• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

WANAWAKE ACHENI KULALAMIKA MNA UWEZO WA KUINUA UCHUMI; DKT NCHIMBI.

Posted on: March 22nd, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi amewataka akina mama wajasiriamali wote kuacha kulalamika na kutumia fursa zilizopo kujiinua kiuchumi kwakuwa wakati wa kulalamika umeisha na sasa ni kuchapa kazi tu. 

Dkt. Nchimbi ametoa rai hiyo mapema leo wakati akizindua rasmi jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi Mkoa wa Singida na kusisitiza kuwa wanawake sio dhaifu bali watu dhaifu ni wale wanaofikiria mwanamke ni dhaifu. 

Dkt. Nchimbi ameongeza kuwa jukwaa hilo alilolizindua liwe sehemu ya kuwafundisha akina mama mbinu na fursa za uwekezaji pamoja na matumizi mazuri ya fedha wanazozipata hasa mikopo.

Amesema ‘kukopa hakukwepeki katika maisha ya sasa, ila akina mama wengine wanakopa na kuzitumia, vibaya ukiona nguo inapita unanunua wakati haikuwa katika malengo ya mkopo, eti ukishakopa ndio unatamani kula kuku ujionyeshe una pesa, hapana….. kwa namna hii hautaweza kufika popote, hakikisha unabaki katika malengo ya mkopo’.

Dkt. Nchimbi amesema jukwaa liwe jicho la kuhakikisha kuna usalama wa chakula Mkoani Singida kwa kuanzia ngazi ya kila kaya ambapo wanapaswa kuelimisha kaya kuhusu matumizi mazuri ya chakula hasa kulima mazao yanayotumia maji kwa ufanisi na kutunza akiba ya chakula.

Ameeleza kuwa majukumu ya jukwaa hilo ni pamoja na kuangalia namna ya kurejesha maadili ya vijana na kuwakemea ili wasijiingize katika matumizi ya madawa ya kulevya kwakuwa limekuwa tatizo katika maeneo mengi.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi Mkoa wa Singida Bi Neema Salumu ambaye amechaguliwa mara baada ya jukwaa hilo kuzinduliwa amewashuruku wajumbe kwa kumuamini na kumchagua huku akiahidi ushirikiano na kufanya kazi kwa bidii katika kuhakikisha wanawake sehemu ya kukuza uchumi.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Angelina M Lutambi amewashukuru wanawake ambao wametoka katika halmashauri zote saba za mkoa wa singida kwa kushiriki uzinduzi wa jukwaa hilo.

Dkt. Lutambi ameongeza kuwa anasimamia na kutekeleza mambo yote yanayohusu maendeleo hasa yanayolenga kuboresha uchumi wa mwanamke Mkoani Singida kwakuwa anaamini ukimuwezesha mwanamke unajenga uchumi wa taifa.

Wajumbe walioshiriki jukwaa la uwezeshaji wanawake uchumi Mkoani Singida wamepewa elimu ya sheria ya kodi na umuhimu wa kulipa kodi, elimu na upatikanaji wa mikopo pamoja na uhusiano wa wanawake na uchumi wa Tanzania.






Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.