• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

WATUMISHI NA VIONGOZI MKOANI SINGIDA WAPEWA MAFUNZO KUINUA UTENDAJI KAZI

Posted on: December 18th, 2024

Katika kuhakikisha viongozi wanafanya kazi zao Kwa uadilifu na utawala Bora,Madiwani,wakuu wa divisheni na vitengo,wenyeviti wa vijiji,Mitaa na vitongoji  katika Wilaya ya Ikungi na Halmashauri ya Singida wamepatiwa Mafunzo Kwa ajili ya kuboresha utendaji wao wa kazi ili kuwa daraja zuri katika kuwaunganisha wananchi na Serikali.

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ndg.Justice L.Kijazi amefungua mafunzo ya kuboresha utendaji kazi kwa madiwani na wakuu wa divisheni na vitengo katika Halmashauri ya wilaya ya Ikungi.

Mafunzo hayo yameanza tarehe 16 Disemba, 2024 huku yakitarajiwa kuendelea mpaka tarehe 20 Disemba, 2024 ambapo Halmashauri imeandaa mafunzo ya ujazaji tamko la maadili kwa viongozi kufuatia matakwa mapya ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa umma ya ujazaji wa tamko la rasilimali na madeni kwa viongozi wa umma kwa njia ya mfumo kwa mujibu wa sheria.

"Tumealika viongozi kutoka taasisi mbalimbali ili kutoa mada kuhusu uboreshaji utendaji kazi wetu hivyo tutakuwa na mada kutoka taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) na tamko la rasilimali na madeni na masuala ya serikali za mitaa" amezungumza Kijazi 

Mkurugenzi Mtendaji ameongeza na kusema kuwa mwisho wa kujaza Tamko la maadili ni tarehe 31 Disemba, 2024.

Kwa upande wao baadhi ya wajumbe katika mafunzo hayo wameishukuru Halmashauri kwa kutenga bajeti kwa ajili ya mafunzo hayo kwani yanaenda kuwa chachu katika utendaji kazi katika maeneo yao.

Lengo la mafunzo hayo ya siku 5 nii kuwawezesha viongozi hao kujifunza maswala ya utawala bora kwa maslahi mapana ya wananchi wa wilaya ya Ikungi na mkoa wa Singida kwa ujumla.

Kwa upande mwingine Wenyeviti wa Vitongoji na Vijiji  kutoka katika halmashauri ya Singida wamepatiwa mafunzo ya Uongozi kwa lengo la kuwajengea uwezo viongozi katika maswala ya uongozi ili kuleta Maendeleo kwa wananchi na kuisaidia Serikali yanayofanyika Kwa siku mbili Disemba 18 na 19,2024 katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Ilongero.


Mafunzo hayo yanayoratibiwa na Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ( OR-TAMISEMI),yameandaliwa na uongozi wa Halmashauri na kutolewa na wawezeshaji kutoka katika Chuo cha Serikali za Mitaa cha Hombolo.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo ambaye ni Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida,Bw.Shabani Mongomongo amewapongeza wenyeviti wa Vitongoji na Vijiji kwa kuaminiwa na   kuchaguliwa kuwaongoza wananchi akiwasihi  kusimamia misingi ya uongozi pasipo kuingiliana katika utendaji kazi.Sambamba na hilo,ametoa Pongezi kwa Chuo Cha Hombolo kwa kukubali kutoa mafunzo hayo.

       Jumla ya wenyeviti wa vijiji 84 na wenyeviti wa vitongoji 435 wanatarajiwa kupata mafunzo hayo ambayo yatatolewa kwa siku mbili.


Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • "SINGIDA IMEJIPANGA KUONGOZA UFAULU KITAIFA":RC DENDEGO

    June 04, 2025
  • MRADI WA TACTIC KULETA NEEMA MANISPAA YA SINGIDA.

    June 02, 2025
  • "WAHITIMU MSIBWETEKE,JIENDELEZENI KATIKA FANI ILI MJIAJIRI"-DKT.MGANGA

    May 30, 2025
  • DKT.MGANGA:"WATUMISHI MSIKUBALI KUTUMIKA VIBAYA,KUWENI NA UTAMBULISHO MZURI"

    May 27, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.