• Contact Us |
    • Complaints |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Blog |
Singida Regional Website

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Singida Regional Website

  • Home
  • About Us
    • History
    • Vision and Mission
    • Regional Leaders
  • Administration
    • Regional Secretariet Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Planning and Coordination
      • Economy and Production
      • Infrustructure
      • Local Government
      • Health
      • Education
      • Water
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Services
      • Procurement and Supply
  • Districts
    • Ikungi
      • HISTORIA
    • Iramba
    • Manyoni
    • Mkalama
    • Singida
  • LGA
    • Ikungi DC
    • Iramba DC
    • Itigi DC
    • Manyoni DC
    • Mkalama DC
    • Singida DC
    • Singida MC
  • Investiment Opportunity
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Mining
  • Our Services
    • Health
      • Medical Specialists
      • Clinical Services
      • Preventive Care
      • Social Welfare
      • Environmental Health
      • Nutrition
    • Education
    • Water
    • Agriculture
  • Publications
    • Bylaw
    • Customer Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • Investment Guide
  • Media Center
    • Gallery
    • Videos
    • Speeches
    • Press Release

Chuo cha VETA kijengwe Manyoni - RC Serukamba

Posted on: April 5th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba leo tarehe 5 Aprili, 2023 amemaliza mgogoro wa eneo kitakapojengwa Chuo cha Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kwa kufikia maamuzi kwamba chuo hicho kujengwa katika eneo la Manyoni Makao makuu ya Wilaya.

Maamuzi hayo ameyatoa katika  kikao kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni na kuwakutanisha wenyeviti wa Halmashauri zote za Wilaya hiyo, Wabunge wa Manyoni, Madiwani wa Halmashauri ya Itigi na Manyoni, Kamati ya Siasa ya Wilaya na ya Mkoa na Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya na mkoa.

RC Serukamba alipitisha uamuzi wa Chuo hicho kujengewa katika eneo la Setelite Manyoni karibu na eneo la mnada  baada ya kuwahoji Madiwani wa upande wa Manyoni na Itigi na kubaini kwamba hapakuwa na ushirikishwaji katika upatikanaji wa eneo lililopendekezwa mwanzoni ambalo ni Kintiku Lusilile.

Madiwani pamoja na Wabunge walilazimika kupiga kura ya wazi kwamba ili kuamua chuo hicho kujengewa wapi kati ya Kintinku, Lusilile au Manyoni Setalite ambapo kura 10 zilitaka kijengwe Lusilile, 4 zilitaka kijengwe Itigi na kura 32 zilitaka kijengwe Manyoni.

Aidha Serukamba alieleza kwamba eneo hilo lipo katikati hivyo ni rahisi kufikiwa na wananchi wa maeneo yote ya Wilaya hiyo,

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba akitoa taarifa ya kura zilizopigwa wakati wa kikao hicho.

"Maoni ya wengi ni Maoni ya Mungu kwa kuwa wengi wameona chuo hicho kijengwe Manyoni lazima tufanye hivyo ili kiweze kuwasaidia wananchi kutoka pande zote, na wote naomba tuweze kusimamia hili," Alisema Serukamba

Hata hivyo amemuagiza Mkuu wa Wilaya hiyo kuhakikisha eneo hilo linapimwa na wakabidhiwe Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kati kwa ajili ya kuanza hatua za Ujenzi.

Hata hivyo amewataka Viongozi wa Wilaya hiyo kuandaa ziara katika kata zilipotakiwa kujengwa chuo hicho na kuwaelimisha sababu za msingi za kuhamishwa ujenzi huo.

Awali Mkurugenzi wa VETA kanda ya Kati John Mwanja, alieleza sifa ya eneo linalotakiwa kujengwa chuo cha VETA kwamba lisiwe na migogoro, kusiwepo na fidia lisiwe chini ya ekari 20.

MATUKIO KATIKA PICHA

Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba akimsikiliza Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni Mhe. Jumanne Shabani Mlagaza, wakati akitoa maoni yake kuhusu eneo litakapojengwa chuo cha VETA Manyoni.

Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kati Dodoma, John Mwanja akitoa ufafanuzi kuhusu sifa za eneo linalopaswa kujengwa chuo cha VETA wakati wa kikao hicho kilichoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida.

Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Kemilembe Lwota akizungumza wakati wa kikao hicho.

Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki, Dkt.Pius Chaya akizungumza wakati wa kikao hicho.

Mbunge wa Manyoni Magharibi Yahaya Masare, akizungumza wakati wa kikao hicho.

Announcements

  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2022_2023 SINGIDA RS July 01, 2022
  • MAJINA YA WALIOCHANGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA - 2023, MKOA WA SINGIDA December 14, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KWA KIPINDI CHA KUANZIA JULAI HADI OCTOBA, 2023 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO November 01, 2023
  • GENERAL PROCUREMENT NOTICE FOR YEAR 2021/2022 SINGIDA RS - GPN 2021 - 2022 July 01, 2021
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI MIRADI SINGIDA DC,MHE DENDEGO ATOA MAAGIZO

    May 13, 2025
  • KAMATI YA LISHE YAJA NA MIPANGO KABAMBE YA UTEKELEZAJI SINGIDA

    May 12, 2025
  • HUDUMA ZA KIBINGWA ZAWAFIKIA WAGONJWA ZAIDI YA 3000 SINGIDA.

    May 09, 2025
  • IKUNGI YAPEPERUSHA BENDERA KWA MIRADI YA KIMKAKATI.

    May 08, 2025
  • View All

Video

Mkoa wa Singida waja na Mikakati ya Kuboresha Elimu
More Videos

Quick Links

  • Press Release
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • Fomu ya Maombi ya Kusafiri Nje ya Nchi
  • SINGIDA RS PROCUREMENT NOTICE
  • KUONA AJIRA ZA WAALIMU WA SAYANSI NA MAFUNDI SANIFU

Related Links

  • UTUMISHI
  • TAMISEMI
  • IKULU
  • WIZARA YA ELIMU
  • NECTA
  • WIZARA YA AFYA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    SINGIDA

    Postal Address: P O BOX 5 SINGIDA

    Telephone: 2502170, 2502089

    Mobile: 2502170, 2502089

    Email: info@singida.go.tz ras@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2023 Singida Regional Commisioner' Office . All rights reserved.