• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

Waziri Ummy awataka Madiwani nchini kuacha mivutano isiyo na tija katika utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo

Posted on: December 22nd, 2021

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Ummy Mwalimu, ameyataka mabaraza ya Madiwani nchini, kupitia vikao vyake kuhakikisha yanafanya maamuzi sahihi yenye tija kwa jamii, badala ya maslahi binafsi yanayosababisha mivutano isiyo na tija.

Mheshimiwa Ummy amesema hayo leo Disemba 22, 2021 wakati akikagua ujenzi wa kituo cha afya cha Kata ya Ilunda, wilaya ya Mkalama mkoani Singida, ambacho Madiwani wa halmashauri ya wilaya hiyo wanapinga ujenzi wake wakitaka kijengwe Kata ya Gumanga huku maagizo ya Serikali yakiwa kijengwe Kata ya Ilunda.

Waziri Ummy, amesema kituo hicho ni muhimu kwa Kata ya Ilunda kutokana na eneo hilo kukosa huduma sahihi za afya kwa muda mrefu na kitahudumia Kata Nne zilizopo wilayani humo.

“Niwaombe waheshimiwa Madiwani tuache mivutano katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo sisi tulichagua kituo cha afya kijengwe katika Kata ya Ilunda kwasababu kitahudumia Kata Nne. Tunaangalia kipi kitaleta tija ya haraka. Tunajua maamuzi yanafanywa na mabaraza ya madiwani lakini tufanye maamuzi yenye tija.” Amesema Mhe. Ummy Mwalimu

Aidha kutokana na mvutano huo uliokuwa ukichelewesha ukamilishwaji wa kituo pamoja na uidhinishaji wa fedha za ujenzi huo kutoka benki, Waziri Ummy akamwagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dorothy Mwaluko, kuhakikisha anachukua jukumu hilo, ili mradi uweze kukamilika kwa wakati.

“Nafahamu mpaka leo (22/12/2021) Mwenyekiti amekataa kusaini mikataba ya ujenzi, Mimi nampa mamlaka Katibu Tawala wa Mkoa ya kusaini. Hatuwezi kuchelewesha ujenzi wa kituo hiki wakati fedha imekuja tangu mwezi wa Nane”. Alisisitiza Mhe. Ummy Mwalimu

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge, amemhakikishia Waziri kuwa Ujenzi wa kituo hicho utakamilika kwa wakati na kuanza kutoa huduma kwa wananchi pamoja na miradi mingine ya maendeleo inayoendelea kujengwa nkoani humo.

Hata hivyo amemshukuru na kumpongeza Waziri wa TAMISEMI kwa kuhitimisha ziara yake ya siku TATU ya kukagua Miradi ya maendeleo, Elimu, Afya na Miundombinu sambamba na kikao na Sekretarieti ya Mkoa pamoja na vikao na mabaraza ya Madiwani katika halmashauri za Mkoa.

Nao wananchi wa Kata hiyo akiwemo Hawa Gyimbi, Oscar Daudi na Josephine Maige, wamefurahishwa na uamuzi huo unaoenda kumaliza tatizo la kufuata huduma za afya umbali mrefu jambo ambalo lilikuwa likiwatesa kwa miaka mingi.

Katika hatua nyingine, Waziri Ummy, amewapongeza Watendaji wa Halmashauri hiyo pamoja na Mkoa kwa jitihada walizozifanya kuhakikisha ujenzi huo unaendelea kwa kasi na kuwataka ukamilishwaji kwa wakati ili huduma za afya zianze kutolewa kwa wananchi hao.

Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama yenye jumla ya zahanati 34, vituo vya afya vinne na hospitali mbili, ilianzishwa mwaka 2013, baada ya kugawanya kutoka wilaya ya Iramba.

MWISHO.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.