• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

CHANGAMOTO ZA WAFUGAJI NA WAVUVI SINGIDA ZAANZA KUPATIWA UFUMBUZI

Posted on: January 10th, 2026

Wananchi wa Wilaya za Iramba na Mkalama mkoani Singida wameeleza matumaini mapya baada ya ziara ya kikazi ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Bashiru Kakurwa (Mb), iliyofanyika leo tarehe 10 Januari 2025, wakisema imefungua fursa ya kusikilizwa na kushughulikiwa changamoto zinazowakabili katika sekta ya mifugo na uvuvi.

Katika Wilaya ya Iramba, wananchi na viongozi wa wilaya walieleza kuwa uchumi wa eneo hilo unategemea kwa kiasi kikubwa ufugaji na uvuvi katika Ziwa Kitangiri. Mkuu wa Wilaya alibainisha kuwa wilaya ina idadi kubwa ya mifugo lakini bado inakabiliwa na upungufu wa miundombinu ya kisasa kama machinjio, minada na majosho, pamoja na uhaba wa watumishi wa mifugo na uvuvi. Alisema hali hiyo imekuwa ikiwalazimu wananchi kutumia gharama kubwa kupata huduma na wakati mwingine kushindwa kufikia masoko yenye tija.

Afisa Uvuvi wa wilaya alieleza kuwa shughuli za uvuvi zinaendelea kufanyika licha ya changamoto za vifaa na rasilimali, akibainisha kuwa wilaya ina wavuvi hai 204, mitumbwi 34 iliyosajiliwa na boti moja pekee. Alisema bado kuna hitaji kubwa la kuimarisha usimamizi wa rasilimali za uvuvi, kutoa elimu ya uvuvi endelevu kwa wananchi na kuboresha miundombinu ya uvuvi ili kuongeza tija na kipato cha wavuvi.

Katika Wilaya ya Mkalama, Mkuu wa Wilaya alisema migogoro ya wakulima na wafugaji imekuwa changamoto ya muda mrefu, hasa katika maeneo ya mipakani, akisisitiza kuwa kuwekwa kwa mipaka rasmi kati ya Wilaya ya Mkalama na Meatu ni hatua muhimu ya kudhibiti migogoro hiyo. Aliongeza kuwa kuna haja ya kulifufua shamba la mifugo la Serikali lililotelekezwa na kuvamiwa, ili kulinda mali ya umma na kutoa mfano wa ufugaji wa kisasa kwa wananchi.

Wananchi wa Kijiji cha Nyahaa walieleza kero zao kuhusu uvamizi wa mifugo, wizi na migogoro iliyosababisha majeruhi na hasara za mali, wakisisitiza umuhimu wa Serikali kuchukua hatua za haraka kurejesha amani na kuimarisha ulinzi wa mifugo.

Kwa ujumla, wananchi walisema ziara hiyo imeongeza uwazi na matumaini mapya, huku viongozi wa wilaya na wataalamu wa sekta wakisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali na wananchi ili kuboresha huduma za mifugo na uvuvi na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika mkoa wa Singida.


Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • MAAFISA UGANI WAASWA KUWA WATATUZI KERO ZA WAKULIMA SHAMBANI

    February 02, 2026
  • TSH. 27,000/- PEKEE KUWASHA UMEME KILA KAYA.

    February 03, 2026
  • SINGIDA YAWEKA MKAZO KILIMO CHA ALIZETI NA MALEZI BORA KWA WATOTO

    February 01, 2026
  • "KILA MMOJA ALINDE ENEO LAKE NA KUFUATA SHERIA" - RC DENDEGO

    January 27, 2026
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.