• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

WAZIRI MKUU AHITIMISHA ZIARA MKOANI SINGIDA, AWAAGIZA WAKUU WA WILAYA KUSIMAMIA FEDHA ZA MAKUSANYO

Posted on: August 6th, 2022

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, amewaagiza Wakuu wa Wilaya kuhakikisha wanasimamia Watumishi wote katika Halmashauri za Mkoa wa Singida ambao walikusanya fedha za mapato lakini hawakuzipeleka benki wanazirudisha haraka.

Ametoa agizo hilo leo kwenye kikao cha majumuisho ya ziara yake ya siku mbili mkoani hapa wakati akizungumza na Watumishi wa Halmashauri za Wilaya ya Singida, Ikungi na Halmashauri ya Manispaa ya Singida.

Alisema kumekuwa na tatizo kubwa kwenye Halmashauri nyingi nchini katika ukusanyaji wa mapato ya ndani ambapo baadhi ya Watumishi wanapokusanya fedha haziingizwi kwenye mfumo wa Serikali jambo ambalo limekuwa kero kubwa.

"Wakuu wa Wilaya hakikisheni Watumishi wanaodaiwa fedha wazirudishe haraka, Iramba, Manyoni na hata Ilongero (Halmashauri ya Wilaya ya Singida) nimepewa orodha ya Watumishi ambao wanadaiwa fedha za makusanyo," alisema.

Majaliwa alisema Rais Samia Suluhu Hassan amekuwa akisisitiza suala la ukusanyaji wa mapato na hata majuzi wakati anawaapisha wakuu wa mikoa lakini cha kushangaza baadhi ya Watumishi wa umma wamegeuka kuwa wabadhirifu.

Alisema ujanja unaofanywa na baadhi ya Watumishi kufuja fedha za makusanyo ni kwamba wanapokusanya fedha hasa wanapobaini ni nyingi wanazima mashine ili zisiingie kwenye mfumo wa Serikali.

Aidha, Waziri Mkuu amewataka Watumishi kuacha urasimu katika utendaji wa kazi kwani mambo hayo ndio yanakaribisha vitendo vya rushwa chini.

Kuhusu idara za manunuzi, alisema limekuwa ni tatizo kubwa ambapo Idara hizo zimekuwa zikiweka makadirio makubwa ya bei za manunuzi ya vifaa vya ujenzi kwenye miradi hususani inayotumia 'force account'.

Aliongeza kuwa kwenye Halmashauri kumekuwa na tatizo kubwa la usimamizi wa miradi inayotekelezwa na kwamba kuna umuhimu kwa Watumishi kuhakikisha suala hili linapewa umuhimu wa juu.

Alisisitiza suala la mahusiano kwa Watumishi wa Umma mahali pa kazi kwani kufanya hivyo kutaboresha utendaji kazi na kuleta ufanisi mkubwa katika kuwatumikia wananchi.

Aidha, alizitaka Halmashauri kuratibu vizuri suala la wafanyabiashara wadogo maarufu wamachinga ili wapewe maeneo ya kufanyia biashara zao bila usumbufu.

Waziri Mkuu (kushoto) akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Singida

Awali Waziri Mkuu aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Singida linalojengwa Ilongero katika kijiji cha Mwahango kwa thamani ya Sh. 2.7 bilioni.

Akizungumza na wananchi wa eneo hilo, alimwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Ester Chaula, kuisimamia idara ya manunuzi ili ujenzi wa jengo hilo uweze kukamilika na kuanza kutumika.

"Nimeridhishwa na ujenzi unavyoendelea, DED (Mkurugenzi wa Halmashauri) isimamie idara ya manunuzi, wasikuvuruge, mkandarasi alipwe fedha zake, " alisema.

Akiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Singida inayojengwa kwa Sh. bilioni 19.5 Waziri Mkuu, alisema ujenzi wa hospitali hiyo itakuwa mkombozi mkubwa kwa wananchi wa mkoa huu na mikoa jirani.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,(kushoto) akimpa mkono wa pongezi Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba mara baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Singida

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.