuwajengea waalimu uwezo wa namna nzuri ya ufundishaji katika madarasa ya awali na ya msingi na pia katika ujumuishi kwa kuhakikisha hakuna mwanafunzi anakosa kabisa haki ya kusoma bila kujali tofauti zao za kimaumbile au jinsia.

Marrystela Emanuel Ndavi, Mwalimu Mkuu Wa Shule ya Msingi Mwembemoja iliyopo Manispaa ya Singida amesema kuwa mafunzo hayo yanakwenda kuwa na tija kubwa sana kwao kwani wanajifunza mambo mbalimbali yenye manufaa katika kuhakikisha ujenzi bora wa majengo ya shule ikiwemo ujenzi unaozingatia mabadiliko ya tabianchi ikiwemo joto au baridi ili waweze kusoma katika mazingira ya aina zote.

Kadhalika ameainisha sababu za miradi mbalimbali ya ujenzi wa madarasa ya shule kukwama kuwa ni ushirikiano mdogo kutoka kwa wananchi ambao hushindwa kutoa nguvu kazi pale ambapo kazi huanza ikiwemo uchimbaji msingi,kubeba mawe nakadhalika hivyo kusuasua kwa kazi hiyo.

Programu hii  ya elimu  Kitaifa inalenga kuboresha ubora,ujumuishwaji na ujifunzaji salama kwa wasichana na wavulana katika Shule za msingi za Serikali nchini Tanzania na inajumuisha jumla ya Mikoa tisa ikiwemo mkoa wa Singida,Dodoma,Katavi,Kigoma,Mara,Rukwa,Simiyu,Pwani na Simiyu ikijumuisha Halmashauri 67,kata 1450,Shule 5,557 waalimu zaidi  49,000 na wanafunzi milioni nne.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • "SINGIDA IMEJIPANGA KUONGOZA UFAULU KITAIFA":RC DENDEGO

    June 04, 2025
  • MRADI WA TACTIC KULETA NEEMA MANISPAA YA SINGIDA.

    June 02, 2025
  • "WAHITIMU MSIBWETEKE,JIENDELEZENI KATIKA FANI ILI MJIAJIRI"-DKT.MGANGA

    May 30, 2025
  • DKT.MGANGA:"WATUMISHI MSIKUBALI KUTUMIKA VIBAYA,KUWENI NA UTAMBULISHO MZURI"

    May 27, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.